Asili ya jina Kilimanjaro

Asili ya jina Kilimanjaro

Omari Makoo

Member
Joined
Sep 6, 2016
Posts
78
Reaction score
39
Inasemekana kwamba Asili ya jina Kilimanjaro ni kwamba
mzungu alikwenda marangu na
akakutana na mzee wa kichaga miaka
hiyo ya nyuma na akauliza huu mlima
unaitwa nini? mzee wa kichaga akajibu
"Kilema Kyaro" akiwa anamaana ni
mlima wa ajabu kwa jinsi ulivyokuwa
ukichemka volcano. Basi mzungu
akapotosha jina na kuuita kilima-njaro!
lakini asili yake ni "KILEMA KYARO"
Hebu na wewe tupe asili ya majina ya mikoa ,wilaya ,vijiji,kata na mitaa unayoifahamu
 
Inasemekana kwamba katika jiji la Dar kilikuwa na mtu aliyeitwa MUSA HASSAN..huyu jamaa alikuwa mbabe sana anaogopwa balaa!..kama unavyojua jiji la dar asili yake ni kabila la wazaramo...basi yule MUSA HASSAN alikuwa anaenda mitaa flani hivi kutisha watu, wale wenyeji wa pale wakawa wanajifungia ndani huku wakiwaambia watoto wao "MWANA NYAMALA, MSASANI KOKWIZA" yaani (Mwanangu nyamaza Musa Hassan anakuja).... basi hayo maeneo yakaitwa MWANANYAMALA na kule alipokuwa akiishi MUSA HASSAN pakaitwa MSASANI.
 
Wilaya ya babati historia yake iko hivi, kulikuwa na mjerumani mmoja alitokea Arusha kuelekea mbulu, kufika maeneo ya ilipo babati akaona ziwa ila hakujua hapo ni sehemu gani, kuangalia mbele kidogo akaona moshi ikabidi aufuate ndipo akakuta nyumba ya nyasi nje kuna watoto wanacheza, mjerumani akawauliza watoto, ''Hapa ni wapi?'' Watoto kwa kutokuelewa wakajibu ''Baba Ti'' wakimaanisha baba yuko ndani, mjerumani akajua panaitwa Babati akaandika kwenye diary yake nakuendelea na safari yake,
 
Inasemekana kwamba Asili ya jina Kilimanjaro ni kwamba
mzungu alikwenda marangu na
akakutana na mzee wa kichaga miaka
hiyo ya nyuma na akauliza huu mlima
unaitwa nini? mzee wa kichaga akajibu
"Kilema Kyaro" akiwa anamaana ni
mlima wa ajabu kwa jinsi ulivyokuwa
ukichemka volcano. Basi mzungu
akapotosha jina na kuuita kilima-njaro!
lakini asili yake ni "KILEMA KYARO"
Hebu na wewe tupe asili ya majina ya mikoa ,wilaya ,vijiji,kata na mitaa unayoifahamu
volcano ya kilimanjaro imesinzia miaka mingi sana iloyo pita.. hata kabla wazungu hawajaja afrika.
 
Asili ya Chekereni. Mzungu alimwambia mchaga aangalie kama treni inakuja " Check Train" lakini kwa kuwa mchaga hakuelewa akamwambia mwenzake "anasema Chekereni" na ikawa hivo mpaka leo ndo mana Chekereni unaona kuna reli ipo pale ndio asili ya jina hilo
 
Kiboriloni Moshi. Hili jina limetokana na neno "Kibo Only" mzungu alifika maeneo hayo akiwa na lengo la kuona vizuri vilele vya mlima Kilimanjaro, cha ajabu aliishia kuona kilele kimoja cha Kibo pekee. Ndipo alipojikuta akiropoka Kibo only, wachaga wakajua amesema kiboroloni. Ikawa ndio jina
 
Zanzibar kuna sehemu kunaitwa Bububu, asili yake kuna bubu alikuwa anaogelea mtoni wakati anaogelea akawa anazama, hivyo ikabidi aombe msaada, ndio ile kuita bu bu bu, pakaitwa ivyo
Uongo. Kaulize tena inatokana na kiberenge!! Sitaki kukulisha kaulize
 
Inasemekana kwamba Asili ya jina Kilimanjaro ni kwamba
mzungu alikwenda marangu na
akakutana na mzee wa kichaga miaka
hiyo ya nyuma na akauliza huu mlima
unaitwa nini? mzee wa kichaga akajibu
"Kilema Kyaro" akiwa anamaana ni
mlima wa ajabu kwa jinsi ulivyokuwa
ukichemka volcano. Basi mzungu
akapotosha jina na kuuita kilima-njaro!
lakini asili yake ni "KILEMA KYARO"
Hebu na wewe tupe asili ya majina ya mikoa ,wilaya ,vijiji,kata na mitaa unayoifahamu
Usidanganye kyaro maana yake mbali
 
Asili ya Chekereni. Mzungu alimwambia mchaga aangalie kama treni inakuja " Check Train" lakini kwa kuwa mchaga hakuelewa akamwambia mwenzake "anasema Chekereni" na ikawa hivo mpaka leo ndo mana Chekereni unaona kuna reli ipo pale ndio asili ya jina hilo
Chekereni ipo Kenya Tanga Arusha. Sasa kote huko walikuwa wachagga? Fikiri zaidi
 
Kila kitu ni mzungu? U F. A. L. A. 100%
Kiboriloni Moshi. Hili jina limetokana na neno "Kibo Only" mzungu alifika maeneo hayo akiwa na lengo la kuona vizuri vilele vya mlima Kilimanjaro, cha ajabu aliishia kuona kilele kimoja cha Kibo pekee. Ndipo alipojikuta akiropoka Kibo only, wachaga wakajua amesema kiboroloni. Ikawa ndio jina
 
Singida ni neno la kibarbeig au mang'ati ISINGIDA maana yake pundamilia.Inasemekana ziwa singida kulikuako pundamilia wengi sana.Hivyo hao mang'ati walipofika wakawakuta wakinywa maji.Mzugu akashindwa kuita hao punda isingida na kuita singida mpaka leo.
 
Inasemekana kwamba katika jiji la Dar kilikuwa na mtu aliyeitwa MUSA HASSAN..huyu jamaa alikuwa mbabe sana anaogopwa balaa!..kama unavyojua jiji la dar asili yake ni kabila la wazaramo...basi yule MUSA HASSAN alikuwa anaenda mitaa flani hivi kutisha watu, wale wenyeji wa pale wakawa wanajifungia ndani huku wakiwaambia watoto wao "MWANA NYAMALA, MSASANI KOKWIZA" yaani (Mwanangu nyamaza Musa Hassan anakuja).... basi hayo maeneo yakaitwa MWANANYAMALA na kule alipokuwa akiishi MUSA HASSAN pakaitwa MSASANI.
Eeeh,, kweli ni huyu huyu MUSA HASSAN MGOSI ndo mwenye mtaa huo!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom