Arumeru Mashariki, CHADEMA kunyakua jimbo?

Arumeru Mashariki, CHADEMA kunyakua jimbo?

Tetesi!
Nasikia ccm wamemtuma siyoi na chligati kukutana na lowasa kumwomba rasmi kuweka nguvu zake hadharani katika kuhakikisha jimbo linabaki chini ya miliki yao. Hii ni kutokana na nguvu ya chadema ktk jimbo hilo, ccm kujikuta hoehae kipesa na kikubwa zaidi ni nguvu aliyonayo lowasa katika jimbo hilo ukichukulia kuwa yeye kazaliwa tengeru jimboni humo na mama yake ni mmeru na hata best man wake wa ndoa ni mmeru kutoka ukoo wa Nyiti.
 
Kweli nimekuja kugundua hii nchi inawatu wazembe wa kufikiri,hivi hichi chama hakina mtu makini wa kuwafungulia kampeni
 
Ngoja tusubiri....kwani CC ya CCM jana ilimpitisha SIOI au? sina updates please nisaidieni?
 
Kwanza naamini kabisa siku hiyo ya ufunguzi wa kampeni ya CCM Mkapa atakuwa ameutwisha, yaani kaunyaka vilivyo. Anafanya hivi ili kuondoa macho ya aibu mbele ya Watz kutokana na madhambi aliyofanya kwao.

Lakini hapa CDM wakicheza karata yao vizuri wanaweza kuibomoa CCM live kabisa. Nawashauri wapange mkutano wao wa ufunguzi baada ya huo wa Mkapa, hasa siku ya pili yake. Halafu wampeleke Marando na Tundu Lissu na Lema kummaliza Mkapa.

Umenivunja mbavu. Mlevi sana huyu hasa siku hizi anapokuwa majukwaani, ni matusi matupu dhidi ya wapinzani. Huko Igunga aliunyaka kisawasawa. Tatizo wapinzani wakiongea kama yeye, vyombo vya serikali ya CCM hurukia na kusema eti matusi hayatakiwi.

Nakubaliana kabisa na hoja kwamba Mkapa ni 'nyama' nzuri ya kuvuruga CCM na mafisadi wao wanaotaka kuwakampenia. Shame upon you CCM!!!!!!
 
Acha kuvunja mioyo ya watu. Ina maana Warumeru wao kazi yao ni kulaghaiwa na akina L? It seems they don't use their common sense.......lo!
 
Kwa upande mwingine, nafikiri Mkapa anakubali kazi hiyo kwa sababu hana njia ya kukataa. Anataka kulindwa na ufisadi wake, hivyo ni lazima ajikombe sana kwa viongozi wa CCm waliopo sasa -- kwa kuogopa kupandishwa kizimbani. Hivyo ndivyo mchezo wa siasa ktk nchi hii unavyochezwa.
 
Mkuu umetoa hoja yenye maana sana, si vizuri kuibeza kishabiki kwa kuwa haija ridhisha nafsi, matarajio, mapenzi na matakwa binafsi. Hapa la msingi sio kwamba chadema wasahau ushindi, la hasha; bali hii hoja iwe chachu ya kuongeza juhudi binafsi katika mapambano ya haki, kuelimisha wana arumeru, na kubwa zaidi kulinda kura zetu. Lowasa kweli mzaliwa wa meru na mama yake mmeru original na best man wao alitoka ktk ukoo wa Nyiti ambao ndo hao washiri. Vilevile vijana wengi wa kimeru hawajendaa shule wameishia mererani kutumikishwa ktk machimbo na hawajajiandikisha, sio wakutegemewa na upinzani ulio makini. Tujipange la sivyo mtoa hoja hajakosea.
 
Tetesi!
Nasikia ccm wamemtuma siyoi na chligati kukutana na lowasa kumwomba rasmi kuweka nguvu zake hadharani katika kuhakikisha jimbo linabaki chini ya miliki yao. Hii ni kutokana na nguvu ya chadema ktk jimbo hilo, ccm kujikuta hoehae kipesa na kikubwa zaidi ni nguvu aliyonayo lowasa katika jimbo hilo ukichukulia kuwa yeye kazaliwa tengeru jimboni humo na mama yake ni mmeru na hata best man wake wa ndoa ni mmeru kutoka ukoo wa Nyiti.
Wakati jimbo la Arusha mjini likichukuliwa na kamanda Lema kwani wakati huo alikuwa hakuzaliwa tengeru.
 
Hehehe Chadema ni vizuri kama itatoa upinzani kwa ajili ya kujiandaa kwa 2015. Sema point ya daftari la kudumu uliyotoa ni ya msingi ni vizuri chadema wenyewe wakachukua initiative kuhakikisha watu wao esp vijana wanajiandikisha.
 
