Anguko kuu la CCM, dalili kuu ya kwanza!

Anguko kuu la CCM, dalili kuu ya kwanza!

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
12,289
Reaction score
38,942
Chama Cha Mapinduzi (CCM ) kimeingia katika
historia ya kipekee Tanzania baada ya mara ya kwanza kwa chama hicho kikongwe kushindwa kumuweka hadharani mgombea wake wa urais kwenye uchaguzi mkuu hadi kufika mwezi may!

Aidha wale wasaka nia mbalimbali za ubunge na madiwani nao hawajaanza pilikapilika za aina yoyote ile! Kwa ufupi chama hicho kipo katika usingizi wa pono!

Katika historia ya Tanzania tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi mambo yamekuwa
kinyume na ya mshangao mkubwa! 'Wakati ambapo upinzani ukiimarika mara dufu na kupambana vilivyo, chama dola kimebaki katika usingizi mzito!

Ni nadra sana kwa vyama dola Africa (hata vile ambavyo vinajua fika kuwa vitashindwa kwenye uchaguzi) ifikapo kipindi cha kukaribia uchaguzi mkuu kukaa katika hali iliyonayo CCM! Kwa ufupi sijawahi kuona!

Hii ni dalili kuu ya kwanza ya Anguko kuu!

Dalili kuu ya pili na ya mwisho ni kusambaratika kwa chama hicho pale ambapo mgombea na wagombea watatangazwa! Hilo liko njiani kuja!

Kufuatia sintofahamu hii ya aina yake inayojitokeza, nimeamua ku-test validity ili kujua ukweli! Nimeamua kujiuliza maswali yafuatayo;

1)Kutokana na hali iliyonayo CCM (ya kutokuhangaika kabisa na ukizingatia hali halisi ya upinzani kwa sasa) PENGINE WANA UHAKIKA KUWA UCHAGUZI MKUU WA TANZANIA BADO SANA! KUNA MIAKA MIWILI MBELE (2017? )

2)Pengine kimepoteza matumaini kabisa ya kuendelea kushikia dola!

3)Pengine kina mbinu mpya na ya kipekee ambayo ipo kwenye makaratasi bado!

Kwa jinsi vyama dola vya Afrika vilivyo, ni vigumu sana kwa namna 2 na 3 kufanywa na vyama hivyo kirahisirahisi tu!

Trend hii inanifanya niamini kuwa namba 1ndiyo jibu sahihi kwa sasa! Si tunavijua vyama dola vya nchi masikini za kiafrika? Huwa vikiachia madaraka ni lazima pachimbike kwanza!

Ukijumlisha na jinsi mchakato wa uandikishwaji wapiga kura unavyoenda? Kwa hakika hapana kitu kilichojificha!

Tuendelee kukodolea macho hili sinema ila kwa kweli ni ndoto kuingia ulingoni oktoba!!!!!!!
 
CCM Imeshajifia mkuu...Ukitaka kuona hilo...angalia mzee kinana anavyohangaika mikoani..hadi kutafuta fisi kwenye mikutano yake ili avute watu kwenda kumsikiliza
 
Chama Cha Mapinduzi (CCM ) kimeingia katika
historia ya kipekee Tanzania baada ya mara ya kwanza kwa chama hicho kikongwe kushindwa kumuweka hadharani mgombea wake wa urais kwenye uchaguzi mkuu hadi kufika mwezi may!

Aidha wale wasaka nia mbalimbali za ubunge na madiwani nao hawajaanza pilikapilika za aina yoyote ile! Kwa ufupi chama hicho kipo katika usingizi wa pono!

Katika historia ya Tanzania tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi mambo yamekuwa
kinyume na ya mshangao mkubwa! 'Wakati ambapo upinzani ukiimarika mara dufu na kupambana vilivyo, chama dola kimebaki katika usingizi mzito!

Ni nadra sana kwa vyama dola Africa (hata vile ambavyo vinajua fika kuwa vitashindwa kwenye uchaguzi) ifikapo kipindi cha kukaribia uchaguzi mkuu kukaa katika hali iliyonayo CCM! Kwa ufupi sijawahi kuona!

