Bwana Yesu asifiwe!
Ndugu wakristo; nawasalimu katika jina la Bwana Wetu, Yesu Kristo
Kama mnavyofahamu, Kanisa lina jambo zito mikononi kwa sasa. Viongozi wetu wamekutana ili kumuomba Mungu ashushe baraka zake zaidi katika Kanisa letu la Kiinjili La Kilutheri Tanzania.
Wamekutana kutekeleza majukumu yao ya kikanisa lakini pia kutekeleza takwa la kikatiba (Katiba ya KKKT – toleo la mwaka 2011) ambalo linahitaji kuwepo kwa mkutano mkuu.
Viongozi wetu pamoja na kupokea ripoti mbalimbali za kanisa, watamchagua kiongozi mkuu wa kanisa tarehe 23/08/2019. Kazi ya kumpata mkuu wa kanisa inahitaji maombi.
Tufunge tuombe Mungu ili kiongozi mkuu wa kanisa apatikane katika mazingira ya amani na utulivu. Kiongozi tupewe aliyeletwa na Mungu mwenyewe ili atuongoze katika haki, maadili ya kanisa na tupate matarajio mema ya kufika mbinguni na sio kwenda motoni. Tunafahamu, sala ndio nguzo kuu katika hili na wanadamu tunatimiza tu mambo ambayo tayari mungu amepanga yatokee.
Mimi na familia yangu tumeendelea kupiga magoti kumuomba sana mungu ili miaka minne ijayo tuendelee kuwa katika utulivu mkubwa wa kikanisa na waumini wote tupate huduma nzuri ya kiroho. Haya ya kibinadamu yatatimia endapo kanisa litakuwa na utulivu, maelewano na kutokuwa na migogoro baina yetu kama washarika wa KKKT.
Hekima, unyenyekevu, umakini, uadilifu na kuwa mtu wa maombi ni sehemu ya sifa ya kiongozi anayetakiwa katikati yetu hivi sasa.
Nimekaa na mkuu wa kanisa anayemaliza muda wake hivi sasa, ndugu yangu baba Askofu Dr. Fredrick Shoo (phd). Miaka minne aliyotuongoza tumejifunza mengi kwake. Tunamshukuru.
Kama alivyosema ndugu yangu Remmy Cameroon wa sauti ya wasio na sauti endapo kutakuwa na mabadiliko, yeye atabaki kuwa Askofu na kijiti hicho atampa askofu mwingine aendelee kuanzia pale alipoishia.
Remmy alisisitiza tarehe 20/08/2019 katika ujumbe wake kwa kanisa kuwa _katiba ya KKKT inaweka bayana kuwa mkuu wa Kkkt ataongoza kwa miaka minne na kama atataka kuchaguliwa tena kwa muhula wa pili atawania nafasi hiyo na kama kuna askofu mwingine atapendekezwa kuwania kiti hicho anaruhusiwa. Iwapo wajumbe hawatamchagua tena Askofu Shoo kwa muhula wa pili halitokuwa tukio geni katika kanisa letu.”
Mambo makubwa ambayo ningependa kuyasema kwa sasa ni kuwa, wanaojitokeza kama mbadala wa shoo basi angalau wawe na vigezo ambavyo mungu ameviweka katika kanisa ili vijidhihirishe machoni pa watu.
Nafahamu, Baba Askofu Dr. Benson bagonza amewahi kuniambia matamanio yake ya kuwa askofu mkuu wa KKKT. Sijui ni lini ila kama ni sasa, naomba mungu atuepushe asikae sasa kwa kuwa bado ana mgogoro mkubwa katika ngazi ya kifamilia.
Tunafundishwa katika kanisa, “ibada njema huanzia nyumbani”. Kitendo cha kumtelekeza mke wake wa pembeni anayeitwa Peace Sylivester ambaye amezaa naye kilimuwekea doa kwa kuwa migogoro ya ndoa kama kiongozi mkuu wa kanisa hataiweza.
Mwanamke huyu anahangaika na watoto, anapiga magoti kuomba misaada lakini baba wa watoto anakaa kivulini kanisani kuhubiri ‘waumini tuwe na mapenzi ya dhati katika familia zetu’. Kama yeye yamemshinda nyumbani, ataweza kuliongoza kanisa kwa miaka minne au nane?
Tunafunga siku ya leo na kesho wakristo ili tupate kiongozi muadilifu, mwenye hofu ya mungu, mwenye kuleta umoja katika kanisa, atakayetuongoza kutatua migogoro iliyopo ndani na nje ya kanisa ili kkkt nasi tujivunie kuliko kunyooshewa vidole kila siku katika jamii.
Hatupendi kanisa letu lisambaratike baada ya uchaguzi huu mkuu.
Wajumbe wa halmashauri kuu, wajumbe wa mkutano mkuu na baraza la maaskofu tujitafakari, tufanye maamuzi magumu yenye baraka kwa washarika wetu na dayosisi tunazoziongoza. Sisi washarika tunawaombea mtimize wajibu wenu katika kanisa.
Msema kweli mpenzi wa mungu.