Unaweza ukawa na point mkuu lakini matokeo ya mwaka jana yana reflect kitu fulani hvi,ngoja tuone kikubwa ni kulinda kura na kuendelea kutoa elimu ya uraia tu!magamba wako ukingoni,na uwa naudhunika sana mimi kama mtanzania kuona watanzania tumeanisha akili zetu na kuzilisha ujinga kua Lowassa aliyechafuka ni mtu mwenye nguvu katika chama chake na nchi pia kiasi kwamba anaweza fanya lolote kwa nchi!wengine tena hata humu jamii forums wamekua ni wafu wa mawazo na akili kwa kushabikia L bila kujua hizo hela zimepatikanaje kwake!hii ni aibu kwa taifa kwani linaonekana ni taifa lililo na watu wasio na uwezo wa kufikiri tena kwa vitu hata vidogo tu visivyohitaji akili nyingi kufikiri
 
Yaliyonenwa hapo juu ni ukweli mtupu na ndicho kinachokuja kutokea
 
Mkuu umetoa hoja yenye maana sana, si vizuri kuibeza kishabiki kwa kuwa haija ridhisha nafsi, matarajio, mapenzi na matakwa binafsi. Hapa la msingi sio kwamba chadema wasahau ushindi, la hasha; bali hii hoja iwe chachu ya kuongeza juhudi binafsi katika mapambano ya haki, kuelimisha wana arumeru, na kubwa zaidi kulinda kura zetu. Lowasa kweli mzaliwa wa meru na mama yake mmeru original na best man wao alitoka ktk ukoo wa Nyiti ambao ndo hao washiri. Vilevile vijana wengi wa kimeru hawajendaa shule wameishia mererani kutumikishwa ktk machimbo na hawajajiandikisha, sio wakutegemewa na upinzani ulio makini. Tujipange la sivyo mtoa hoja hajakosea.

Nakubaliana nawe kiongozi
 
Siwezi kusema chochote kwa kuwa siijui Arumeru wala wakazi wake ila najiandaa kwenda kujionea. Nikifika huko nitasema.
 
Wanajamvi:

Habari nilizopata kutoka Arumeru kwamba vijana wengi wa CCM huko wanaona hawaafiki hatua ya chama chao kumtumia fisadi ambaye wamempachika jina la ‘baba wa ufisadi’ – yaani Benjamin Mkapa kufungua na kufunga mikutano ya kampeni.


Wanasema huyu anahusika sana na kuruhusu ufisadi wa EPA, Deep Green, Radar, kuuza nyumba za serikali na mengineyo, na wanadai bila shaka alifaidika na fisidi hizo dhidi ya wananchi wa Tanzania

Wanasema pia Mkapa alijimilikisha mgodi wa makaa yam awe wa Kiwira. Hivyo wanasema ni tusi kubwa kwa wakazi wa Arumeru na Watanzania kwa ujumla kumteua fisadi huyo kuwafungulia kampeni kwani wanaona ana husika sana katika kuifilisi nchi na hivyo kuwafanya vijana wan chi hii kukosa mwelekeo – kuwapo kwa elimu duni na kuzorota kwa huduma nyingine za serikali kwa raia.

Kuna wengine wanasema siku ya mkutano wa kampeni watakwenda na mabango kuwakumbusha wananchi wa Arumeru kuhusu uovu wa mtu huyu.

2pe source ya habari?
 
Kama tuna watanzania 30% tu wenye mawazo mgando kama hayo then hii nchi kwisha kabisa. Hivi huyu Lowasa ni nani na ana nini cha ajabu kiasi cha kuwafanya watanzania kumuogopa na kusujudia mambo yake kwa kiasi hicho? Kitu chochote anachotia mkono Lowasa basi kila mtu anaona ndo kitakachokuwa.

Tabia hii niliiona kipindi kile cha JK alipokosa nafasi ya urais, kila alichokuwa anakifanya watu waliona hakuna mtu kama yeye. he endup kuwa Rais wa Tz. haya mniambie katufikisha wapi!

Huyu Lowasa mnaemwambudu ni janga jingine la kitaifa, Mungu apishie mbali asijepewa utawala wa hii nchi. Watanzania tutajuta mara 100 ya sasa tunavyojuta under JK. Narudia tena mtu yeyote m-binafsi anaeweka utukufu wake mbele kama EL ni janga kubwa.

Watanzania tujitahidi kuzuia janga hili kabla halijatumeza. Lets finish Lowasa and the Gang AND their CCM as whole.
 
Nionavyo mimi hapo kwenye red pafanyiwe kazi sana. hawa watu ni illiterate sana kiasi hawawezi kuwa na msimamo hata kidogo. You might be right. Lakini matokeoa ya uchaguzi uliopita yanaonyesha anakubalika. Lakini watu hawaaminiki.
kulinganisha na watu gani?.... karatu? au kigoma kaskazini?
 
Hao hawana tofauti na ndege wanaoitwa Chichi dodo ambao hawataki kugusa kinyesi lakini wanakula funza watokanao na kinyesi.
 
Back
Top Bottom