Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 2,786
- 7,567
Wakuu,
Askofu Bagonza Disemba 8 aliuliza, "Kuvaa kininja mahakamani na kuteka/kukamata bila sare; aseme IGP au Waziri? Askari wamfuate yupi? Nani awaamue?"
Aliuliza swali hilo, kukiwa na mfululizo wa matukio yanayotokea polisi wakiwa wanaendelea kukamata watu bila ya kufuata utaratibu baada ya Waziri Simbachawene kutoa maagizo ya taratibu kufuata pindi mtu anakuwa anakamatwa.
Majuzi kuna askari alisema kwenye mahojiano kwamba watuhumiwa ni wajanja, wakisikia wanaenda kukamatwa wanakimbia, kwahiyo nao inabidi wavae kiraia ili waende nao sambamba! Hili linatosha kuhalalisha taratibu kuvunjwa?
Tukirudi kwenye swali la msingi la Askofu Bagonza, nani anatakiwa kutoa maagizo hayo, kama hata baada ya Waziri Simbachawene kutoa maagizo, baado ukamataji ule ambao haufuati taratibu na sheria unaendelea?
Askofu Bagonza Disemba 8 aliuliza, "Kuvaa kininja mahakamani na kuteka/kukamata bila sare; aseme IGP au Waziri? Askari wamfuate yupi? Nani awaamue?"
Aliuliza swali hilo, kukiwa na mfululizo wa matukio yanayotokea polisi wakiwa wanaendelea kukamata watu bila ya kufuata utaratibu baada ya Waziri Simbachawene kutoa maagizo ya taratibu kufuata pindi mtu anakuwa anakamatwa.
Majuzi kuna askari alisema kwenye mahojiano kwamba watuhumiwa ni wajanja, wakisikia wanaenda kukamatwa wanakimbia, kwahiyo nao inabidi wavae kiraia ili waende nao sambamba! Hili linatosha kuhalalisha taratibu kuvunjwa?
Tukirudi kwenye swali la msingi la Askofu Bagonza, nani anatakiwa kutoa maagizo hayo, kama hata baada ya Waziri Simbachawene kutoa maagizo, baado ukamataji ule ambao haufuati taratibu na sheria unaendelea?