Dr. Mwombeki, Kamugisha
Karagwe
Ndugu wakristo; nawasalimu katika jina la Bwana Wetu, Yesu Kristo
Kama mnavyofahamu, Kanisa lina jambo zito mikononi kwa sasa. Viongozi wetu wamekutana ili kumuomba Mungu ashushe baraka zake zaidi katika Kanisa letu la Kiinjili La Kilutheri Tanzania.
Wamekutana kutekeleza majukumu yao ya kikanisa lakini pia kutekeleza takwa la kikatiba (Katiba ya KKKT – toleo la mwaka 2011) ambalo linahitaji kuwepo kwa mkutano mkuu.
Viongozi wetu pamoja na kupokea ripoti mbalimbali za kanisa, watamchagua kiongozi mkuu wa kanisa tarehe 23/08/2019. Kazi ya kumpata mkuu wa kanisa inahitaji maombi.
Tufunge tuombe Mungu ili kiongozi mkuu wa kanisa apatikane katika mazingira ya amani na utulivu. Kiongozi tupewe aliyeletwa na Mungu mwenyewe ili atuongoze katika haki, maadili ya kanisa na tupate matarajio mema ya kufika mbinguni na sio kwenda motoni. Tunafahamu, sala ndio nguzo kuu katika hili na wanadamu tunatimiza tu mambo ambayo tayari mungu amepanga yatokee.
Mimi na familia yangu tumeendelea kupiga magoti kumuomba sana mungu ili miaka minne ijayo tuendelee kuwa katika utulivu mkubwa wa kikanisa na waumini wote tupate huduma nzuri ya kiroho. Haya ya kibinadamu yatatimia endapo kanisa litakuwa na utulivu, maelewano na kutokuwa na migogoro baina yetu kama washarika wa KKKT.
Hekima, unyenyekevu, umakini, uadilifu na kuwa mtu wa maombi ni sehemu ya sifa ya kiongozi anayetakiwa katikati yetu hivi sasa.
Nimekaa na mkuu wa kanisa anayemaliza muda wake hivi sasa, ndugu yangu baba Askofu Dr. Fredrick Shoo (phd). Miaka minne aliyotuongoza tumejifunza mengi kwake. Tunamshukuru.
Kama alivyosema ndugu yangu Remmy Cameroon wa sauti ya wasio na sauti endapo kutakuwa na mabadiliko, yeye atabaki kuwa Askofu na kijiti hicho atampa askofu mwingine aendelee kuanzia pale alipoishia.
Remmy alisisitiza tarehe 20/08/2019 katika ujumbe wake kwa kanisa kuwa _katiba ya KKKT inaweka bayana kuwa mkuu wa Kkkt ataongoza kwa miaka minne na kama atataka kuchaguliwa tena kwa muhula wa pili atawania nafasi hiyo na kama kuna askofu mwingine atapendekezwa kuwania kiti hicho anaruhusiwa. Iwapo wajumbe hawatamchagua tena Askofu Shoo kwa muhula wa pili halitokuwa tukio geni katika kanisa letu.”
Mambo makubwa ambayo ningependa kuyasema kwa sasa ni kuwa, wanaojitokeza kama mbadala wa shoo basi angalau wawe na vigezo ambavyo mungu ameviweka katika kanisa ili vijidhihirishe machoni pa watu.
Nafahamu, Baba Askofu Dr. Benson bagonza amewahi kuniambia matamanio yake ya kuwa askofu mkuu wa KKKT. Sijui ni lini ila kama ni sasa, naomba mungu atuepushe asikae sasa kwa kuwa bado ana mgogoro mkubwa katika ngazi ya kifamilia.
Tunafundishwa katika kanisa, “ibada njema huanzia nyumbani”. Kitendo cha kumtelekeza mke wake wa pembeni anayeitwa Peace Sylivester ambaye amezaa naye kilimuwekea doa kwa kuwa migogoro ya ndoa kama kiongozi mkuu wa kanisa hataiweza.
Mwanamke huyu anahangaika na watoto, anapiga magoti kuomba misaada lakini baba wa watoto anakaa kivulini kanisani kuhubiri ‘waumini tuwe na mapenzi ya dhati katika familia zetu’. Kama yeye yamemshinda nyumbani, ataweza kuliongoza kanisa kwa miaka minne au nane?
Tunafunga siku ya leo na kesho wakristo ili tupate kiongozi muadilifu, mwenye hofu ya mungu, mwenye kuleta umoja katika kanisa, atakayetuongoza kutatua migogoro iliyopo ndani na nje ya kanisa ili kkkt nasi tujivunie kuliko kunyooshewa vidole kila siku katika jamii.
Hatupendi kanisa letu lisambaratike baada ya uchaguzi huu mkuu.
Wajumbe wa halmashauri kuu, wajumbe wa mkutano mkuu na baraza la maaskofu tujitafakari, tufanye maamuzi magumu yenye baraka kwa washarika wetu na dayosisi tunazoziongoza. Sisi washarika tunawaombea mtimize wajibu wenu katika kanisa.
Msema kweli mpenzi wa mungu.
Dr. Mwombeki, Kamugisha
Karagwe