Arusha: Hongera Monaban (Mollel), CCM umeibeba vya kutosha

Arusha: Hongera Monaban (Mollel), CCM umeibeba vya kutosha

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Nipo Arusha kwasasa kwa shughuli binafsi. Nitakwenda pia Manyara. Lakini, mwanasiasa haachi siasa. Nimejikuta nimefuatilia kilichojiri na kinachoonekana hapa Arusha kisiasa. Ninashuhudia CCM dhaifu kuliko mkoa wowote wa Tanzania Bara (kwakuwa Pemba inazidi). Nashuhudia CCM ikijifichaficha kufanya siasa na CHADEMA wakitamba watakavyo.

Nashuhudia kila kona,kila nyumba CCM ikibezwa na kumezwa. Kila kona, kila nyumba CCM inasemwa vibaya bila haya kwa kila mwanakaya. CCM ni kama haipo Arusha. CCM inanyanyasika vya kutosha na kutisha hapa Arusha. Nikawakumbuka wakuu mmaranguoriginal na sirluta. Jinsi wanavyojitahidi kufa na tai zao shingoni.

Kutokana na niyaonayo, nampongeza Bwana Mollel aliyekuwa mgombea wa CCM yetu hapa Arusha. Kwa kupata kura zaidi ya thelathini elfu. Bwana Mollel almaarufu kama MONABAN amekibeba vya kutosha chama chetu. Amekipunguzia aibu ya kupata kura kiduchu hapa Arusha.

Hakuna propaganda itakayoiponya CCM Arusha zaidi ya kuhuishwa. CCM Arusha wana kazi ya kufanya. Mkuu MUSSA ALLAN, tafadhali rudi kundini tukirejeshe chama chetu kwenye mstari hapa Arusha. CCM haistahili kupata manyanyaso ya aina hii. Ingawa Lema anakubalika, lakini nasi yatupasa kutikisa.

Kuna kazi kubwa ya kufanyika!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Arusha)
 
Last edited by a moderator:
Ni ngumu sana ku deal na watu walioamua kuchagua viongozi/chama based on ethnic groups. Watakapoelimika watafanya maamuzi sahihi
 
Nilikuwa nimesema kabla kwamba kama Lema hangeshinda kura zaidi ya 30 elfu ningejitoa jf
 
Monaban anakata rufaa kama hujui
Hata Wassira pia, Kafulila, na wengineo CCM na UKAWA. Ni haki yao, kwa hiyo acha akate tu rufaa. Kama ana sababu za msingi atashinda. nakumbuka hata 2010 Lema alikatiwa rufaa.
 
Monaban anakata rufaa kama hujui

Hata Wassira naye anakata rufaa, na sababu kubwa ni kuwa mila za mkoa wa Mara zimekiukwa kwa kuruhusu Mwanamke kumgaragaza mwanamume. Tena mwanamume mwenyewe bonge la baba kama alivyo Steven.
Sijui sababu hizo zina sound kisheria? Mie sijui.
 
Hiyo rufaa ni ya kujifurahisha tu. Arusha hata agombee Magufuli CCM hamtoshinda
Uko sahihi...ushahidi ni yeye kupata kura 65 elfu wakati Lowassa kapata zaidi ya kura 150 elfu! Kama ilivyo kwa maeneo ambayo CCM ni "kila kitu", Arusha wanaichukulia CHADEMA kuwa "kila kitu".
 
Ni ngumu sana ku deal na watu walioamua kuchagua viongozi/chama based on ethnic groups. Watakapoelimika watafanya maamuzi sahihi

Huijui Arusha wewe,Ni very cosmopolitan Ni mchanganyiko WA makabila mengi wanaojitambua sio mangombe wasioelimika kama Dodoma
 
Lakini hata ufahamu wa wana Arusha ni tofauti na dodoma na Sumbawanga
 
Ni ngumu sana ku deal na watu walioamua kuchagua viongozi/chama based on ethnic groups. Watakapoelimika watafanya maamuzi sahihi

Bw. Mollel (Monaban) ni kabila gani? Wewe ni kabila gani? Watu wa jimbo la uchaguzi Arusha ni kabila gani? Watu 30,000 waliompa kura Mollel ni kabila gani?
 
Hizo kura kapata baada ya vijana wengi kukata tamaa ya kupiga kura, ingefanyika tar 25 oct, watu walikuwa na hamasa lema angeshinda kwa 80%
=> uelewa wa watu/vijana arusha ni tofauti na dodoma pwani ruvuma watu wanawaza mabadiliko tu!
 
Kama vile Matonya wa Dodoma na Waswahili wa Msoga
Huu ni ushahidi tosha kwamba Rais wa Taifa hili kamwe hatatoka huko "kaskazini". Si kwa kizazi hiki tu bali na vizazi vyako vyote vijavyo. Tulia utawaliwe, huna budi mpuuzi mkubwa wewe na vijidharau vyako visivyo na tija.
 
Back
Top Bottom