Hii ni dalili kuu ya kwanza ya Anguko kuu!

Dalili kuu ya pili na ya mwisho ni kusambaratika kwa chama hicho pale ambapo mgombea na wagombea watatangazwa! Hilo liko njiani kuja!

Kufuatia sintofahamu hii ya aina yake inayojitokeza, nimeamua ku-test validity ili kujua ukweli! Nimeamua kujiuliza maswali yafuatayo;

1)Kutokana na hali iliyonayo CCM (ya kutokuhangaika kabisa na ukizingatia hali halisi ya upinzani kwa sasa) PENGINE WANA UHAKIKA KUWA UCHAGUZI MKUU WA TANZANIA BADO SANA! KUNA MIAKA MIWILI MBELE (2017? )

2)Pengine kimepoteza matumaini kabisa ya kuendelea kushikia dola!

3)Pengine kina mbinu mpya na ya kipekee ambayo ipo kwenye makaratasi bado!

Kwa jinsi vyama dola vya Afrika vilivyo, ni vigumu sana kwa namna 2 na 3 kufanywa na vyama hivyo kirahisirahisi tu!

Trend hii inanifanya niamini kuwa namba 1ndiyo jibu sahihi kwa sasa! Si tunavijua vyama dola vya nchi masikini za kiafrika? Huwa vikiachia madaraka ni lazima pachimbike kwanza!

Ukijumlisha na jinsi mchakato wa uandikishwaji wapiga kura unavyoenda? Kwa hakika hapana kitu kilichojificha!

Tuendelee kukodolea macho hili sinema ila kwa kweli ni ndoto kuingia ulingoni oktoba!!!!!!!

Kwa hakika mkuu! Itazame nchi ya Marekani, Uchaguzi wao ni wa 2017, Vyama vikuu vyote vimeshaweka wagombea wao wazi. Na mimi nataka kuamini Inawezekana CCM wanategea kujua kua upinzani watammeka nani awe mgombea.Kama ni hivyo basi wamekwisha.
 
Chama Cha Mapinduzi (CCM ) kimeingia katika
historia ya kipekee Tanzania baada ya mara ya kwanza kwa chama hicho kikongwe kushindwa kumuweka hadharani mgombea wake wa urais kwenye uchaguzi mkuu hadi kufika mwezi may!

Aidha wale wasaka nia mbalimbali za ubunge na madiwani nao hawajaanza pilikapilika za aina yoyote ile! Kwa ufupi chama hicho kipo katika usingizi wa pono!

Katika historia ya Tanzania tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi mambo yamekuwa
kinyume na ya mshangao mkubwa! 'Wakati ambapo upinzani ukiimarika mara dufu na kupambana vilivyo, chama dola kimebaki katika usingizi mzito!

Ni nadra sana kwa vyama dola Africa (hata vile ambavyo vinajua fika kuwa vitashindwa kwenye uchaguzi) ifikapo kipindi cha kukaribia uchaguzi mkuu kukaa katika hali iliyonayo CCM! Kwa ufupi sijawahi kuona!

Hii ni dalili kuu ya kwanza ya Anguko kuu!

Dalili kuu ya pili na ya mwisho ni kusambaratika kwa chama hicho pale ambapo mgombea na wagombea watatangazwa! Hilo liko njiani kuja!

Kufuatia sintofahamu hii ya aina yake inayojitokeza, nimeamua ku-test validity ili kujua ukweli! Nimeamua kujiuliza maswali yafuatayo;

1)Kutokana na hali iliyonayo CCM (ya kutokuhangaika kabisa na ukizingatia hali halisi ya upinzani kwa sasa) PENGINE WANA UHAKIKA KUWA UCHAGUZI MKUU WA TANZANIA BADO SANA! KUNA MIAKA MIWILI MBELE (2017? )

2)Pengine kimepoteza matumaini kabisa ya kuendelea kushikia dola!

3)Pengine kina mbinu mpya na ya kipekee ambayo ipo kwenye makaratasi bado!

Kwa jinsi vyama dola vya Afrika vilivyo, ni vigumu sana kwa namna 2 na 3 kufanywa na vyama hivyo kirahisirahisi tu!

