"Appointment" ilikua enzi zetu

Elli

Platinum Member
Mar 17, 2008
55,500
86,042
Ni mchana tulivu wa Jumapili hii, nimekumbuka mbali sana nikaamua tushee hii habari, kila nikiangalia vijana wa siku hizi wanaofanya miadi kwa simu naona kama vile wanamisi utamu fulani hivi, haina raha kuulizana kila saa umefika wapi "Dear" mbona hufiki? Mbona unakawia sana? aaah hii haina raha kabisa. Ona uzoefu wangu kipindi hicho....

Tumekutana Jumamosi hiii na inabidi tukutane jumapili ijayo, kwahio tunapata muda. Tutakutana kwene kona ileee chini ya ule mti jiarni na kale kamto pale bondeni saa nane na nusu, kwa hio baada ya hapo mnaachana kila mtu anaeda zake. Unasubiri wiki nzima then jumapili inafika, kuna jua kali kama la leo....unatafuta sababu ya kutoka home...unaipata. Taratiiibu unaanza kujongea sehemu ya tukio, ni saa nane na ROBO nakaribia eneo la tukio, hakuna kitu!! Najivuta mbele kidogo jua ni kali mara kwa mbaaali kidogo namuona binti anakuja ameshika kijifimbo anapiga piga majani!!! Ni saa nane kama dakika 31 hivi, tunasalimiana na kujuliana hali then tunaenda kukaa eneo letu la tukio. Ni saa kumi na moja na kidogo tunaamua kuagana na kurudi makwetu hadi jumamosi tena saa tisa maana "Baba Mkwe" to be atakuepo home bado.

Ni jumamosi imefika kwa shida sana ile ahadi imekua ikinitesa sana maana kila sekunde inakua kama lisaa, najivuta tena leo tunaenda kukutana chini ya jiwe fulani jirani kidogo na mto kuna mti wa Eucalyptus (sp), leo nachelewa kidogo kama dakika chache hivi ila namkuta mtoto ameshafika anacheza cheza na vijiti na matete, pana ka upepo kazuri kweeli. Huwezi amini tunakaa hapo hadi saa kumi na moja na nusu!!!!! Tunaagana kwa furaha na kurejea makwetu kila mtu karidhika sana, tunapotembea kila dakika tunageuka nyuma na kuagana tena, hadi tunakatisha kona na hapo hakuna anemuona mwenzie tena!!!!!

Tumeenda shule sasa, tuko mbali mbali ila tunawasiliana kwa barua hasa "Airform" sijui kama bado zipo, zilikua very cost-effective. Barua zimepambwa hadi raha, unaisoma, unaiweka chini ya mto, mmmhh unasoma shule ya Boys tupu, mwenzio yuko kwene Co-school. Ahhhhhh ni raha sana.

Tumerudi tena home, appointment zetu zinaendelea vizuri, nimeombwa nifike home maana baba hatakuepo! Najipiga moyo konde nimeambiwa nifike saa nane maana baada ya muda huo baba atakua ameshakula lunch na kupumzika kidogo na kuondoka kuelekea mjini. Nimefika tayari, nimejificha kwene vichaka, namsubiria Dingi atoke ili nitume mtu au nijipitishe pale nje anione!!! Inaenda kama ilivyopangwa, ni ahadi kamilifu sana hadi raha, anavyinisindikiza kuna kua na hali ya mvua, inabidi tujifiche chini ya msitu kwene miti ili mvua ipite, kumbe nimevaa koti la Jinzi la "kuchovya" (kwa wale wanaokumbuka-kuchovya). Ndani nimevaa Tisheti nyeupe, duh najikuta ile rangi yote imehamia kwene tisheti, mmmhh bado ni upendo tu.

Jamani nina mengi yanayodhihirisha kuwa appointment za enzi zile zilikua tamu sana, yaani unapomuona mpenzio hadi raha, mmmh nimemkumbushia leo ikiwa ni miaka kibao imepita tumeishia kucheka tu. Wewe je uzoefu wako ukoje? Kikubwa ni kwamba baada ya miaka yote hio ya appointment za tabu tulikuja kuoona, appointment za simu hazina ladha jamani!!!! Jumapili njema
 
Airform!! kweli wakati unakimbia. Kwa kweli enzi hizo, kupata kitu roho inataka, ilikuwa ni struggle kweli kweli. Maana ile kuonekana kijana wa kiume akiongea na wa kike, ilikuwa ni tendo lililokuwa linatafsiriwa kwa tahadhari sana.
 
