Kwani hata ana hizo akili za kufikiria hivyo chifu!! Unamwonea bure!Huyu bwana mwisho wa maisha yake utakuwa mbaya sana.
Ameliishwa maneno mengi sana ya kinafiki ,sina shaka kabla jogoo halijawika atakanusha maneno yake na utakua sio msimamo wa kanisa!
Kakelwa ndio kilugha gani na unamaanisha nini wewe Bashite?Sema Askofu kakelwa, sio Maas kofu wamekelwa.
Yeye anasubiria dhifa za kitaifa akapige mpunga kitenesi tinge kubwa kama limao.VIPI sheikh Mkuu Wa Dar vurugu za Mbweni Saranga hawajaziona?
Kuna jambo gani baya na kubwa kuliko yote zaidi ya kutoa roho za watu wasio na hatia Kisa tuu kutafuta ushindi tena wa Udiwani,je ukiwa wa Urais itakuwaje?Hilo ndilo aliloliona. Kuna mambo mangapi ya ovyo yaliyokuwa yakifanyika hapa nchini na asipaze sauti ya kukemea?
unauzungumziaje wa kenya!Mkuu sintoshangaa huyo askofu akikanusha hayo maneno yake kama ulivyotabiri. Kwa mazingira ya mtu kupigwa risasi na waliokupiga wasifahamike ni askofu gani hajipendi? Ila hata huyo askofu aseme asiseme uchaguzi ule uliopita wananchi wameudharau kwa jinsi ilivyotumika nguvu kubwa kupata matokea ya kuhalilisha kukubalika kwa ccm. Huu ni ukweli unaouma. Sisi tunaoweza siasa za wastani tulijua hili litatokea mara baada ya kuwapokea madiwani waliohamia ccm mbele ya hafla ya kijeshi. Ile ni ishara kuwa hata raia wasipochagua wanaccm basi jeshi litahakikisha ccm inatawala, ule ulikuwa ni ujembe ulio ubaoni kila mtu kuweza kuona.
yeye kaona hilo hayo mengine na wewe semaHilo ndilo aliloliona. Kuna mambo mangapi ya ovyo yaliyokuwa yakifanyika hapa nchini na asipaze sauti ya kukemea?
Dua la kuku halimpati mweweHuyu bwana mwisho wa maisha yake utakuwa mbaya sana.
Mimi ni mkala, ninamaanisha amekerwa, ameudhiwa, umen-copy?Kakelwa ndio kilugha gani na unamaanisha nini wewe Bashite?
Huyo ni askofu au muangalizi tu wa huduma?MATOKEO ya uchaguzi wa udiwani katika kata 43 nchi nzima uliofanyika Jumapili yameleta taswira kwamba itafika wakati Watanzania wapige kura kwa kutamka mgombea wanayemtaka badala ya kupiga kura kwa kutumia karatasi vituoni.
Kauli hii imetolewa leo na Askofu William Mwamalanga wa Kanisa la Pentekoste nchini (PEC), akitathmini matokeo ya uchaguzi huo pamoja na matukio yaliyoandamana na upigaji kura.
Uchaguzi uligubikwa na matukio ya vurugu na ukamataji wa mawakala na viongozi wa vyama vya upinzani kwa visingizio vya kuhusika na vurugu. Hakuna hata kiongozi mmoja wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) aliyekamatwa.
Askofu Mwamalanga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Maadili, Amani na Haki za Binadamu kwa Jamii ya Viongozi wa Dini, amesema ripoti zinazotoka kwa watu katika maeneo mengi ambako uchaguzi ulifanyika, zinaonesha kulikuwa na mpango mahsusi wa kuvuruga uchaguzi kwa manufaa ya CCM.
“Ukisikiliza yanayosemwa na watu waliokuwa maeneo ya uchaguzi utajenga hisia kuwa palikuwa na kila dalili watawala walitaka kulazimisha matokeo wayatakayo wao na sio kulingana na matakwa ya wananchi ambao ndio hutoa ridhaa kwa viongozi wawatakao. Sasa tunapata malalamiko ya wananchi kwamba wanataka wasikilizwe na vyombo vya kisheria kuhusu namna ya kupata haki yao ya kuchagua.
“Watu wanatulalamikia sisi viongozi wa dini kuwa hatushughuliki kukemea mtindo huu wa kuminya haki za raia wakati wa uchaguzi hivyo kuonesha kama tunaridhika na mtindo huu. Ni kadhia inayoonesha utawala bora umo kwenye mtihani katika nchi yetu.
