Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 4,783
- 14,975
Mara baada ya kusambaa kwa Barua mitandaoni iliyodaiwa kuwa imetoka kwa Msajili wa Jumuiya za Kiraia, Emmanuel Kihampa ikihusu kufungia shughuli za Kanisa la Glory of Christ Tanzania (Kanisa la Ufunuo na Uzima), Kiongozi wa Kanisa hilo, Askofu Josephat Gwajima amesema kuna Mtu amefika Kanisani hapo kwa lengo la kuleta barua jioni ya leo Juni 2, 2025
Amesema “Nikiwa kwenye ibada Wasaidizi wangu wamesema kuna Mtu alifika akasema ameagizwa kuleta barua, hawakuipokea, kitambulisho na taarifa zake tunazo, amesema atarudi kesho, tunamsubiri.”
Ameongeza “Hapa nipo na Maaskofu na Viongozi wengi wa Dini wote wanahoji kuhusu hiyo barua iliyosambaa Mtandaoni ambayo nilieleza kuwa siyo ya kweli kwa kuwa sikuwa nimepokea barua yoyote na ilizua taharuki kwamba Kanisa letu limefungiwa.”
Soma Pia: Serikali yalifutia usajili Kanisa la Askofu Gwajima kwa kuingilia masuala ya siasa kwa nia ya kuichonganisha Serikali na Wananchi
Awali, barua hiyo ambayo hakuna Mamlaka iliyojitokeza kuizungumzia ilieleza Kanisa hilo limefungiwa kwa maelezo ya kutoa mahubiri yenye mwelekeo wa Kisiasa na nia ya kuichonganisha Serikali na Wananchi
Amesema “Nikiwa kwenye ibada Wasaidizi wangu wamesema kuna Mtu alifika akasema ameagizwa kuleta barua, hawakuipokea, kitambulisho na taarifa zake tunazo, amesema atarudi kesho, tunamsubiri.”
Ameongeza “Hapa nipo na Maaskofu na Viongozi wengi wa Dini wote wanahoji kuhusu hiyo barua iliyosambaa Mtandaoni ambayo nilieleza kuwa siyo ya kweli kwa kuwa sikuwa nimepokea barua yoyote na ilizua taharuki kwamba Kanisa letu limefungiwa.”
Soma Pia: Serikali yalifutia usajili Kanisa la Askofu Gwajima kwa kuingilia masuala ya siasa kwa nia ya kuichonganisha Serikali na Wananchi
Awali, barua hiyo ambayo hakuna Mamlaka iliyojitokeza kuizungumzia ilieleza Kanisa hilo limefungiwa kwa maelezo ya kutoa mahubiri yenye mwelekeo wa Kisiasa na nia ya kuichonganisha Serikali na Wananchi