Hio ni mfano michache sana sikutaka kuwachosha ila dah asikwambie mtu
 
Mkuuu sisi vijana wa siku hizi 2napata matatizo sana ukipanga ukutane na mpenzi wako hatokei ukipiga simu hapokei mpaka um2mie buku mbili ndio anapokea simu

alafu cha kushangaza ukim2mia vocha akipata anakubip umpigie ndio akwambie asante ili hali umem2mia buku kumi
 
Pole sana Mpwa, kwakweli sie enzi zile hakukua hata na kuhongana, yaani ilikua ni true love kweli kweli, tatizo ilikua siafu na matawi ya miti!!! I wish nyakati zile zingerudi, kweli nyakati zile zilikua tamu kweli, nilikuja kusoma kitabu kinaitwa Weep Not Child na chenyewe kilikua na element hizo za appointment ninazozingumzia.
Mkuuu sisi vijana wa siku hizi 2napata matatizo sana ukipanga ukutane na mpenzi wako hatokei ukipiga simu hapokei mpaka um2mie buku mbili ndio anapokea simu

alafu cha kushangaza ukim2mia vocha akipata anakubip umpigie ndio akwambie asante ili hali umem2mia buku kumi
 
Niliishi enzi hizo lakini sizitamani kabisaaa, ni sawa na mkulima wa jembe la mkono apatiwe power tiller halafu aseme haifanyi kazi vizuri kama kutifua kwa mkono. siku hizi hata mtu aliye marekani wewe upo bongo kijijini mnapanga as if mko katika nyumba moja tofauti nivyumba tu. kwa hiyo ndugu yangu nakuomba ubadilike kufuatana na wakati, ndio maana nimeona watu waliotoa maoni kuhusu mabadiliko ya katiba wakapendekeza watu wenye umri zaidi ya miaka 60 wasipige kura, hapa naanza kukubaliana nao, kwani vijana wanaona tunawacheleweshea maendeleo kwani tuna mawazo mgando.
 
sintosahau nilipomwagiwa maji ya ukoko baada ya kupewa appointment nijibanze chini ya dirisha la jikoni huku nikiimba kawimbo ka ni miyo mahoza nitangwa mahoza nihoze viima nihoze viima uko shambaai wavika ughanga wavika ughanga tate na mame wakunda kutoana wakunda kutoana aii mamemee.

Binti aliniambia saa mbili kamili niimbe hako kawimbo nikiwa niko usawa wa dirisha na atakaposikia atatoka au kumtuma.Kwakuwa niliwahi 10minutes kabla ya muda nilishikadirisha ili niruke niangalie kwasababu dirisha lilikuwa juu kidogo ilinicheeki kama mpenzi yupo ndani anapikawakati najiandaa kuruka mama mtu akarusha maji ya ukoko dirishani na kwakuwa appointment hii nikiimisi lazima nisubirie wiki nyingine ilibidi nisiondoke nikakaa hadi muda ulipofika nikaimba nikasikia mtoto akiaga ndani kuwa anakwenda kuchukua kitabu cha sayansi kimu kwa rafiki yake hivyo wakamwambia mdogo wake wa kiume ambaye alikuwa na miaka 9 amsindikize ambaye baadaye tulimuacha nje akicheza na wenzake mchezo wa baba na mama huku wakipika Vieng'a(binti alichukua chenga za mchele wakati anatoka ndani).

Sisi tukaenda kuchukua kitabu cha sayansi kimu kwa rafiki yake halafu tukaenda zetu kwenye majengo ya shule na kuchagua Darasa moja tukakaa ndani na kuendelea na maongezi yetu.