“Lakini kwa hakika tunasema mambo haya kila wakati kwamba si mazuri; lazima raia walindwe ikiwemo kuthaminiwa kwa kura zao wakati wa uchaguzi maana hii ni haki yao ya msingi ya kuchagua viongozi wanaowataka.
“Si vizuri watu kulalamika kuwa wamemchagua mgombea fulani awe kiongozi wao lakini mwishoni mwa uchaguzi, anatangazwa mtu mwingine ambae wananchi wana uhakika amepata kura ndogo sana,” alisema katika mahojiano yake maalum na MwanaHALISI Online, yaliyofanyika leo kwa njia ya simu.
Amesema misingi ya demokrasia inapaswa kuenziwa kwani ina maana yake kubwa ikiwamo kuondoa taratibu za kupata viongozi kwa njia za asili kama wananchi kusimama nyuma ya mgombea ambaye mtu anamtaka au kutamka jina la mgombea anayemtaka.
Ameongeza kuwa inashangaza kuitarajia haki kwa mfano katika mazingira ambayo Jeshi la Polisi limekamata mawakala wote wa vyama vya upinzani kwenye kituo cha uchaguzi. “Ni nani atakayesimamia haki ya wagombea ambao mawakala wao wamekamatwa na kupelekwa vituoni,” alihoji.
Jeshi la Polisi kupitia makamanda wa mikoa mbalimbali walikaririwa wakisema kwamba walilazimika kukamata watu walioripotiwa kuwa wameshiriki vitendo vya fujo wakati wa uchaguzi. Hata hivyo, hakuna maelezo ya kuridhisha kuhusu wale waliokamatwa siku moja kabla ya Jumapili, siku ya uchaguzi.
Viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wa maeneo mbalimbali walikamatwa siku ya kabla ya uchaguzi na kuwekwa vituoni mwa polisi.
Katika uchaguzi huo, CCM imetangazwa kushinda Kata 42, zikiwemo kata tano za Arumeru mkoani Arusha ambako madiwani wake walijiuzulu kwa mkupuo katika kile kilichosadikika kuwa ni njama za CCM kuhodhi siasa za maeneo hayo na hivyo kutawala kimaamuzi kwenye halmashauri. Madiwani waliojiuzulu ni wale waliochaguliwa na wananchi katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 2015.
Chadema ilifanikiwa kukamata vielelezo vya kuonesha kuwa hatua hiyo ilikuwa ni mkakati wa CCM kwa kutumia viongozi wa kiserikali ambao waliwashawishi madiwani kwa ahadi ya fedha na vyeo.
Chanzo: Mwanahalisi Online
Political vicious circle at it again!!!! Had the opposition swooped all 42 wards, would there have been the same arugument??????????? Man of the clothe!!!!!!!!!!!MATOKEO ya uchaguzi wa udiwani katika kata 43 nchi nzima uliofanyika Jumapili yameleta taswira kwamba itafika wakati Watanzania wapige kura kwa kutamka mgombea wanayemtaka badala ya kupiga kura kwa kutumia karatasi vituoni.
Kauli hii imetolewa leo na Askofu William Mwamalanga wa Kanisa la Pentekoste nchini (PEC), akitathmini matokeo ya uchaguzi huo pamoja na matukio yaliyoandamana na upigaji kura.
Uchaguzi uligubikwa na matukio ya vurugu na ukamataji wa mawakala na viongozi wa vyama vya upinzani kwa visingizio vya kuhusika na vurugu. Hakuna hata kiongozi mmoja wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) aliyekamatwa.
Askofu Mwamalanga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Maadili, Amani na Haki za Binadamu kwa Jamii ya Viongozi wa Dini, amesema ripoti zinazotoka kwa watu katika maeneo mengi ambako uchaguzi ulifanyika, zinaonesha kulikuwa na mpango mahsusi wa kuvuruga uchaguzi kwa manufaa ya CCM.
“Ukisikiliza yanayosemwa na watu waliokuwa maeneo ya uchaguzi utajenga hisia kuwa palikuwa na kila dalili watawala walitaka kulazimisha matokeo wayatakayo wao na sio kulingana na matakwa ya wananchi ambao ndio hutoa ridhaa kwa viongozi wawatakao. Sasa tunapata malalamiko ya wananchi kwamba wanataka wasikilizwe na vyombo vya kisheria kuhusu namna ya kupata haki yao ya kuchagua.
