Askofu Gwajima aidanganya mahakama

10000

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2013
Posts
839
Reaction score
785
Katika uchambuzi wa mageziti asubui ya leo nimesikia gazeti moja likiandika kwamba;

Askofu wa kanisa la ufufuo na uzima Gwajima amekanusha mashtaka aliyoshtakiwa kwayo na JMT kufuatia kumtukana Askofu mkuu wa jimbo kuu katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo.

Uongo aliousema askofu Gwajima ni kukataa mbele ya hakimu kwamba hakumuita askofu Pengo mtoto, mpuuzi. Maneno ambayo yanaweza kusababisha uvunjifu wa amani.

Kukataa kwake kusema ukweli inadhihirishia umma wa Tanzania kwamba Askofu Gwajima ni mtu muongo.

CHANZO:
MWANANCHI

 
huenda tafsiri ya neno mtoto na mpuuzi inamaanisha kitu kingine kwa gwajima na sio hakimu anavyofikiria, atakapoulizwa maana tutamsikia akitoa ufafanuz
 
10000

mkuu tulia usikurupuke kiasi hicho sheria ni noma unaweza ukasema kaidanganya mahakama lakin ktk utetezi wake akawa na point za kutosha na kuwabwaga mbaya
 
Last edited by a moderator:
Hakuna kesi hapo ni uhuni tu nna upotevu wa pesa za umma kuiendesha kesi za kipuuzi na kipumbavu. Kesi ziko nyingi serikali inakomalia kesi zisizo na tija,, ilikua presha ya pinda kwa kutukanwa mfipa mwezake sasa amekatwa awe mpole.

Gwajima atashinda hiyo kesi.
 
10000

hivi kuna watu bado wamfuata gwajima...jamani wandugu fungukeni ata macho bac...ni nyakati za mwisho...
 
Last edited by a moderator:
10000

Tena uongo wa mtu ambaye waumini wake wanaamini maneno yake halafu leo anakanusha huo ni uhuni ambao ni mbaya sana hakuna tofauti na ibilisi mwenyewe. Tena katika clip anasikika akisema Askofu Mkuu Pengo ni sawa na mtoto anayevaa pampas. Inashangaza leo anakana hayo, kama kiongozi wa dini ilifaa sana awe mkweli kwani ingekuwa ni ushuhuda na mfano bora kwake nabkwa kanisa lake.
 
Last edited by a moderator:
Wewe nenda ukawe hakimu/jaji kama unadhani mahakama imedanganywa...
 
Kesi kazi hizi huwa zinajifia zenyewe kimya kimya
 
Ndiyo nimesikia leo kwamba neno "MTOTO" ni tusi linaloweza kupelekea uvunjifu wa amani. Na ni nani mlalamikaji katika hili shauri?
 
kesi ambayo mlalamikaji ni jamhuri mara nyingi jamhuri huwa anapigwa chini

Jamhuri bila shahidi anayethibitisha athari za neno mtoto kwake?

Hivi mtoto ni tusi?

Hapa naona hata shetani anasingiziwa! Shetani ni cha mtoto!
 
Pengo alishamsamehe Gwajima sasa kesi mlalamikaji ni nani?siasa za mpaka mahakamani
 

Awe mkweli mbele ya nani. Sheria haiendi hivyo, lazima ukatae ili kesi iendelee upate muda wa kujieleza/ utetezi. Ukisema ndio kesi inaisha unapangiwa siku ya hukumu.
 
Last edited by a moderator:
sasa mtu anayesema anafufua watu anaachaje kuwa muongo..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…