RAYAN THE DON
JF-Expert Member
- Aug 21, 2019
- 679
- 1,220
Habari ya asubuhi wanabodi?
Ni tumaini langu kwamba tuko salama na tunaendelea kupambana katika kulijenga taifa letu.
Ndugu wanabodi katika kuendelea na mapambano ya kulijenga taifa letu nawaomba sana msijisahau kujilinda na ugonjwa wa COVID-19. Tuendelee kuchukua tahadhali na kuwa waangalifu wa hali ya juu.
Wanabodi wa JF, kama kichwa cha uzi huu kisemavyo hapo juu ni kwamba CHADEMA ni chama cha ajabu sana kwani kimeshindwa kusimamia misingi ya demokrasia na haki asilia(Natural justice). Kwa mantiki hii CHADEMA mwaka huu imejichimbia kaburi bila kujijua.
Wanabodi, CHADEMA ni chama ambacho kinahubiri demokrasia na wakati mwingine huwa wanenda mbali zaidi na kumtuhumu mheshimiwa Rais wa JMT kwamba ni dikteta, hapendi ushauri n.k ila kwa kipindi hiki CHADEMA imedhihirisha ni jinsi gani walivyo wanafiki, wazandiki na madikteta kutokana na matendo ya mwenyekiti wao.
Wanabodi, CHADEMA kuwafukuza wabunge wake bila kuwapa haki ya kuwasikiliza wanatuonesha picha gani sisi wananchi wa kawaida?
Wanabodi, CHADEMA kutoa amri kwa wabunge wake wasiingie bungeni na kukataa kueleza lengo la hiyo amri na sababu za msingi za kufikia huo uamuzi wa kutokuingia bungeni na kutowashilikisha wabunge wake katika hilo jambo, je inaleta picha gani kwa wananchi wa kawaida na wanachama wake?
CHADEMA, kuwakata wabunge mishahara yao kwa ajili ya kuanzisha akaunti maalumu ambayo itawasaidia wabunge hao katika kampeni pale ambapo watakuwa wamekwama na kutumia hiy o hela kinyume na makubaliano ya wanufaika(wabunge wa CHADEMA) inaleta picha gani kwa jamii?
WanaCHADEMA ile demokrasia, utawala wa sheria na haki asilia ambayo mmekuwa mkihubiri bungeni, kwenye mitandao ya kijamii iko wapi katika chama chenu? Kwanini mnapenda kuwanyooshea wezenu vidole kwamba wao ni wachafu wakati nyie ndiyo wachafu wakuu, wazandiki na wanafiki wakubwa?
Kwa mantiki hiyo, mkipewa dhamana ya kuongoza nchi yetu mnataweza kweli? Kama mambo mmeshindwa kutekeleza katiba yenu pamoja na katiba ya JMT mtawezaje kuongoza nchi?
Mwaka 2005 nilitokea kuipenda sana CHADEMA kwani ilikuwa na watu wenye uwezo mkubwa sana katika mambo ya kisiasa. Waliposimama kutoa hotuba/hoja hakika ni watu ambao walionesha uwezo, ukomavu na weledi katika siasa. Ila kutokana na udikteta wa DJ umesababisha anguko kubwa sana la CHADEMA. Wale watu wote wameanza kuikimbia CHADEMA kwani inaongozwa na mtu ambaye siyo sahihi. Siku zote ni ngumu sana mtu mwenye akili ndogo kumuongoza mtu mwenye akili kubwa na ndiyo maana Dr. slaa, Zito Kabwe na wenzake waliondoka mapema CHADEMA kwani waliona mbali sana kama mnabii.
Mwisho, CHADEMA acheni unafiki wenu. Unafiki ni jambo baya sana katika Dunia hii. Kama mnafikiri wananchi hawaoni mnachofanya nawapa pole sana. Kwa sasa wananchi tupo makini sana. Sijui kwa mwaka huu matakuja na sera gani za kuwashawishi wanachi.
