Katika hili sipendi kuwa ' Mnafiki ' kwa Kupepesa macho, Kutikisa masikio na Kuyamung'unya maneno kwa kusema kwamba Watumiaji wengi wa Magari wanapenda sana ' Kuwadharau ' Askari barabarani na kuna muda mwingine utakuta Mtu kabisa anatoka ' maskani ' anakuambieni kuwa leo naenda kuwazingua ' Matrafiki ' na akitiimiza hilo anarudi na kuanza kuwacheka na kuwadhihaki.
Najua kwamba wapo ' Matrafiki ' wanaozingua ila kwa jinsi hivi sasa wanavyosimamiwa vyema na Wakubwa wao na Jeshi lao na Sisi tunaopita na kukutana nao barabarani kila uchao huku tukishuhudia mengi ni dhahiri shahiri kwamba Wamiliki wengi wa Magari huwafanya vitendo vya makusudi dhidi yao na pia kumbukeni kuwa hata Wao pia ni Binadamu na wana mioyo vile vile. Tukijiheshimu na kufuata taratibu zote za matumizi ya Magari na Usalama wa Barabarani nina uhakika hizi adha / kero zitapungua kama siyo kuisha kabisa.
Kwa mfano unakuta Mtu kabisa anaona barabara imefungwa kwa muda tu ili kupisha Msafara wa Kiongozi wa Kitaifa kupita hapo halafu unaona Mtu kabisa kwa makusudi analichomeka Gari lake ' Kiubishi ' ili tu apite kwa nia ya kuiwahi huo Msafara halafu ile akitokeza tu barabarani hapo anakutaka na Pikipiki ya Polisi ya Msafara nayo ikiwa Kasi na pengine hata kuhatarisha Usalama wake na wa yule Kiongozi anayepitishwa. Hivi kwa ' scenario ' kama hii hao ' Matrafiki ' wakikupa mkong'oto wa haja utawalaumu?
Tuwe tunatafakari kabla ya kulaumu au kuwatupia Watu lawama.