G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 12,289
- 38,942
Chama Cha Mapinduzi (CCM ) kimeingia katika
historia ya kipekee Tanzania baada ya mara ya kwanza kwa chama hicho kikongwe kushindwa kumuweka hadharani mgombea wake wa urais kwenye uchaguzi mkuu hadi kufika mwezi may!
Aidha wale wasaka nia mbalimbali za ubunge na madiwani nao hawajaanza pilikapilika za aina yoyote ile! Kwa ufupi chama hicho kipo katika usingizi wa pono!
Katika historia ya Tanzania tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi mambo yamekuwa
kinyume na ya mshangao mkubwa! 'Wakati ambapo upinzani ukiimarika mara dufu na kupambana vilivyo, chama dola kimebaki katika usingizi mzito!
Ni nadra sana kwa vyama dola Africa (hata vile ambavyo vinajua fika kuwa vitashindwa kwenye uchaguzi) ifikapo kipindi cha kukaribia uchaguzi mkuu kukaa katika hali iliyonayo CCM! Kwa ufupi sijawahi kuona!
Hii ni dalili kuu ya kwanza ya Anguko kuu!
Dalili kuu ya pili na ya mwisho ni kusambaratika kwa chama hicho pale ambapo mgombea na wagombea watatangazwa! Hilo liko njiani kuja!
Kufuatia sintofahamu hii ya aina yake inayojitokeza, nimeamua ku-test validity ili kujua ukweli! Nimeamua kujiuliza maswali yafuatayo;
1)Kutokana na hali iliyonayo CCM (ya kutokuhangaika kabisa na ukizingatia hali halisi ya upinzani kwa sasa) PENGINE WANA UHAKIKA KUWA UCHAGUZI MKUU WA TANZANIA BADO SANA! KUNA MIAKA MIWILI MBELE (2017? )
2)Pengine kimepoteza matumaini kabisa ya kuendelea kushikia dola!
3)Pengine kina mbinu mpya na ya kipekee ambayo ipo kwenye makaratasi bado!
Kwa jinsi vyama dola vya Afrika vilivyo, ni vigumu sana kwa namna 2 na 3 kufanywa na vyama hivyo kirahisirahisi tu!
Trend hii inanifanya niamini kuwa namba 1ndiyo jibu sahihi kwa sasa! Si tunavijua vyama dola vya nchi masikini za kiafrika? Huwa vikiachia madaraka ni lazima pachimbike kwanza!
Ukijumlisha na jinsi mchakato wa uandikishwaji wapiga kura unavyoenda? Kwa hakika hapana kitu kilichojificha!
Tuendelee kukodolea macho hili sinema ila kwa kweli ni ndoto kuingia ulingoni oktoba!!!!!!!
historia ya kipekee Tanzania baada ya mara ya kwanza kwa chama hicho kikongwe kushindwa kumuweka hadharani mgombea wake wa urais kwenye uchaguzi mkuu hadi kufika mwezi may!
Aidha wale wasaka nia mbalimbali za ubunge na madiwani nao hawajaanza pilikapilika za aina yoyote ile! Kwa ufupi chama hicho kipo katika usingizi wa pono!
Katika historia ya Tanzania tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi mambo yamekuwa
kinyume na ya mshangao mkubwa! 'Wakati ambapo upinzani ukiimarika mara dufu na kupambana vilivyo, chama dola kimebaki katika usingizi mzito!
Ni nadra sana kwa vyama dola Africa (hata vile ambavyo vinajua fika kuwa vitashindwa kwenye uchaguzi) ifikapo kipindi cha kukaribia uchaguzi mkuu kukaa katika hali iliyonayo CCM! Kwa ufupi sijawahi kuona!
Hii ni dalili kuu ya kwanza ya Anguko kuu!
Dalili kuu ya pili na ya mwisho ni kusambaratika kwa chama hicho pale ambapo mgombea na wagombea watatangazwa! Hilo liko njiani kuja!
Kufuatia sintofahamu hii ya aina yake inayojitokeza, nimeamua ku-test validity ili kujua ukweli! Nimeamua kujiuliza maswali yafuatayo;
1)Kutokana na hali iliyonayo CCM (ya kutokuhangaika kabisa na ukizingatia hali halisi ya upinzani kwa sasa) PENGINE WANA UHAKIKA KUWA UCHAGUZI MKUU WA TANZANIA BADO SANA! KUNA MIAKA MIWILI MBELE (2017? )
2)Pengine kimepoteza matumaini kabisa ya kuendelea kushikia dola!
3)Pengine kina mbinu mpya na ya kipekee ambayo ipo kwenye makaratasi bado!
Kwa jinsi vyama dola vya Afrika vilivyo, ni vigumu sana kwa namna 2 na 3 kufanywa na vyama hivyo kirahisirahisi tu!
Trend hii inanifanya niamini kuwa namba 1ndiyo jibu sahihi kwa sasa! Si tunavijua vyama dola vya nchi masikini za kiafrika? Huwa vikiachia madaraka ni lazima pachimbike kwanza!
Ukijumlisha na jinsi mchakato wa uandikishwaji wapiga kura unavyoenda? Kwa hakika hapana kitu kilichojificha!
Tuendelee kukodolea macho hili sinema ila kwa kweli ni ndoto kuingia ulingoni oktoba!!!!!!!