#COVID19 Askofu Gwajima: Ni ujinga kuruhusu Taifa zima kuwa 'Experiment' kwa sababu tuna haraka ya Corona

Hivi huyu mbulula anasoma conspiracy theories anapeleka Bungeni. Hakuna kanuni inayozuia kuongea mambo yasiyo ya kiutafuti bungeni? Hivi hizi akili kumbe huwa ni za Kisukuma maana Hayati nae yalikuwa mawazo yake

Sent from my vivo 1915 using JamiiForums mobile app

Wameaminishwa na kina msukuma kuwa hata darasa la 7 ni bora kuliko wasomi.
 
Mbunge wa Jimbo la Kawe, Askofu Josephat Gwajima ametaka kuwepo umakini wa kuchagua Chanjo dhidi ya Ugonjwa wa COVID-19. Amesema hayo akiwa Bungeni Dodoma leo wakati wa Mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Afya iliyowasilishwa na Waziri Dorothy Gwajima.

Amefafanua, "Mimi sipo kinyume na Chanjo za Corona wala Chanjo yoyote. Mtu asininukuu napinga Chanjo, hapana! Tanzania tulishachanjwa Chanjo ya Kifua Kikuu, Surua, Kifaduro na Polio".

Amesema ni kweli Tanzania ikikataa Chanjo inaweza kuwekewa zuio la kwenda Ulaya. Ameeleza, "Tunakabiliwa na uchaguzi mbaya sana, tuchanjwe kitu tusichokijua sawa sawa au tusichanjwe tuzuiwe kwenda Ulaya".

Ameiomba Wizara ya Afya kuangalia suala la Chanjo kwa umakini, akisema waangalie madhara ya sasa, ya siku zijazo na ya Taifa. Ameongeza kuwa, tatizo lililopo ni kufikiri kila kinachotoka Ulaya kinafaa.

Amesema, "Before we venture into what kind of vaccine we should take, tunatakiwa tuwe na wataalamu wetu wa hapa".


Kuna Watanzania wanapenda ushabiki badala ya kusikiliza Madaktari wa watu wana sikiliza madaktari wa mapambio! Tena eti wenye kudanganya walalahoi wanauwezo wa kusalia watu waliokufa na kufufuka. Wale wanao waambia waumini pesa yao ya mapato asilimia 10% ya zaka inaenda kwa Mungu kumbe inaenda kununua ndege na helikopta binafsi. Tuacheni ujinga wa kusikiliza matapeli tumechoka kufanywa wajinga na huyu jamaa
 
Gwajima ametoa hoja, badala ya kuchangia hoja kwa kukosoa au kuongezea nyama unaanza kumjadili mtoa mada, sasa una akili au matope

Huwezi kuwa na hoja katika eneo usilokuwa na ujuzi nalo. Kwamba wewe umeona hoja ya "microbaolojia na virusi" tokea kwa Gwajima asiyekuwa na mbele wala nyuma kwenye eneo hili? Wewe una akili au matope?

Haya si ndiyo mambo ya nyungu?

Kwenye masuala hayo, tunawasikiliza hawa:

"Akizungumza na Mwananchi, Mtaalamu wa maicobaolojia na virusi kutoka Chuo kikuu cha Muhimbili (Muhas), Dk Joel Manyahi alisema aina hiyo ya kirusi kina tabia ya kujibadilisha mara kwa mara."

Wenye bahati zao.

Kina Gwajima hata kama wakikaa kimya tu, kwenye masuala haya hawana tofauti na kina msukuma au hata wale very illitrates vijijini ambao hawakwenda shule kabisa.
 
Gwajiboy kaongea point.
Ushauri wake ufanyiwe kazi
Hatutakiwi kuchukulia issue ya chanjo kama fashion lazima tujiridhishe na hii issue iwe ni hiyari ya mtu, isiwe lazima
Nakazia...

HII KITU IWE NI HIARI YA MTU ISIWE LAZIMA hasa kwa sisi watumishi wa ngazi za chini ambao tumekuwa tukifanywa chambo kwa kila kitu
 
Mkuu ila pamoja tz not covid 19 free country lakini Hata ingekua free on covid 19 lazima taifa kujikita na kuatayari katika hatua zote za prevention namanisha
Primary prevention
Second prevention
Tertiary prevention and no way as anation we can escape to take measures as far as covid is concerned
What have we done to protect our people from dying ....secondary to HIV,MALARIA,DIABETES,HEART DESEASES AND MATERNAL DEATHS?
 
Mbunge wa Jimbo la Kawe, Askofu Josephat Gwajima ametaka kuwepo umakini wa kuchagua Chanjo dhidi ya Ugonjwa wa COVID-19. Amesema hayo akiwa Bungeni Dodoma leo wakati wa Mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Afya iliyowasilishwa na Waziri Dorothy Gwajima.

Amefafanua, "Mimi sipo kinyume na Chanjo za Corona wala Chanjo yoyote. Mtu asininukuu napinga Chanjo, hapana! Tanzania tulishachanjwa Chanjo ya Kifua Kikuu, Surua, Kifaduro na Polio".

