Raia mtiifu
Member
- Apr 26, 2019
- 17
- 53
Kuna baadhi ya mambo yanafanyika mpaka inafikia hatua ya kuanza kujiuliza huyu mtu alikuwa na maana ipi.
Leo nikiwa safarini natokea Arusha na basi ya kampuni ya Harambee,baada ya kupita Korogwe mjini kilometa chache mbele kuna kona ambapo majira ya jioni/usiku panakuwa na askari ambao hutimiza majukumu yao ya kila siku.
Kilichonifanya niandike andiko hili ni kitendo cha askari mmojawapo kati ya waliokuwa pale barabarani kusimama katikati ya barabara akiwa na tochi yenye mwanga mkali na kuelekezea kwenye kioo cha mbele cha dereva(tena akimlenga yeye).
Nilikuwa nimekaa mbele na kushuhudia dereva wa basi lile akihangaika kutafuta nini cha kufanya huku akiyumba na hatimae kufanikiwa kusimama pembeni.Kiukweli abiria tulioshuhudia tukio lile tulipatwa na butwaa huku hasira zikitawala na kuanza kumfokea yule askari na kwa aibu alijiondokea na kukaa pembeni na tochi yake.Hatukuweza kutambua sura yake wala namba yake kwa kuwa hatukushuka kwenye gari na ilikuwa giza limeshaingia.
Tunaomba vyombo vinavyohusika kuchunguza askari hawa hasa wanaosimama barabarani usiku maana inawezekana hawana utaalamu wa kazi hiyo.
Nawasilisha!
Leo nikiwa safarini natokea Arusha na basi ya kampuni ya Harambee,baada ya kupita Korogwe mjini kilometa chache mbele kuna kona ambapo majira ya jioni/usiku panakuwa na askari ambao hutimiza majukumu yao ya kila siku.
Kilichonifanya niandike andiko hili ni kitendo cha askari mmojawapo kati ya waliokuwa pale barabarani kusimama katikati ya barabara akiwa na tochi yenye mwanga mkali na kuelekezea kwenye kioo cha mbele cha dereva(tena akimlenga yeye).
Nilikuwa nimekaa mbele na kushuhudia dereva wa basi lile akihangaika kutafuta nini cha kufanya huku akiyumba na hatimae kufanikiwa kusimama pembeni.Kiukweli abiria tulioshuhudia tukio lile tulipatwa na butwaa huku hasira zikitawala na kuanza kumfokea yule askari na kwa aibu alijiondokea na kukaa pembeni na tochi yake.Hatukuweza kutambua sura yake wala namba yake kwa kuwa hatukushuka kwenye gari na ilikuwa giza limeshaingia.
Tunaomba vyombo vinavyohusika kuchunguza askari hawa hasa wanaosimama barabarani usiku maana inawezekana hawana utaalamu wa kazi hiyo.
Nawasilisha!