“Watu wanatulalamikia sisi viongozi wa dini kuwa hatushughuliki kukemea mtindo huu wa kuminya haki za raia wakati wa uchaguzi hivyo kuonesha kama tunaridhika na mtindo huu. Ni kadhia inayoonesha utawala bora umo kwenye mtihani katika nchi yetu.
“Lakini kwa hakika tunasema mambo haya kila wakati kwamba si mazuri; lazima raia walindwe ikiwemo kuthaminiwa kwa kura zao wakati wa uchaguzi maana hii ni haki yao ya msingi ya kuchagua viongozi wanaowataka.
“Si vizuri watu kulalamika kuwa wamemchagua mgombea fulani awe kiongozi wao lakini mwishoni mwa uchaguzi, anatangazwa mtu mwingine ambae wananchi wana uhakika amepata kura ndogo sana,” alisema katika mahojiano yake maalum na MwanaHALISI Online, yaliyofanyika leo kwa njia ya simu.
Amesema misingi ya demokrasia inapaswa kuenziwa kwani ina maana yake kubwa ikiwamo kuondoa taratibu za kupata viongozi kwa njia za asili kama wananchi kusimama nyuma ya mgombea ambaye mtu anamtaka au kutamka jina la mgombea anayemtaka.
Ameongeza kuwa inashangaza kuitarajia haki kwa mfano katika mazingira ambayo Jeshi la Polisi limekamata mawakala wote wa vyama vya upinzani kwenye kituo cha uchaguzi. “Ni nani atakayesimamia haki ya wagombea ambao mawakala wao wamekamatwa na kupelekwa vituoni,” alihoji.
Jeshi la Polisi kupitia makamanda wa mikoa mbalimbali walikaririwa wakisema kwamba walilazimika kukamata watu walioripotiwa kuwa wameshiriki vitendo vya fujo wakati wa uchaguzi. Hata hivyo, hakuna maelezo ya kuridhisha kuhusu wale waliokamatwa siku moja kabla ya Jumapili, siku ya uchaguzi.
Viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wa maeneo mbalimbali walikamatwa siku ya kabla ya uchaguzi na kuwekwa vituoni mwa polisi.
Katika uchaguzi huo, CCM imetangazwa kushinda Kata 42, zikiwemo kata tano za Arumeru mkoani Arusha ambako madiwani wake walijiuzulu kwa mkupuo katika kile kilichosadikika kuwa ni njama za CCM kuhodhi siasa za maeneo hayo na hivyo kutawala kimaamuzi kwenye halmashauri. Madiwani waliojiuzulu ni wale waliochaguliwa na wananchi katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 2015.
Chadema ilifanikiwa kukamata vielelezo vya kuonesha kuwa hatua hiyo ilikuwa ni mkakati wa CCM kwa kutumia viongozi wa kiserikali ambao waliwashawishi madiwani kwa ahadi ya fedha na vyeo.
Chanzo: Mwanahalisi Online
unauzungumziaje wa kenya!
HuoniAskofu nae ni binadamu, ana mapungufu yake, kwani hakuna mwanadamu mkamilifu, ana mapenzi yake, ana mahaba yake, anapendelea vitu flaniflani. Hakuna jipya kwenye matamshi yake.
Si Kila Askofu asemalo linatoka Moyoni.
We unaona?Huoni
SIO KWELI UZUSHIMATOKEO ya uchaguzi wa udiwani katika kata 43 nchi nzima uliofanyika Jumapili yameleta taswira kwamba itafika wakati Watanzania wapige kura kwa kutamka mgombea wanayemtaka badala ya kupiga kura kwa kutumia karatasi vituoni.
Kauli hii imetolewa leo na Askofu William Mwamalanga wa Kanisa la Pentekoste nchini (PEC), akitathmini matokeo ya uchaguzi huo pamoja na matukio yaliyoandamana na upigaji kura.
Uchaguzi uligubikwa na matukio ya vurugu na ukamataji wa mawakala na viongozi wa vyama vya upinzani kwa visingizio vya kuhusika na vurugu. Hakuna hata kiongozi mmoja wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) aliyekamatwa.
Askofu Mwamalanga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Maadili, Amani na Haki za Binadamu kwa Jamii ya Viongozi wa Dini, amesema ripoti zinazotoka kwa watu katika maeneo mengi ambako uchaguzi ulifanyika, zinaonesha kulikuwa na mpango mahsusi wa kuvuruga uchaguzi kwa manufaa ya CCM.
“Ukisikiliza yanayosemwa na watu waliokuwa maeneo ya uchaguzi utajenga hisia kuwa palikuwa na kila dalili watawala walitaka kulazimisha matokeo wayatakayo wao na sio kulingana na matakwa ya wananchi ambao ndio hutoa ridhaa kwa viongozi wawatakao. Sasa tunapata malalamiko ya wananchi kwamba wanataka wasikilizwe na vyombo vya kisheria kuhusu namna ya kupata haki yao ya kuchagua.
“Watu wanatulalamikia sisi viongozi wa dini kuwa hatushughuliki kukemea mtindo huu wa kuminya haki za raia wakati wa uchaguzi hivyo kuonesha kama tunaridhika na mtindo huu. Ni kadhia inayoonesha utawala bora umo kwenye mtihani katika nchi yetu.
“Lakini kwa hakika tunasema mambo haya kila wakati kwamba si mazuri; lazima raia walindwe ikiwemo kuthaminiwa kwa kura zao wakati wa uchaguzi maana hii ni haki yao ya msingi ya kuchagua viongozi wanaowataka.
“Si vizuri watu kulalamika kuwa wamemchagua mgombea fulani awe kiongozi wao lakini mwishoni mwa uchaguzi, anatangazwa mtu mwingine ambae wananchi wana uhakika amepata kura ndogo sana,” alisema katika mahojiano yake maalum na MwanaHALISI Online, yaliyofanyika leo kwa njia ya simu.
Amesema misingi ya demokrasia inapaswa kuenziwa kwani ina maana yake kubwa ikiwamo kuondoa taratibu za kupata viongozi kwa njia za asili kama wananchi kusimama nyuma ya mgombea ambaye mtu anamtaka au kutamka jina la mgombea anayemtaka.
Ameongeza kuwa inashangaza kuitarajia haki kwa mfano katika mazingira ambayo Jeshi la Polisi limekamata mawakala wote wa vyama vya upinzani kwenye kituo cha uchaguzi. “Ni nani atakayesimamia haki ya wagombea ambao mawakala wao wamekamatwa na kupelekwa vituoni,” alihoji.
Jeshi la Polisi kupitia makamanda wa mikoa mbalimbali walikaririwa wakisema kwamba walilazimika kukamata watu walioripotiwa kuwa wameshiriki vitendo vya fujo wakati wa uchaguzi. Hata hivyo, hakuna maelezo ya kuridhisha kuhusu wale waliokamatwa siku moja kabla ya Jumapili, siku ya uchaguzi.
Viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wa maeneo mbalimbali walikamatwa siku ya kabla ya uchaguzi na kuwekwa vituoni mwa polisi.
Katika uchaguzi huo, CCM imetangazwa kushinda Kata 42, zikiwemo kata tano za Arumeru mkoani Arusha ambako madiwani wake walijiuzulu kwa mkupuo katika kile kilichosadikika kuwa ni njama za CCM kuhodhi siasa za maeneo hayo na hivyo kutawala kimaamuzi kwenye halmashauri. Madiwani waliojiuzulu ni wale waliochaguliwa na wananchi katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 2015.
Chadema ilifanikiwa kukamata vielelezo vya kuonesha kuwa hatua hiyo ilikuwa ni mkakati wa CCM kwa kutumia viongozi wa kiserikali ambao waliwashawishi madiwani kwa ahadi ya fedha na vyeo.
Chanzo: Mwanahalisi Online
Wewe nyamaza kwa sababu hujui hata makanisa yanavyooperate. Pia hujui hata punje Biblia inamweleza askofu kuwa ni nani na anapatikanaje? Soma biblia na uje na neatral observation sio hii ya kuvutea na ukatolik au ukkkt. Askofu hapigiwi kura kama diwani, mbunge au rais kwani yeye sio mwanasiasa. Sikatai taratibu za wakatoliki, walutheri, waanglican na wengineo wa kumchagua askofu lakini biblia haijaeleza kuwa huo ndio exclusive methodology ya kumpata askofu. Pia hukutaja makanisa yenye kumpata askofu kwa mtindo huo unaothani wewe ni borq. Mfano TAGMaaskofu ambao siyo self declared ni RC, KKKT, Anglicana, Moravian. The rest ni akina Gwajima hawana impact kwenye siasa za dunia. Wana impact kisiasa tu za maeneo waliyopo.
Maaskofu ambao siyo self declared ni RC, KKKT, Anglicana, Moravian. The rest ni akina Gwajima hawana impact kwenye siasa za dunia. Wana impact kisiasa tu za maeneo waliyopo.