Amesema ni kweli Tanzania ikikataa Chanjo
inaweza kuwekewa zuio la kwenda Ulaya. Ameeleza, "Tunakabiliwa na uchaguzi mbaya sana, tuchanjwe kitu tusichokijua sawa sawa au tusichanjwe tuzuiwe kwenda Ulaya".

Ameiomba Wizara ya Afya kuangalia suala la Chanjo kwa umakini, akisema waangalie madhara ya sasa, ya siku zijazo na ya Taifa. Ameongeza kuwa, tatizo lililopo ni kufikiri kila kinachotoka Ulaya kinafaa.

Amesema, "Before we venture into what kind of vaccine we should take, tunatakiwa tuwe na wataalamu wetu wa hapa".
Hizo chanjo alizochanjwa zamani alizijua na alizifanyia utafiti kwanza kabla ya kuchanjwa na zilimletea madhara gani mpaka aanze kuwa na wasiwasi? Kwenye haya mambo ya kitaalamu lazima tuwe na trust na honesty pia maana hatutawezi kuthibitisha kila kitu. Ndiyo maana tukienda hospitali tukiambiwa tunaumwa na tunatakiwa tutumie dawa fulani ili tupome, tuna'trust' maana hatuwezi kuthibitisha (hatuna utaalamu huo). Huu ni muda mzuri wa kuimarisha urafiki wetu na marafiki wetu wa enzi na enzi na ambao hawajawahi kutufanyia ubaya wowote. Sidhani kama kwa sababu ya Covid-19 wamegeuka kuwa wabaya kiasi cha kuanza kuwatilia mashaka kama ambavyo kauli mbalimbali zilikuwa zikitolewa hapo nyuma. Nilimsikia wakati fulani (kama wiki 2 au tatu zilizopita) kuhusu hizi chanjo, nikashangaa sana. Alikuwa ana'speculate' mambo na nilishangaa sana kuona wahubiriwa walikuwa tu wakipiga makofi na kushangilia na kwa kufanya hivyo aliendelea kuwafunga kamba utadhani alishafanya utafiti wowote wa kumfanya aanze kuzitilia mashaka. Tujitafakari!
 
Watu laki 5 kwa miaka 70 (tokea chanjo ya YF ianze kutumika) na diniani in watu billioni 7, unajikuta vifo vya homa ya majano kidogo sana. Sasa unaweza kukadiria kama chanjo ya Corona inaweza kuuwa watu wangapi katika miaka 70 ijayo? Jibu ni gumu kwasababu hatujuwi madhara ambayo hizi chanjo za dharula yatazilita kwenye miaka ya usoni.

Kuna watu wamesha ambukizwa Corona na wengine kufa kwa Corona na huku wakuwa na chanjo zote mbili lakini takwimu hizo hazitolewe na WTO wala makampuni yanyotengenza hizo chanjo kwa kuofia kuvurukika kwa biashara yao na pia kutowatia hofu watu ambao bado haja chanjwa.

Sawa dawa na tabibu zote zina madhara yake (side affects), kakini hizo tiba hazikutegenezwa leo na kuuzwa kesho. Tunaonglea si chini ya miaka kumi kwa dawa kuwa salama kwa matumizi ya mwanadamu.

Na swala la mwisho kwanini nchi zinazo tengeneza hizo dawa wanalazimisha kwa nguvu nchi masikini wanunuwe chanjo zao na ukikataa wanakuwekea vikwazo vya uchumi?
Nchi gani imelazimisha chanjo zake zinunuliwe? Mbona Russia na China wametengeneza za kwao na WHO imewapa endorsement?

Okay unasema vifo laki 5 kwa miaka 70 ni halali ila vifo 50 kati ya watu million zaidi ya 30 waliochanjwa kwa Astra Zeneca ndio sample nzuri ya kudiscredit chanjo?

Kingine chanjo sio tiba na hapa ndio mnakosea.... Chanjo ni kama condom tu inazuia maambukizi ila yakipenya haiwezi kukuokoa tena!! Hata ARVs kuna watu wanatumia na bado wanakufa kwa maradhi ya VVU so its not a big deal to be honest
 
Point yako haina mashiko, chanjo ya homa ya manjano imekuwepo kwa zaidi ya miaka 70, na tafiti nyingi zimefanyika zikishirikisha nchi nyinyi Tanzania ikiwemo. Leo hii nionyeshe nchi ambayo inazalisha chanjo ya Corona walikubali kumshirikisha mtu au nchi yoyote ambayo inanunua chanjo ya corona. Unachopewa ni chanjo na kuambiwa tuambia hao uliowachanja wamepata madhara gani. kwa kifupi we are guinea pigs na mtu kama wewe unakubali tu. Nchi kama Kenya na Rwanda walikuwa wanashangilia walipopewa chanjo, soon after, side effects zikanaza kujitikeza kila kona. Leo hii wao wanahali mbaya kuliko sisi ambao we didn't care less.
Acha kupotosha watu aliyekudanganya Kenya na Rwanda wamepata shida na chanjo ni nani. Mmemponza ndugu yenu mpaka corona imemla kichwa
 
hivi watalaamu wetu wa ndani wana capacity ya kujua ubora, udhaifu, madhara, faida ya cnanjo zilizopo kwa sasa na years to come?