Hakika sinto msahau binti huyu ambaye baadaye alikuja kuwa my wife tukikumbushia enzi hizo maana pamoja na maukoko kulowanisha nguo zangu lkn hatukujali utakuta hatuna mbavu
 
imeifanya jumapili iwe njema sana kwangu, kwani nimetabasam peke yangu.! Hasa hiyo jinsi ya kuchovya nakumbuka walikua wanarusha mnadani.!
 
Mmenikumbusha mbali sana. Enzi za kujipaka sabuni mwilini baada ya kuoga kwa kuwa mafuta ya kujipaka hamna halafu kichwani unapitisha kwaruzo.Unapigilia shati la kubana na suruali ya pekoz na chini raizon ya bora, hakika mambo ni tofauti sana siku hizi.
 
Ni mchana tulivu wa Jumapili hii, nimekumbuka mbali sana nikaamua tushee hii habari, kila nikiangalia vijana wa siku hizi wanaofanya miadi kwa simu naona kama vile wanamisi utamu fulani hivi, haina raha kuulizana kila saa umefika wapi "Dear" mbona hufiki? Mbona unakawia sana? aaah hii haina raha kabisa. Ona uzoefu wangu kipindi hicho....

Tumekutana Jumamosi hiii na inabidi tukutane jumapili ijayo, kwahio tunapata muda. Tutakutana kwene kona ileee chini ya ule mti jiarni na kale kamto pale bondeni saa nane na nusu, kwa hio baada ya hapo mnaachana kila mtu anaeda zake. Unasubiri wiki nzima then jumapili inafika, kuna jua kali kama la leo....unatafuta sababu ya kutoka home...unaipata. Taratiiibu unaanza kujongea sehemu ya tukio, ni saa nane na ROBO nakaribia eneo la tukio, hakuna kitu!! Najivuta mbele kidogo jua ni kali mara kwa mbaaali kidogo namuona binti anakuja ameshika kijifimbo anapiga piga majani!!! Ni saa nane kama dakika 31 hivi, tunasalimiana na kujuliana hali then tunaenda kukaa eneo letu la tukio. Ni saa kumi na moja na kidogo tunaamua kuagana na kurudi makwetu hadi jumamosi tena saa tisa maana "Baba Mkwe" to be atakuepo home bado.

Ni jumamosi imefika kwa shida sana ile ahadi imekua ikinitesa sana maana kila sekunde inakua kama lisaa, najivuta tena leo tunaenda kukutana chini ya jiwe fulani jirani kidogo na mto kuna mti wa Eucalyptus (sp), leo nachelewa kidogo kama dakika chache hivi ila namkuta mtoto ameshafika anacheza cheza na vijiti na matete, pana ka upepo kazuri kweeli. Huwezi amini tunakaa hapo hadi saa kumi na moja na nusu!!!!! Tunaagana kwa furaha na kurejea makwetu kila mtu karidhika sana, tunapotembea kila dakika tunageuka nyuma na kuagana tena, hadi tunakatisha kona na hapo hakuna anemuona mwenzie tena!!!!!

Tumeenda shule sasa, tuko mbali mbali ila tunawasiliana kwa barua hasa "Airform" sijui kama bado zipo, zilikua very cost-effective. Barua zimepambwa hadi raha, unaisoma, unaiweka chini ya mto, mmmhh unasoma shule ya Boys tupu, mwenzio yuko kwene Co-school. Ahhhhhh ni raha sana.

Tumerudi tena home, appointment zetu zinaendelea vizuri, nimeombwa nifike home maana baba hatakuepo! Najipiga moyo konde nimeambiwa nifike saa nane maana baada ya muda huo baba atakua ameshakula lunch na kupumzika kidogo na kuondoka kuelekea mjini. Nimefika tayari, nimejificha kwene vichaka, namsubiria Dingi atoke ili nitume mtu au nijipitishe pale nje anione!!! Inaenda kama ilivyopangwa, ni ahadi kamilifu sana hadi raha, anavyinisindikiza kuna kua na hali ya mvua, inabidi tujifiche chini ya msitu kwene miti ili mvua ipite, kumbe nimevaa koti la Jinzi la "kuchovya" (kwa wale wanaokumbuka-kuchovya). Ndani nimevaa Tisheti nyeupe, duh najikuta ile rangi yote imehamia kwene tisheti, mmmhh bado ni upendo tu.

