MAHANJU
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 5,255
- 8,027
Usiku wa jana kulikua na mahojiano katika kipindi cha Kuelekea 2015 startv, mahojiano yalikua kati ya Abubakari Asenga mjumbe wa mkutano mkuu Uvccm taifa na Angalieni mpendu upande wa Dar, Upande wa Mwanza alikuepo bibie Upendo Peneza, mjumbe wa mkutano mkuu Bawacha taifa na mtangazaji Dotto Bulendu.Kila moja aliulizwa kutoa maana halisi ya falsafa ya chama chake, Kila moja alijaribu kadri alivyoweza. Kati ya hawa wanasiasa chipukizi nani kaonesha umahiri wa hali ya juu? Nani ni hazina yetu ya taifa la kesho?