Askofu Fernandes: Tunasimama na Serikali, mkifanya vizuri tutawabariki, mkifanya vibaya tutawakemea

Askofu Fernandes: Tunasimama na Serikali, mkifanya vizuri tutawabariki, mkifanya vibaya tutawakemea

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Mwenyekiti wa Umoja wa Maaskofu wa Makanisa ya Kipentekoste (CPCT), Askofu Dr. Vernon Fernandes, akiwa Madhabahuni mbele ya Makamu wa Rais, Emmanuel Nchimbi, amesema mara kadhaa kuwa Kanisa la Kipentekoste limekuwa likitengwa na Serikali. Hata wakialikwa kwenye vikao vingi, bado hawapewi nafasi ya kuzungumza.

"Wengine wanaitwa, sisi wanatuita njoo, lakini hatupewi nafasi. Hata hivyo, awamu hii mmetuheshimu sana, mmejenga uhusiano nasi. Sisi tunasema tunasimama na Serikali: wakati mnafanya vizuri tutawabariki, na wakati mnafanya vibaya tutawakemea."

Dr. Vernon Fernandes amesema hayo Februari 6, 2026, wakati wa hafla ya Usimikaji na Uzinduzi wa Uongozi wa Awamu ya Tano wa The Council of Pentecostal Churches of Tanzania (CPCT), iliyofanyika Ukumbi wa Agape Life Church, Mbezi Jogoo, jijini Dar es Salaam.

Soma:
 
Wanaiba kura
Wanauwa ndugu zetu
Wanasema tusimame nao
mahaini hawa
 
Rushwa waliyopewa na Rais ya milioni 100 na kiwanja cha hekari 12 Dodoma.
 
Na miaka ya nyuma walisema upinzani ndio wataleta vurugu kwenye nchi endapo watatawala. Sasa kinyume chake wao ndio wameiharibu nchi.
Dar hakuna maji muda Sasa yanapuyanga tu Dodoma
Utasikia muheshimiwa waziri wa maji kenge hawa
 
Mwenyekiti wa Umoja wa Maaskofu wa Makanisa ya Kipentekoste (CPCT), Askofu Dr. Vernon Fernandes, akiwa Madhabahuni mbele ya Makamu wa Rais, Emmanuel Nchimbi, amesema mara kadhaa kuwa Kanisa la Kipentekoste limekuwa likitengwa na Serikali. Hata wakialikwa kwenye vikao vingi, bado hawapewi nafasi ya kuzungumza.

"Wengine wanaitwa, sisi wanatuita njoo, lakini hatupewi nafasi. Hata hivyo, awamu hii mmetuheshimu sana, mmejenga uhusiano nasi. Sisi tunasema tunasimama na Serikali: wakati mnafanya vizuri tutawabariki, na wakati mnafanya vibaya tutawakemea."

Dr. Vernon Fernandes amesema hayo Februari 6, 2026, wakati wa hafla ya Usimikaji na Uzinduzi wa Uongozi wa Awamu ya Tano wa The Council of Pentecostal Churches of Tanzania (CPCT), iliyofanyika Ukumbi wa Agape Life Church, Mbezi Jogoo, jijini Dar es Salaam.
Soma:
well done bishop Fernandes:KasugaYeah:
 
Back
Top Bottom