Ndugu yangu historia ni mwalimu mzuri sana; kama ukirudisha mkanda nyuma ukajiuliza ni kwa nini Anne Makinda ni spika wa bunge la Tanzania, alifikafika je katika nafasi hiyo na katika mazingira gani unapata jawabu lisilo na mashaka; agenda ilikuwa kumg'oa Mzee wa kasi na viwango Samuel Sitta ambaye CCM walikuwa wanamtuhumu kwa kukisaliti chama chake kwa sababu alikuwa anawapa wabunge wa upinzani nafasi sawa ya kuchangia hoja mbali mbali jambo ambalo lilisababisha madudu mengi ya serikali ya CCM kuibuliwa na kuwekwa hadharani; kashfa moja kubwa ilikuwa ile ya RICHMONDULI iliyomg'oa Edward Lowassa kutoka kwenye uwaziri mkuu, kwa hiyo ukaasisiwa mkakati wa kumg'oa Sitta akawekwa Makinda na matokeo yake ndio sindimba unayoiona bungeni sasa hivi, makinda, naibu wake na wenyeviti wa bunge wanatekeleza mkakati huo; pamoja na hayo kaa kwa amani watanzania wameshaamka mbinu hiyo itawasaidia kwa muda tu halafu itasambalatika, kuna mbinu nyingi za kuleta mabadiliko ya kweli katika nchi yetu sio lazima kupitia bungeni!
Daima kumbuka: Haki huwa haitolewi kwenye sahani kama zawadi bali Haki hudaiwa na kupiganiwa; M4C oyee!