Arusha: Kinana, Nape awageuza CCM "Toys"

Arusha: Kinana, Nape awageuza CCM "Toys"

Hilipendo

Senior Member
Joined
Sep 13, 2011
Posts
188
Reaction score
97
Kazi mojawapo kwenye job descriptions alizopewa Kinana ambazo ni kupata viongozi kutoka CHADEMA, imeshamshinda.

Tena yeye mwenyewe Kwa kujua au kutojua, anakiri kushindwa hayo majukumu aliyopewa na maCCM wenzake.

Kwa watu wanaofuatilia ziara za Kinana mikoani akijaribu kuinasua CCM chumba cha ICU, watakuwa wamebaini aibu aliyoipata juzi huko Ngorongoro ambapo aliingizwa mkenge na wenzake.

Wakamwekea watu wawili. Akaambiwa kuwa eti ni viongozi wakubwa au vigogo huko CHADEMA. Loh! Naye kama ilivyo kawaida ya CCM akaingia kichwa kichwa na kuwapokea jukwaani eti anapokea viongozi wa CHADEMA.

Alas! Kumbe Mzee mzima na ujeshi wake amelambishwa galasa na viongozi wake.

Kumbe hao wote alioambiwa kwamba ni vigogo wa CHADEMA kumbe wako CCM kitambo hadi mmoja amegombea uchaguzi wa Serikali za Mitaa na akabahatika kushinda nafasi Kwenye serikali za mitaa...

Leo pia kaharibikiwa huko Longido.

Si tu kwamba amelamba galasa tena Kwa mara nyingine, bali safari hii kampokea mtu aliyekuwa mlinzi wa ofisi akiambiwa ni kiongozi mkubwa wa CHADEMA, kigogo wa Wilaya ya Longido.

Tutoe wito kwa CCM; kwanza hiyo job description waliyompatia Kinana ya kuendelea kufanya siasa za ghiliba za kununua au kulaghai viongozi wa CHADEMA imeshamshinda.

Kama walimpatia target za ku-meet wajiandae kumwonesha njia aliyoelekezwa Mangula, Makamba na Mkama.

Katika hali ya umahututi wa kisiasa ambayo CCM imefikia, si Kikwete, Kinana wala kijana wao asiyejua hadhi ya mdomo wake, wanaweza kuinua chama hicho.

Tunashukuru ziara za Kinana zinashuhudia namna CHADEMA ilivyojikita akilini na mioyoni mwa watu. Hawakununuliwa wale. Hawajaghilibiwa. Ni Hoja za kisiasa zinazozungumzia maendeleo yao na mstakabali wa maisha yao na taifa hili.

Wakati Kinana katika kukimbizana na target alizopewa na aliyemtuma za kununua viongozi wa CHADEMA eti kama njia ya kushusha morali wa mapambano ya wanyonge dhidi ya mfumo na utawala mbovu, CHADEMA inaendelea kusimika mizizi si kwa wale wenye vyama tu, bali ikilenga constituent kubwa ya Watanzania ambao hawakuwahi kuwa CCM wala chama kingine cha siasa na sasa wanatambua kuwa SIASA si porojo (kama za CCM) bali ni maisha yao. Ndiyo maana waliweza kuthubutu kuamka usiku wa manane kwenda kujipanga kujiandikisha ili kupiga kura ya MABADILIKO uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.


Source: Makene.
 
Huyu Kinana hadi aondoka Arusha, atakuwa amekausha akaunti ya Chama!
 
Kinana kazi imemshinda bora akaendeleze kazi yake ya zamani
 
Huyu Kinana hadi aondoka Arusha, atakuwa amekausha akaunti ya Chama!

...kwa ajili ya kununua viongozi feki wa CDM.
Kinana, Nape na Migiro ni mizigo CCM, wanakula tu Per Diem kwa ajili ya ziara zisizo na tija kwa Chama Chao!
 
Kinaa kazeeka anasumbuka bure kujisafisha tembo alizouwa. Weka temba mbali na kinana
 
mwaka huu CCM watamuua kinana na kazi. Juzi hapa nimeona kabeba tofari la saruji huku akipanda ngazi. Haya maigizo yake siku moja atakauka akiwa katika maigizo.
 
hyena.jpg
A_green_hyena_110121-230915-035009.jpg
Green_Hyena_ID_by_Korrok.jpg
 
Kinana kazi imemshinda bora akaendeleze kazi yake ya zamani

Nawasikitikia wanaccm wanaoendelea kumuamini. Leo amekuja daraja la nadaare kata ya kisongo yani watu waliofika hawafiki hata ishiri waliojazana pale ni ule msafara wake basi. Hakuna kitu kila mtu yuko bize. Utadhani ni kikao cha dharura cha M/kiti wa kitongoji.
 
It is about time 'changes'....!the Tanzanians' citizens from Arusha are asking for a change!and so are the Tanzanians kwa ujumla wao!

