Mangisandy
JF-Expert Member
- Apr 23, 2012
- 2,652
- 2,272
Mheshimiwa Eduward Ngoyai Lowasa, nikiwa kijana wa Kitanzania, napenda kutambua Mchango wako mkubwa katika kuelekea mabadiliko Tanzania. Lengo lako na wengi tunaopenda mabadiliko ya kweli ilikua: IKULU.
Tulitaka ukasimamie mchakato wa mabadiliko kwa dhati, ukiwa kamanda namba moja. Kuonesha Imani yetu kwako tulikupa kura nyingi zaidi ya kura alizowahi kupata mgombea wa upinzani nchini Tanzania, na labda kuna kura zako nyingi zimepotea au kupotezwa!
Maamuzi uliyo fanya ni Yale ambayo Watanzania wengi wanaogopa kufanya, sababu kubwa ikiwa ile "fear of unknown" aliyo sema Sumaye. Kung'oka kwako CCM ni sauti ya kudumu ya kuhamasisha watu kukataa mfumo kandamizi, wenye dhuluma na msingi wake ukiwa maamuzi ya wachache.
Historia itakukumbuka kwa Ujasiri wa kukataa dhuluma na kuwa tayari kudai mabadiliko, hata nje ya mfumo, ambao wengine kwa kudanganywa, kwa uoga au kwa ujinga, wanauabudu! Matokeo hayaoneshi kukidhi matarajio yetu, lakini misingi imewekwa na ujumbe umefika!
ENL, umeweka tofali lako katika kuelekea MABADILIKO. Asante sana kwa kudhubutu, Mungu akubariki.
Tulitaka ukasimamie mchakato wa mabadiliko kwa dhati, ukiwa kamanda namba moja. Kuonesha Imani yetu kwako tulikupa kura nyingi zaidi ya kura alizowahi kupata mgombea wa upinzani nchini Tanzania, na labda kuna kura zako nyingi zimepotea au kupotezwa!
Maamuzi uliyo fanya ni Yale ambayo Watanzania wengi wanaogopa kufanya, sababu kubwa ikiwa ile "fear of unknown" aliyo sema Sumaye. Kung'oka kwako CCM ni sauti ya kudumu ya kuhamasisha watu kukataa mfumo kandamizi, wenye dhuluma na msingi wake ukiwa maamuzi ya wachache.
Historia itakukumbuka kwa Ujasiri wa kukataa dhuluma na kuwa tayari kudai mabadiliko, hata nje ya mfumo, ambao wengine kwa kudanganywa, kwa uoga au kwa ujinga, wanauabudu! Matokeo hayaoneshi kukidhi matarajio yetu, lakini misingi imewekwa na ujumbe umefika!
ENL, umeweka tofali lako katika kuelekea MABADILIKO. Asante sana kwa kudhubutu, Mungu akubariki.