Ndugu yangu historia ni mwalimu mzuri sana; kama ukirudisha mkanda nyuma ukajiuliza ni kwa nini Anne Makinda ni spika wa bunge la Tanzania, alifikafika je katika nafasi hiyo na katika mazingira gani unapata jawabu lisilo na mashaka; agenda ilikuwa kumg'oa Mzee wa kasi na viwango Samuel Sitta ambaye CCM walikuwa wanamtuhumu kwa kukisaliti chama chake kwa sababu alikuwa anawapa wabunge wa upinzani nafasi sawa ya kuchangia hoja mbali mbali jambo ambalo lilisababisha madudu mengi ya serikali ya CCM kuibuliwa na kuwekwa hadharani; kashfa moja kubwa ilikuwa ile ya RICHMONDULI iliyomg'oa Edward Lowassa kutoka kwenye uwaziri mkuu, kwa hiyo ukaasisiwa mkakati wa kumg'oa Sitta akawekwa Makinda na matokeo yake ndio sindimba unayoiona bungeni sasa hivi, makinda, naibu wake na wenyeviti wa bunge wanatekeleza mkakati huo; pamoja na hayo kaa kwa amani watanzania wameshaamka mbinu hiyo itawasaidia kwa muda tu halafu itasambalatika, kuna mbinu nyingi za kuleta mabadiliko ya kweli katika nchi yetu sio lazima kupitia bungeni!
Daima kumbuka: Haki huwa haitolewi kwenye sahani kama zawadi bali Haki hudaiwa na kupiganiwa; M4C oyee!
Kwa kweli kanun zinakiukwa tu na Bunge linaendeshwa Kidikteta...INAWEZEKANA UMEWEKWA KWA MASLAH YA WACHACHE!
Kwani hukumbuki kuwa alifuatwa nyumbani kwake na akina Rostam na wenzake na wakaahidi kumpigia kifua apate uspika? Lengo lilikuwa kumuweka ili awalinde mafisadi kwani Sita alishindwa kufanya kazi hiyo. Haya ni matokeo yake hata kama mwanzoni alipohojiwa na vyombo vya habari kuwa amepandikizwa alikana lakini anachokifanya kinathibitisha yote.
Tatizo ni busara za kiti. Sijafanikiwa kuelewa hizi busara za kiti huwa ziko kwenye sehemu gani hasa ya hicho kiti. Sijui ni kwenye miguu ya kiti, au sehemu ya kuegemea au ya kukalia au kwenye makalio ya waliokikalia?
Ndugu yangu historia ni mwalimu mzuri sana; kama ukirudisha mkanda nyuma ukajiuliza ni kwa nini Anne Makinda ni spika wa bunge la Tanzania, alifikafika je katika nafasi hiyo na katika mazingira gani unapata jawabu lisilo na mashaka; agenda ilikuwa kumg'oa Mzee wa kasi na viwango Samuel Sitta ambaye CCM walikuwa wanamtuhumu kwa kukisaliti chama chake kwa sababu alikuwa anawapa wabunge wa upinzani nafasi sawa ya kuchangia hoja mbali mbali jambo ambalo lilisababisha madudu mengi ya serikali ya CCM kuibuliwa na kuwekwa hadharani; kashfa moja kubwa ilikuwa ile ya RICHMONDULI iliyomg'oa Edward Lowassa kutoka kwenye uwaziri mkuu, kwa hiyo ukaasisiwa mkakati wa kumg'oa Sitta akawekwa Makinda na matokeo yake ndio sindimba unayoiona bungeni sasa hivi, makinda, naibu wake na wenyeviti wa bunge wanatekeleza mkakati huo; pamoja na hayo kaa kwa amani watanzania wameshaamka mbinu hiyo itawasaidia kwa muda tu halafu itasambalatika, kuna mbinu nyingi za kuleta mabadiliko ya kweli katika nchi yetu sio lazima kupitia bungeni!
Daima kumbuka: Haki huwa haitolewi kwenye sahani kama zawadi bali Haki hudaiwa na kupiganiwa; M4C oyee!