Hawana uwezo wowote wa kufanya chochote zaidi ya kutuambia waliojifunza kupitia peer review. Kama wanaweza kuwa kimya karibu miezi sita toka habari za chanjo zianze, umuhimu wao haupo tena!! Magonjwa hatari miezi sita inatosha kabisa kuleta madhara makubwa. Ungonjwa huu umeanza 2019, sasa 2021 bado hata hawajasema wamegundua kitu kimoja!!! Wanakuja na ushauri wa NIMCARF, Covidol, nyungu huku wakiita ugonjwa huu “changamoto ya upumuaji”.

Kwa ujumla Gwajima ana point - kama anayosema ndio yangekuwa yanatokea. Tutaingia kwenye chanjo ya covid kama tulivoingia kwenye za polio, dondakoo, surua, kifaduro nk. Hatukufanya utafiti wa hizo!!!
 
COVID-19 ilikuwepo Kenya 🇰🇪, Uganda 🇺🇬, Rwanda 🇷🇼 na nchi nyingine zinazotuzunguka na ulimwenguni kote.

Na nchi zote hizo tayari walishatumia chanjo ya kuangamiza COVID-19 kwa kukiri kuwa COVID-19 ipo na inauwa.

Sasa kwa upande wa Tanzania 🇹🇿, hizo taarifa za uwepo wa COVID-19 zinasemaje?

Kwa sababu COVID-19 ni janga la dunia "GLOBAL PANDEMIC", kwanini Tanzania 🇹🇿 ikimbilie kwenye chanjo bila kukiri uwepo wa COVID-19?
Chanjo si unajikinga tu bila kujali ugonjwa upo ama haupo!! Ni precautionary motive tu na ndio alichosema Rais kwamba hata kma Covid Haipo Tz ila wave ikija lazima ikute mmejiandaa.
 
Hivi unajua kuwa wataalamu wanapuuzwa na corona inapelekwa kisiasa zaidi kuliko kisayansi? Kasome kitabu cha Corona False Alarm? Fact and figures.
Mkuu ww hujawahi kuamini Covid 19 ipo..... Nili conclude kwamba utaamini siku Ikimpata ndugu yako wa karibu akafia mikononi mwako ICU bila kupewa chance ya kumuaga ndio utakiri kuwa it's real.
 
Hivi Corona ipo au haipo kwa upande wa Tanzania?

Sasa hivi tunashuhudia chanjo! Wakati mwanzo Tanzania ilisema inafanya tafiti!

Majibu ya hiyo tafiti bado tu? Au kuna mengine nyuma ya pazia!

Na kama tafiti bado, kwanini Tanzania ikimbilie kwenye chanjo.

Kama Corona ipo siitangazwe tujue moja!

Kuliko kuficha ficha huku Watanzania wengi wakiendelea kupukutika.
Watu washasaini mkataba wa mkopo we unaulizia haya sahizi! Tulieni mtiwe astra zeneca muanze kupuputika!
 
Huyu Mnafiki kwenye yale mabanda yake anayojiita ni kanisa anawadanganya wapuuzi wanaomfata eti Chanjo ya Corona ni Alama ya Mnyama, Mpinga Krist
Health education as primary prevention,drugs priscription(ant malaria,ant dm,ART ,ant hypertensive ) as secondary prevention ,mnx of complications associated mentioned conditions to avoid disiabililities as tertiary prevention
What have we done to protect our people from dying ....secondary to HIV,MALARIA,DIABETES,HEART DESEASES AND MATERNAL DEATHS?
 
Mbunge wa Jimbo la Kawe, Askofu Josephat Gwajima ametaka kuwepo umakini wa kuchagua Chanjo dhidi ya Ugonjwa wa COVID-19. Amesema hayo akiwa Bungeni Dodoma leo wakati wa Mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Afya iliyowasilishwa na Waziri Dorothy Gwajima.

Amefafanua, "Mimi sipo kinyume na Chanjo za Corona wala Chanjo yoyote. Mtu asininukuu napinga Chanjo, hapana! Tanzania tulishachanjwa Chanjo ya Kifua Kikuu, Surua, Kifaduro na Polio".

Amesema ni kweli Tanzania ikikataa Chanjo inaweza kuwekewa zuio la kwenda Ulaya. Ameeleza, "Tunakabiliwa na uchaguzi mbaya sana, tuchanjwe kitu tusichokijua sawa sawa au tusichanjwe tuzuiwe kwenda Ulaya".

Ameiomba Wizara ya Afya kuangalia suala la Chanjo kwa umakini, akisema waangalie madhara ya sasa, ya siku zijazo na ya Taifa. Ameongeza kuwa, tatizo lililopo ni kufikiri kila kinachotoka Ulaya kinafaa.

Amesema, "Before we venture into what kind of vaccine we should take, tunatakiwa tuwe na wataalamu wetu wa hapa".
Swali ni je, tuna wataalamu au utaalamu wa kutambua chanjo ipi ni salama na ipi si salama? Otherwise naunga mkono hoja.
 
Back
Top Bottom