Aris TPSC Dar kwanini mnabadili matokeo ya wanafunzi?

Donatila

JF-Expert Member
Oct 23, 2014
7,557
21,497
Habari wakuu,

Nina mtoto wa ndugu yangu namsomesha Chuo Cha Utumishi wa Umma Dar (TPSC) kimezoeleka kwa jina la Magogoni..

Ni mara ya pili matokeo ya mtoto wa ndugu yangu yamebadilishwa..

Nimeona nilete huku maana wahusika hawataki kufanyia kazi.

Pia sio huyu mtoto wa ndugu yangu tu anasema hili ni tatizo kwa wanafunzi wengi na wahusika wa chuo wamekaa kimya.

Matokeo yakitoka yanakuwa yamewekwa katika mtandao wao wa aris TPSC.

Sasa cha kushangaza mtoto alileta matokeo yake ya kwanza kapata B 4 na C 1 akafurahi na mimi nikafurahi kafaulu.

Baada ya waliofeli kurudia mtihani na matokeo kuwekwa. Amekuta na yeye yamebadilishwa ana B3 na C2.

Kwenda kufuatilia anaambiwa ni kazi kurudisha yawe kama zamani.

Kama kuweka matokeo mtandaoni kumewashinda rudisheni ubaoni...

Sasa wakuu...kweli ni haki kubadili matokeo ya mwanafunzi?

Huu ni uonevu...na pia inavunja moyo wa mwanafunzi kusoma.


Naweka matokeo ya awali na yaliyobadilishwa..
 
Ki msingi haya matatizo yapo kwenye Mifumo sio wanabadirisha. Miaka yangu mitatu yote ya chuo nime experience hii shida.

Wakirekebesha mfumo matokeo yanakaa poa. Ukitaka matokeo halisi mwanafunzi au mzazi nenda Idara au kwa Examination officer utapewa print out ya progression report. Kama evidence
 
Ukiyaweka hapa matokeo unakuwa umemdhalilisha bint na chuo chenyewe pia,ni vizuri ukaenda mwenyewe chuo ukaonana na uongozi mkajua la kufanya kuliko hapa mtandaoni
Hawataki kubadilisha...mtoto alifwata...jibu alilopewa...amekata tamaa
 
Wasomi Ndiyo Wanaotuangusha Sasa Hivi
Mtu Anasoma Anapata B 4 Baadaye B 3 Halafu Unafikiria Angekuwa Wa Darasa La Saba B Angefanya Hivyo
 
Wakati wa kuweka kumbuka kuficha Reg. Ya mtoto maana unapoelekea utamletea matatizo zaidi. Ikiwezekana hata baadhi ya masomo ficha
Ha ha kweli
tapatalk_1566666533217.jpeg
 
Wasomi Ndiyo Wanaotuangusha Sasa Hivi
Mtu Anasoma Anapata B 4 Baadaye B 3 Halafu Unafikiria Angekuwa Wa Darasa La Saba B Angefanya Hivyo
Umeona mkuu...saivi dogo atakuwa asomi mikarai tu atapata..
 
Nadhani ingekuwa vyema zaidi Donatila kama lalamiko lingepelekwa chuoni.

Wanafunzi wamepeleka hawasikilizwi...wazazi nendeni mtapewa jibu.
 
Basi kuna tatizo mahali tena kubwa tu. Hakuna haja ya mtihani kama matokeo yanayotoka siyo halali ya mwanafunzi...kama wahadhiri wanatakiwa walitatue haraka.
Limefika hapa JF...litatatuliwa
 
Back
Top Bottom