Jamani nina mengi yanayodhihirisha kuwa appointment za enzi zile zilikua tamu sana, yaani unapomuona mpenzio hadi raha, mmmh nimemkumbushia leo ikiwa ni miaka kibao imepita tumeishia kucheka tu. Wewe je uzoefu wako ukoje? Kikubwa ni kwamba baada ya miaka yote hio ya appointment za tabu tulikuja kuoona, appointment za simu hazina ladha jamani!!!! Jumapili njema

Mkuu KUWA MTU UNAYEPENDA MABADILIKO.Mimi mwenyewe nina umri mkubwa tu kwani nimezaliwa miaka ya 1960 lakini sipendi maisha ya enzi hizo kwani yalikuwa ni ya shida tu.Vitu vingi tulivyonavyo sasa havikuwapo hapo zamani eg mobile phones,TV NA VINGINEVYO.kwa hiyo unakuta unapanga appointment na demu mkutane sehemu flani lakini ukitangulia kufika ile sehemu na ukakuta kuna kiwingu huwezi kubadilisha mahali pa kukutana tena kwa sababu ya kukosekana mawasiliano ya mbali ambayo ni ya haraka hivyo unaamua kuondoka.Hata hivyo uzuri wa zamani ni kuwa kulikuwa hakuna UKIMWI hivyo ilikuwa ukila demu ulikuwa huna wasi wasi sana kama sasa.Anyway u must change from Analog to Digital life.
 
hahahaaaa asante sana, i think tunakosa mengi
Mmenikumbusha mbali sana. Enzi za kujipaka sabuni mwilini baada ya kuoga kwa kuwa mafuta ya kujipaka hamna halafu kichwani unapitisha kwaruzo.Unapigilia shati la kubana na suruali ya pekoz na chini raizon ya bora, hakika mambo ni tofauti sana siku hizi.
 
Hahahhaaa mie mkwe wangu alikua ana presha na kisukari so hakua na nguvu sana ila naskia alikua anudhika sana nikikutana nae maeneo kisha binti akachelewa kurudi basi ilikua full shida, alikua na Gobole
sintosahau nilipomwagiwa maji ya ukoko baada ya kupewa appointment nijibanze chini ya dirisha la jikoni huku nikiimba kawimbo ka ni miyo mahoza nitangwa mahoza nihoze viima nihoze viima uko shambaai wavika ughanga wavika ughanga tate na mame wakunda kutoana wakunda kutoana aii mamemee.

Binti aliniambia saa mbili kamili niimbe hako kawimbo nikiwa niko usawa wa dirisha na atakaposikia atatoka au kumtuma.Kwakuwa niliwahi 10minutes kabla ya muda nilishikadirisha ili niruke niangalie kwasababu dirisha lilikuwa juu kidogo ilinicheeki kama mpenzi yupo ndani anapikawakati najiandaa kuruka mama mtu akarusha maji ya ukoko dirishani na kwakuwa appointment hii nikiimisi lazima nisubirie wiki nyingine ilibidi nisiondoke nikakaa hadi muda ulipofika nikaimba nikasikia mtoto akiaga ndani kuwa anakwenda kuchukua kitabu cha sayansi kimu kwa rafiki yake hivyo wakamwambia mdogo wake wa kiume ambaye alikuwa na miaka 9 amsindikize ambaye baadaye tulimuacha nje akicheza na wenzake mchezo wa baba na mama huku wakipika Vieng'a(binti alichukua chenga za mchele wakati anatoka ndani).

Sisi tukaenda kuchukua kitabu cha sayansi kimu kwa rafiki yake halafu tukaenda zetu kwenye majengo ya shule na kuchagua Darasa moja tukakaa ndani na kuendelea na maongezi yetu.

Hakika sinto msahau binti huyu ambaye baadaye alikuja kuwa my wife tukikumbushia enzi hizo maana pamoja na maukoko kulowanisha nguo zangu lkn hatukujali utakuta hatuna mbavu
 
Back
Top Bottom