Ahsanteni na karibuni kwa michango.
Ni tumaini langu kwamba tuko salama na tunaendelea kupambana katika kulijenga taifa letu.
Ndugu wanabodi katika kuendelea na mapambano ya kulijenga taifa letu nawaomba sana msijisahau kujilinda na ugonjwa wa COVID-19. Tuendelee kuchukua tahadhali na kuwa waangalifu wa hali ya juu.
Wanabodi wa JF, kama kichwa cha uzi huu kisemavyo hapo juu ni kwamba CHADEMA ni chama cha ajabu sana kwani kimeshindwa kusimamia misingi ya demokrasia na haki asilia(Natural justice). Kwa mantiki hii CHADEMA mwaka huu imejichimbia kaburi bila kujijua.
Wanabodi, CHADEMA ni chama ambacho kinahubiri demokrasia na wakati mwingine huwa wanenda mbali zaidi na kumtuhumu mheshimiwa Rais wa JMT kwamba ni dikteta, hapendi ushauri n.k ila kwa kipindi hiki CHADEMA imedhihirisha ni jinsi gani walivyo wanafiki, wazandiki na madikteta kutokana na matendo ya mwenyekiti wao.
Wanabodi, CHADEMA kuwafukuza wabunge wake bila kuwapa haki ya kuwasikiliza wanatuonesha picha gani sisi wananchi wa kawaida?
Wanabodi, CHADEMA kutoa amri kwa wabunge wake wasiingie bungeni na kukataa kueleza lengo la hiyo amri na sababu za msingi za kufikia huo uamuzi wa kutokuingia bungeni na kutowashilikisha wabunge wake katika hilo jambo, je inaleta picha gani kwa wananchi wa kawaida na wanachama wake?
CHADEMA, kuwakata wabunge mishahara yao kwa ajili ya kuanzisha akaunti maalumu ambayo itawasaidia wabunge hao katika kampeni pale ambapo watakuwa wamekwama na kutumia hiy o hela kinyume na makubaliano ya wanufaika(wabunge wa CHADEMA) inaleta picha gani kwa jamii?
WanaCHADEMA ile demokrasia, utawala wa sheria na haki asilia ambayo mmekuwa mkihubiri bungeni, kwenye mitandao ya kijamii iko wapi katika chama chenu? Kwanini mnapenda kuwanyooshea wezenu vidole kwamba wao ni wachafu wakati nyie ndiyo wachafu wakuu, wazandiki na wanafiki wakubwa?
Kwa mantiki hiyo, mkipewa dhamana ya kuongoza nchi yetu mnataweza kweli? Kama mambo mmeshindwa kutekeleza katiba yenu pamoja na katiba ya JMT mtawezaje kuongoza nchi?
Mwaka 2005 nilitokea kuipenda sana CHADEMA kwani ilikuwa na watu wenye uwezo mkubwa sana katika mambo ya kisiasa. Waliposimama kutoa hotuba/hoja hakika ni watu ambao walionesha uwezo, ukomavu na weledi katika siasa. Ila kutokana na udikteta wa DJ umesababisha anguko kubwa sana la CHADEMA. Wale watu wote wameanza kuikimbia CHADEMA kwani inaongozwa na mtu ambaye siyo sahihi. Siku zote ni ngumu sana mtu mwenye akili ndogo kumuongoza mtu mwenye akili kubwa na ndiyo maana Dr. slaa, Zito Kabwe na wenzake waliondoka mapema CHADEMA kwani waliona mbali sana kama mnabii.
Mwisho, CHADEMA acheni unafiki wenu. Unafiki ni jambo baya sana katika Dunia hii. Kama mnafikiri wananchi hawaoni mnachofanya nawapa pole sana. Kwa sasa wananchi tupo makini sana. Sijui kwa mwaka huu matakuja na sera gani za kuwashawishi wanachi.
Ahsanteni na karibuni kwa michango.