Angola 2010: Africa Cup of Nations updates

Angola 2010: Africa Cup of Nations updates

  • salam ziwafikie wakuu, wadau wa sports hivi huyu coach wa Nigeria anamatatizo gani? unajua sijamuelewa kabisa alikua anamaanisha nini kumtoa obi na kumuingiza kanu, yani of all players anamwingiza huyu mzee wakati speed ya misri inaeleweka...?? haikuishia hapo kulikua na huyu yakub alikua hafanyi kitu pale mbele lakini cha ajabu wakina odemwinge na obafemi martins wakawa bench kwanzia mechi inaanza mpaka mwisho....



  • hivi alikua anawapima misri au?? yani ukiangalia ball possesion walikua wanaongoza nigeria lakini hamna goli, af yeye kakaa tu kama kawekewa gundi.....nimechukia sana kwakweli....


ile mechi ilikua 9ja washinde kabisa, namkubali yele obaso(aliefunga goli) dogo ni mkali, level zake ni za barca...lazima tumchukue yule bwa mdogo....anastamina ya hatari af yupo makini sana...
 
Nigeria ni mabishoo
hawajui kucheza jihadi......

Kombe la dunia watatia aibu sana.
 
Huyu golikipa Chinga kidogo achome nyumba moto. Anasommesault mpira anaucha nyuma duh!
 
100112183246_egypt_nigeria_386.jpg


Pharaohs baada ya kuwachabanga Super Eagles
ilibidi wabadilishane jezi.
 
najiskia vibaya kuona kwamba wawakilishi wetu world cup wamefuka mechi za kwanza
 
Si unaona vitu vyao lakini 2 - 2

Nimeviona mjukuu. Wanachofanya wakipata mpira ni kupiga mbele tu, ila kama inawapa magoli hakuna noma.Tabu ni kwamba pc yangu imepata kwikwi hizi dakika noma kweli.
 
najiskia vibaya kuona kwamba wawakilishi wetu world cup wamefuka mechi za kwanza

Hata siku moja usishabikie Nigeria. Wale ni sawa na Mafia (kama Chelsick teh teh teh) wakipata mpunga kwenye betting mambo kwishnei. Si unakumbuka hata ile World cup waliyocheza mara ya mwisho walikuwa na timu nzuri tu lakini hakuna walichofanya.

Timu za Africa kwenye world cup zenye heshima ni mbili tu Cameron na Algeria hao iko heka heka. Hata Pharaohs ni kazi bure tu onea buji.
 
kwa kweli hata mie imenishangaza sana kuona yule simba mzee anaingia wakati obafemi martins kakaa benchi, kanu basi watamuua bure jamani
 
najiskia vibaya kuona kwamba wawakilishi wetu world cup wamefuka mechi za kwanza

Usijisikie vibaya mashindano haya yatawafanya wajipange vizuri na pengine watatafuta walimu wazuri. Huyu kocha wa Nigeria kama Makisimo tu wakati wa mapumziko anaongea na mnwandishi anasema tatizo anaelewa kuwa ni defence, sasa kama alikuwa anafahamu hilo kwa nini hakulirekebisha. Shwain kabisa huyu.
 
Nigeria wameshajichokea wachezaji wao wengi wanadhani watarudia kile walichofanya kwenye World Cup 94.
 
kwa kweli hata mie imenishangaza sana kuona yule simba mzee anaingia wakati obafemi martins kakaa benchi, kanu basi watamuua bure jamani

Strength ya Kanu ni ku'hold' mpira na kwa hali hiyo kuruhusu wenzake wajipange vizuri. Obafemi ni mzuri (ni papara vilevile), lakini scoring rate yake ni chini mno (chini ya 1 goal per 1000 minutes) ukulinganisha na Yakubu. Makocha huwa wanaangalia statistics kama hizi.
 
1769633707.jpg



Adou Mouftaou wa Benin na Pelembe Elias wa Musumbiji wakioneshana utemi
progress.gif
 
Back
Top Bottom