Askari polisi kutoboa sikio hii imekaaje??

Askari polisi kutoboa sikio hii imekaaje??

adakiss23

JF-Expert Member
Joined
Jan 23, 2011
Posts
4,896
Reaction score
5,258
Juzi jioni nilikuwa sehemu flani kulikuwa kuna tukio linaendelea (la amani tu). Kwa kuwa kulikuwa na mkusanyiko wa watu na mali basi waandaaji walikuwa wameandaa askari polisi ili kuhakikisha hakuna lolote baya litajiri eneo hilo.

Nilishtuka sana kuona mmoja wa askari aliyekuwa pale (alisogea sehemu ambayo tuliyopo ktk kutuhakikia usalama) ametoboa sikio la kushoto. Si kutoboa kama baadhi ya mila za baadhi ya makabila. Utoboaji ule ni wa kihuni kabisa.

Nikawaonesha wenzangu tuliokuwa nao wajionee maajabu kila mmoja alipigwa na butwaa inakuwaje hali ile. Tulijaribu walau tupate picha lakini ilikuwa ngumu sana. Tukaacha kama ilivyo.

Ila bado nina maswali kadhaa wanaajiriwaje mtu wa namna hiyo?? Tena kwenye sehemu nyeti kama hiyo?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Si najua wanachunguzwaga hayo mambo na kuna mwaka wapo waliorudishwa toka CCP sababu ya tatoo na mambo kama hayo?
 
Yawezekana alikuwa mwanamke mwenye muonekano wa kiume, who knows.? Kama alikuwa mwanaume basi jua kuwa na SHOGA!
 
Jeshi la Saidi Mwema hilo; full intelligensia! Natamani Nyerere angefufuka leo ajionee "Vijana" wake walivyokichakachua chama alichokijenga na kuchakachuaa kila asasi katika serikali ya wahuni hawa (CCM). Sasa tunao mapolisi full mlegezo (Na bila shaka wapo mashoga), wanaotembea wakitimuaa moshi wa sigara utadhani lilipita treni, wanaotoboa masikio, wanawake wanaoweka kofia zao juu ya mawigi na kila takataka!
Hakika tumekwisha. Mungu ibariki Tanzania.
 
Labda ni wale askarikanzu wanajichanganya waonekane bongo fleva...wanavaa jinsi milegezo,vipuri na wengine wanaendesha boda boda ila ni askari kanzu!wako wengi sana wengine shoe shinners vituo vya dala dala....
 
Hakuna polisi wa ukweli sasa ivi idadi kubwa ni wavuta bangi wavaa vinguo vya ajabu ni watekaji wakijua una kitu ni watu wa kuwakwepa sana zama hizi
 
will mutunga jaji mkuu wa kenya mwenye heren sikioni je?
 
kutoboa sikio kihuni haikubaliki, ila upatikanaji wa ajira za polisi ni kwa kufahamiana, na kwa rushwa na kufanya uchekechaji kwa waajiriwa kuwa bora liende.
 
Excuse me!! kwani askari hawaruhusiwi kutoboa sikio?
Ni askari wa kiume tuu ndio hawaruhusiwi lakini kama ni askari mwanamke then haina tatizo.
Unless mtoas mada kama ange'specify ni wa jinsi gani?
 
Excuse me!! kwani askari hawaruhusiwi kutoboa sikio?
Ni askari wa kiume tuu ndio hawaruhusiwi lakini kama ni askari mwanamke then haina tatizo.
Unless mtoas mada kama ange'specify ni wa jinsi gani?

Inaonyesha itakuwa wa kiume, ikiwa wakike anashangaa itakuwa hatari kubwa... lakini hawa safari kwa Sasa Hawan a adabu wengi wanavaa chini ya makalio...
 
Juzi jioni nilikuwa sehemu flani kulikuwa kuna tukio linaendelea (la amani tu). Kwa kuwa kulikuwa na mkusanyiko wa watu na mali basi waandaaji walikuwa wameandaa askari polisi ili kuhakikisha hakuna lolote baya litajiri eneo hilo.

Nilishtuka sana kuona mmoja wa askari aliyekuwa pale (alisogea sehemu ambayo tuliyopo ktk kutuhakikia usalama) ametoboa sikio la kushoto. Si kutoboa kama baadhi ya mila za baadhi ya makabila. Utoboaji ule ni wa kihuni kabisa.

Nikawaonesha wenzangu tuliokuwa nao wajionee maajabu kila mmoja alipigwa na butwaa inakuwaje hali ile. Tulijaribu walau tupate picha lakini ilikuwa ngumu sana. Tukaacha kama ilivyo.

Ila bado nina maswali kadhaa wanaajiriwaje mtu wa namna hiyo?? Tena kwenye sehemu nyeti kama hiyo?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
hiyo yasikitisha,haiko poa
 
sasa unaona kipi cha ajabu kuna wafanyakazi wangapi hawana maadili ukimuona askari mmoja ndio useme hana maadili ndio useme wote hawana harafu hata picha hujaweka tutaamini vipi au ndio majungu tu ya kuharibu sifa ya mtu kasome sheria ya utumishi wa umma inayosimamia mavazi na muonekano mzima wa watumishi wa umma ya mwaka 2007 ibara ya 3 na siyo kuhukumu mtu kwani wewe kama mfanyakazi unavaa na kuonekana mbele ya jamii kama sharia inavyoeleza hapo juu au ndio kuongea tu
 
....Mkuu, Ulitofautishaje Utoboaji Masikio wa Kimila na Ule wa Kihuni?? :A S 39:
 
kaka huyo pimbi yupo ki2o fulani mkoa wa temeke na anakaa kotazi za kilwa road dogo anajivunia baba yake ni kiongozi wa juu wa jeshi hilo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom