Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,444
- 7,792
Michezo ya kombe la shirikisho inaendelea na sasa ni klabu ya soka ya African Lyon dhidi ya Simba SC kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.
======
00' Muamuzi anapiga filimbi kuashiria mwanzo wa mchezo
09' Ibrahim Hajibu anaweka kamba ya kwanza kwa Simba, African Lyon 0-1 Simba
17' Bwalya anajaribu shuti kali kuelekea lango la African Lyon lakini linaishia kwa walinzi
18' Medie Kagere anajaribu na kipa wa African Lyon anafanya kazi ya ziada kuupangua
20' Chikwende anawekwa chini na mlinzi wa African Lyon, Simba inapata Penalt
22' Medie Kagere anakosa mkwaju wa penalt kwa kupiga nje
29' Mwashiuya anajaribu shuti kubwa nje ya 18 katika harakati za kusawazisha lakini mpira unapaa juu ya goli
39' Dilunga anamlamba chenga golikipa wa African Lyon lakini kasi ya mpira inamzidi na kupiga nje ya lango
43' Ibrahim Ajib Migomba anaweka goli lake la pili baada ya kupiga shuti kwenye mpira unaoambaa kutokana na mlinda mlango kuokoa shuti la Bwalya, African Lyon 0-2 Simba
45+2' Mwamuzi anapuliza filimbi kuashiria mapumziko, Ibrahim Ajib anakuwa shujaa wa kipindi cha kwanza kwa kuipa Simba goli mbili za kuongoza
UMILIKI WA MPIRA, AFRICAN LYON 37% - SIMBA 63%
45' Mpira unarejea kutoka mapumziko
47' Mwashiuya anapiga kona pacha kuelekea lango la Simba lakini zote zinakuwa hazina manufaa
62' Chikwende anaweka goli maridadi kwa upande wa Simba baada ya kupokea pasi maridadi kutoka kwa Miraji Athumani
65' Simba wanacheza mpira wa gonga lakini juhudi zao zinaishia kwa Gadiel Michael kuwa 'Offside'. African Lyon 0-3 Simba SC
68' Rehani Kibingu anajaribu kuitafutia African Lyon lakini shuti lake linaishia nyavu za pembeni
70' Saidi Khamis anaingia kuchua nafasi ya Rally Bwalya kwa upande wa Simba
71' Saidi Kipanga anatumia vizuri makosa ya mabeki wa Simba kuupoka mpira lakini shuti lake linapaa Juuu
75' Emmanuel Daudi analamba kadi ya njano kwa kumvuta ili kumpunguza kasi mchezaji wa Simba
81' John Bocco anachukua nafasi ya Meddie Kagere
87' Mwalami Abdalla anamdondosha Chikwende nje kidogo ya 18, anapewa kadi ya njano
FT' African Lyon inakubali kichapo na kuondoshwa kombe la shirikisho. Sasa Simba kukutana na Kagera Sugar hatua ya 16 bora. African Lyon 0-3 Simba.
======
00' Muamuzi anapiga filimbi kuashiria mwanzo wa mchezo
09' Ibrahim Hajibu anaweka kamba ya kwanza kwa Simba, African Lyon 0-1 Simba
17' Bwalya anajaribu shuti kali kuelekea lango la African Lyon lakini linaishia kwa walinzi
18' Medie Kagere anajaribu na kipa wa African Lyon anafanya kazi ya ziada kuupangua
20' Chikwende anawekwa chini na mlinzi wa African Lyon, Simba inapata Penalt
22' Medie Kagere anakosa mkwaju wa penalt kwa kupiga nje
29' Mwashiuya anajaribu shuti kubwa nje ya 18 katika harakati za kusawazisha lakini mpira unapaa juu ya goli
39' Dilunga anamlamba chenga golikipa wa African Lyon lakini kasi ya mpira inamzidi na kupiga nje ya lango
43' Ibrahim Ajib Migomba anaweka goli lake la pili baada ya kupiga shuti kwenye mpira unaoambaa kutokana na mlinda mlango kuokoa shuti la Bwalya, African Lyon 0-2 Simba
45+2' Mwamuzi anapuliza filimbi kuashiria mapumziko, Ibrahim Ajib anakuwa shujaa wa kipindi cha kwanza kwa kuipa Simba goli mbili za kuongoza
UMILIKI WA MPIRA, AFRICAN LYON 37% - SIMBA 63%
45' Mpira unarejea kutoka mapumziko
47' Mwashiuya anapiga kona pacha kuelekea lango la Simba lakini zote zinakuwa hazina manufaa
62' Chikwende anaweka goli maridadi kwa upande wa Simba baada ya kupokea pasi maridadi kutoka kwa Miraji Athumani
65' Simba wanacheza mpira wa gonga lakini juhudi zao zinaishia kwa Gadiel Michael kuwa 'Offside'. African Lyon 0-3 Simba SC
68' Rehani Kibingu anajaribu kuitafutia African Lyon lakini shuti lake linaishia nyavu za pembeni
70' Saidi Khamis anaingia kuchua nafasi ya Rally Bwalya kwa upande wa Simba
71' Saidi Kipanga anatumia vizuri makosa ya mabeki wa Simba kuupoka mpira lakini shuti lake linapaa Juuu
75' Emmanuel Daudi analamba kadi ya njano kwa kumvuta ili kumpunguza kasi mchezaji wa Simba
81' John Bocco anachukua nafasi ya Meddie Kagere
87' Mwalami Abdalla anamdondosha Chikwende nje kidogo ya 18, anapewa kadi ya njano
FT' African Lyon inakubali kichapo na kuondoshwa kombe la shirikisho. Sasa Simba kukutana na Kagera Sugar hatua ya 16 bora. African Lyon 0-3 Simba.