Wanajamiiforums, baada ya matokeo ya uchaguzi wa jimbo la Arumeru Mashariki kutangazwa na mgombea wa CDM Joshua Nasari kuibuka mshindi, mimi nina mawazo yafuatayo:
- Wananchi sasa hivi wameanza kujua haki zao na kwamba wameanza kukataa kudanganywa na wanasiasa;
- Wanasiasa wanatakiwa kutimiza ahadi zao walizoahidi kwa wananchi baada ya kushinda uchaguzi;
- Wanasiasa wanatakiwa kuwa karibu sana na wananchi waliowachagua na siyo kukimbilia Kuishi Dar mara baada ya uchaguzi;
- CCM imeanza kupoteza mvuto kwa wananchi;
- CCM wakae chini na kutafakari kulikoni; etc