Arusha: Yaliyojiri mapokezi ya Godbless Lema, Adai VICOBA ni umasikini, Mama lishe ni utumwa, Samia asitukanwe, Mbowe ampa kazi ya Katiba Mpya

TUNAWEZAJE KUIONDOA CCM KWA KUDHIHAKI KAZI ZA WANANCHI?

Ndio Bodaboda ni kazi Kama zilivyo kazi zingine halali.

Pikipiki ni usafiri wa umma Kama yalivyo Magari, Ndege na vyombo vingine vya usafiri Kuna wanaotumia kama chombo binafsi Cha usafiri lakini wasionavyo wanachukua kwa malipo ya route au muda.

Changamoto wanazokutana nazo maafisa Bodaboda haifanyi KAZI YA BODABODA KUWA KAZI YA LAANA.

Hakuna kazi isiyo na changamoto, hata kazi ya siasa inachangamoto ambazo Kuna watu hawatamani wao Wala watoto wao kuingia kwenye siasa.

Kama ni ajali hata mafunzi ujenzi wanapata ajali wakiwa kazini, madereva wa magari ya abiria na binafsi yakiwemo ya wanasiasa yanapata ajali na kusababisha vilema na vifo kwa madereva na abiria.

Hoja ya kwamba hakuna watoto wa vigogo kwenye kazi ya bodaboda Basi hivyo ni kazi ya laana ni mfu sana. Ukienda pale msamvu Kuna wapiga debe, ukienda kule mabondeni Kuna watu wanaopoa mchanga, wapo Machinga na mama lishe kote huko hakuna watoto wa viongozi... Je nazo hizo ni kazi za laana? Kumbuka hao wachimba mchanga, Machinga, mama ntilie nk. Hawapo tu Tanzania, hata nchi nyingine wapo.

Hatuwezi wote tukawa viongozi, hatuwezi wote tukawa wabunge, hatuwezi wote tukawa wafanyabiashara wakubwa, hatuwezi wote tukawa maaskofu.

Ndio maana lazima tutafute njia za kujikwamua kimaisha, na kazi zetu ziheshimiwe.

Wengine hatuwezi kazi za wizi wa Magari na utapeli Wala hatuwezi kutengeneza michongo ya ukimbizi ili tukalelewe na wanaume wenzetu ughaibuni.

Vijana zipendeni kazi zenu, changamoto tuendelee kukabiliana nazo na mahala pa kupaza sauti zetu tupaze, tusikatishwe tamaa na wanaobeza kazi zinazotufanya tulee familia zetu.
Kwanza huyu jamaa amerudi Tanzania Tanzania kwa hisani ya mama Samia baada ya kufutiwa kesi na kulipiwa madeni ndio maana anakosa sera/hoja anaishia kutukana bodaboda na vicoba.

MUNGU IBARIKI TANZANIA

Mwambieni LEMA kazi za laana ni wizi wa Magari na kukimbia Madeni unayodaiwa.
 
Unapowashambulia Bodaboda na Vicoba kuna mambo ya maendeleo unayakwamisha

Ni vema Chadema wakaitumia Vizuri hii ruhusa iliyotolewa na Rais Samia ya vyama vya siasa kufanya mikutano

Mlale Unono!
Ujinga na siasa tumbo au ukabila ni hatari sana, na ndio tatizo lako wewe sio kwamba hujui ukweli unapaswa kuwa upi ula kuamua kuchagua ushenzi.
 
Waambie bodaboda kuwa kazi yenu ni nzuri inalipa, mtakuwa matajiri wakubwa. Endeleeni kwa bidii, itawatoa. Wanataka kusikia hilo.

Kitokacho mdomoni hakirudi: ufanyeje: waambie nimebadilisha maoni, Mungu amenifunulia na kuniotesha. Kazi yenu imebarikiwa, mtakuwa matajiri wakubwa. Umemaliza mkwaruzano/ mtifuano.
Watanzania wengi ni wepesi kutafuta matusi na kejeli kuliko kuchangia hoja yenyewe. Kama Tanzania ingekuwa inatumia viwango vya takwimu na kutoa takwimu halisi za idadi ya ajali, vilema na idadi ya vifo vilivyosababishwa na bodaboda tangu usafiri wa bodaboda kurasmishwa kuwa biashara bila kujali kuwa polisi wana uwezo kuwasimamia kutii sheria za barabarani, ungeelewa kwa nini nchi zenye uongozi unaojitambua zimepiga marufuku biashara hii! Tunatumia hisia za kisiasa na kipato kipya bila madhara yake halisi katika jamii. Vizazi vijavyo kama vitakuwa vimezindukana kwenye usingizi pono wa kizazi hiki, watataka kufukua makaburi kupima wastani wa uzito au ukubwa wa ubongo wetu kama ulikuwa pungufu au ulikuwa na mapungufu gani hasa kuweza kuruhusu ghasia ya aina hii! Vipeperushi kwenye nchi zingine vimeandikwa kuwa na hadhari ya bodaboda, siyo simba kwenye mbuga za wanyama, ukitembelea Tanzania.
 
China wanatengeneza bodaboda lakini hakuna bodaboda, bodaboda sio Kazi ni kupoteza nguvu Kazi ya taifa.
Niambie bodaboda mwenye nyumba au gari
 
Na watoto wake wakikuwa wakawa na tabia chafu Canada watakuja kumlaani kwa kuwapeleka Ukimbizini
Karma mbaya sana

Tumuombe Mungu sana

Yeye kachagua kuwalipua wanae na mke wake na yeye kama mkimbizi ila sisi hatusemi kuwa ni laana bali ni maisha aliyochagua

Hakuna anaejua kesho tuishi kwa adabu kwenye huu mgongo wa ardhi
 
Laana ya mama yake, kuna mtu ninamfahamu anasomesha na kulea familia kwa usafiri huo huo, ajali nyingi ni wendawazimu wa wahusika.. padri akibaka hatufungi kanisa… hana adabu na ni limbukeni wa maisha, miaka miwili tu Canada anajufanya amesahau bodaboda…RIP Mr. ebbo
 
Wakuu poleni na pilikapilika za Mapokezi, hakika leo historia imeandikwa, sasa kwa vile mambo ni mengi na muda ni mchache naomba niingie moja kwa moja kwenye mada.

Baada ya Mapokezi mazito ya Nabii wa Mungu Godbless Lema, Jioni hii tena kuna Mkutano kabambe wa hadhara unaofanyika viwanja vya relini Jijini humo.

Tayari viwanja hivyo vimenona, Wananchi kwa maelfu wamejitokeza.

Hali ndio kama mnavyoiona.

View attachment 2533853View attachment 2533854

Kwa vile leo wazungumzaji ni wengi, akiwemo Baba Askofu Mwamakula basi tutaweka, vipande vya hotuba vya kila msemaji kwa ufupi ufupi.

Kama kawaida Mtumishi wenu Erythrocyte nitawaletea yote kwa uaminifu mkubwa.

Usiondoke JF

==========
UPDATES

Sugu amemuomba Gambo ajenge nyumba mapema ili asije akarudi kwenye ghetto la ukoo Ilala.
Wazee wa nyomi
 
Back
Top Bottom