Trend hii inanifanya niamini kuwa namba 1ndiyo jibu sahihi kwa sasa! Si tunavijua vyama dola vya nchi masikini za kiafrika? Huwa vikiachia madaraka ni lazima pachimbike kwanza!

Ukijumlisha na jinsi mchakato wa uandikishwaji wapiga kura unavyoenda? Kwa hakika hapana kitu kilichojificha!

Tuendelee kukodolea macho hili sinema ila kwa kweli ni ndoto kuingia ulingoni oktoba!!!!!!!

mkuu! Waache waendelee kulala 2 usiwashtue hata kidogo, waache walale na wakiamka 2 waamkie upinzani. He he he he sipati picha bunge lijalo nitakapo mwona sita na pinda wakiomba mwöngozo wa spika na wasira naye akiunga mkono hoja kuwa seri ya chama cha democrasia hakiwasikilzi.
 
Na safari hii ni lazima ufanyike mdahalo wa wagombea ili kuepuka mabo ya kuuziwa mbuzi kwenye gunia. Na hata Mzee Mangula akileta story kama za Makamba kuzuia 'mchakato' majimboni ni wazi hali itakuwa ngumu zaidi maana uelewa wa wananchi wa kawaida umepanda kwa zaidi ya 150%!
 
Kwa hakika mkuu! Itazame nchi ya Marekani, Uchaguzi wao ni wa 2017, Vyama vikuu vyote vimeshaweka wagombea wao wazi. Na mimi nataka kuamini Inawezekana CCM wanategea kujua kua upinzani watammeka nani awe mgombea.Kama ni hivyo basi wamekwisha.
Mkuu ukiangalia ni dhahiri kuwa wapinzani wameshajipanga tayari na mgombea wao wanamjua ila wanafanya siri! CCM hawajafanya kikao chochote cha mchakato na hasa ikizingatiwa kuwa kuna miezi mitatu tu kabla mechi haijachezwa! Hawajafanya kikao chochote kile kuelezea mchakato wao.

Mimi nawaona 'wajinga' wale wanaodhani kuwa wapinzani kuonyesha wasiwasi wao juu ya uwepo wa uchaguzi mkuu mwaka huu wanakosea! Hivi chama dola kuwa na mazingira kama haya unategemea nini?
 
Na safari hii ni lazima ufanyike mdahalo wa wagombea ili kuepuka mabo ya kuuziwa mbuzi kwenye gunia. Na hata Mzee Mangula akileta story kama za Makamba kuzuia 'mchakato' majimboni ni wazi hali itakuwa ngumu zaidi maana uelewa wa wananchi wa kawaida umepanda kwa zaidi ya 150%!

Safari wagombea wa CCM hakuna kukimbia midahalo. Kuanzia udiwani jadi urais.
 
Hapa CCM wanatafuta namna ya kuchomoka. Wanatamani kura ya maoni ya katiba izibe uchaguzi mkuu, lakini sasa kura ya maoni haipo ki-katiba wakati katiba inaelekeza wazi kuwa uchaguzi mkuu ni October. Wanatamani kura ya maoni ivuruge utaratibuwa uchaguzi hasa kutumia kipindi cha mpito endapo kura ya maoni itakuwepo na katiba kupitishwa. Ni yamoto kumeza na tamu kutema!
 
Ccm wanaamini hakuna uchaguzi mwezi Oct.
 
Chama Cha Mapinduzi (CCM ) kimeingia katika
historia ya kipekee Tanzania baada ya mara ya kwanza kwa chama hicho kikongwe kushindwa kumuweka hadharani mgombea wake wa urais kwenye uchaguzi mkuu hadi kufika mwezi may!
Mkuu G Sam, kuchelewa ndio mpango mzima ili wakimpiga mtu chini, there will be no time to jump ships!.

Pasco
 
Anguko pekee la CCM ni endapo tu hawatampitisha Lowasa.
 
Anguko la ccm limeshakaribia hakuna mwenye uwezo wa kuzuia hilo anguko
 
Back
Top Bottom