Watawala amkeni...!it is about time mabadiliko!...msilazimishe mambo...!in so doing you might be pushing people somewhere else...
 
Mimi si mwanachama wa chama chochote, (neutral) ila huwa napiga kura kwa mgombea anaenivutia. Ila huwa naweza sana kuhusu kinana najiuliza vimaswali kwamba Hivi atendelea kusikiliza hizi kero zetu hata baada ya Uchaguzi??? Na pia mara ingine unamwona analima Haya ni maisha yake halisi au anajifanyisha na pia anauwezo wa kutosha kutatua hizi kero anazoambiwa au akiliwa amepata......
 
mwaka huu CCM watamuua kinana na kazi. Juzi hapa nimeona kabeba tofari la saruji huku akipanda ngazi. Haya maigizo yake siku moja atakauka akiwa katika maigizo.

Na mimi niliwaza kitu km hiko nilipomuona kavua viatu analipa. Anamdanganya nani kwa dunia ya leo? Watz wanajua yupi yuko location na yupi anafanya ukweli.
 
Kinaa kazeeka anasumbuka bure kujisafisha tembo alizouwa. Weka temba mbali na kinana

Sio hilo amenikumbusha mbali mpaka machozi.
Alishataifisha mashine ya kufulia nguo za wagonjwa Mount Meru Hospital. Sasa nawaza anavyozunguka huku na huko sio anatafuta cha kukwapua tena jamani huyu baba. Tuna uchungu sana na huyu Kinana mana ni zaidi ya jizi.
 
Yu wapi Dead wood; Juliana Shonza akanushe taarifa hii?!
 
Ccm lazima watajua cheusi chekundu Machali wa Chuga watawachezesha gwaride pole yao
 
Kazi mojawapo kwenye job descriptions alizopewa Kinana ambazo ni kupata viongozi kutoka CHADEMA, imeshamshinda.

Tena yeye mwenyewe Kwa kujua au kutojua, anakiri kushindwa hayo majukumu aliyopewa na maCCM wenzake.

Kwa watu wanaofuatilia ziara za Kinana mikoani akijaribu kuinasua CCM chumba cha ICU, watakuwa wamebaini aibu aliyoipata juzi huko Ngorongoro ambapo aliingizwa mkenge na wenzake.

Wakamwekea watu wawili. Akaambiwa kuwa eti ni viongozi wakubwa au vigogo huko CHADEMA. Loh! Naye kama ilivyo kawaida ya CCM akaingia kichwa kichwa na kuwapokea jukwaani eti anapokea viongozi wa CHADEMA.

Alas! Kumbe Mzee mzima na ujeshi wake amelambishwa galasa na viongozi wake.

Kumbe hao wote alioambiwa kwamba ni vigogo wa CHADEMA kumbe wako CCM kitambo hadi mmoja amegombea uchaguzi wa Serikali za Mitaa na akabahatika kushinda nafasi Kwenye serikali za mitaa...

Leo pia kaharibikiwa huko Longido.

Si tu kwamba amelamba galasa tena Kwa mara nyingine, bali safari hii kampokea mtu aliyekuwa mlinzi wa ofisi akiambiwa ni kiongozi mkubwa wa CHADEMA, kigogo wa Wilaya ya Longido.

Tutoe wito kwa CCM; kwanza hiyo job description waliyompatia Kinana ya kuendelea kufanya siasa za ghiliba za kununua au kulaghai viongozi wa CHADEMA imeshamshinda.

Kama walimpatia target za ku-meet wajiandae kumwonesha njia aliyoelekezwa Mangula, Makamba na Mkama.

Katika hali ya umahututi wa kisiasa ambayo CCM imefikia, si Kikwete, Kinana wala kijana wao asiyejua hadhi ya mdomo wake, wanaweza kuinua chama hicho.

Tunashukuru ziara za Kinana zinashuhudia namna CHADEMA ilivyojikita akilini na mioyoni mwa watu. Hawakununuliwa wale. Hawajaghilibiwa. Ni Hoja za kisiasa zinazozungumzia maendeleo yao na mstakabali wa maisha yao na taifa hili.

Wakati Kinana katika kukimbizana na target alizopewa na aliyemtuma za kununua viongozi wa CHADEMA eti kama njia ya kushusha morali wa mapambano ya wanyonge dhidi ya mfumo na utawala mbovu, CHADEMA inaendelea kusimika mizizi si kwa wale wenye vyama tu, bali ikilenga constituent kubwa ya Watanzania ambao hawakuwahi kuwa CCM wala chama kingine cha siasa na sasa wanatambua kuwa SIASA si porojo (kama za CCM) bali ni maisha yao. Ndiyo maana waliweza kuthubutu kuamka usiku wa manane kwenda kujipanga kujiandikisha ili kupiga kura ya MABADILIKO uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.


Source: Makene.

Wale fisi hawana soko mahala nje ya nchi??
 
Back
Top Bottom