Angela Mke Wangu, yote ulitaka wewe

Angela Mke Wangu, yote ulitaka wewe

Aiseee naona Mentor unaendelea kuwinda akanana.
Hahahaha
angela wivu gb 20
Mentor na lara 1 mnanifanya nizidi kulipenda jukwaa.
 
Last edited by a moderator:
majirani nao

Angela acha kulia,wajiumiza we na familia
Mumeo kajitakia,shimoni kudumbukia
sheitwani alimuachia,moyowe kujitwalia
Mwache atange na njia,machweo atakurejea


Ni mengi umepitia,jiranizo twashuhudia
Si wa kwanza nakuambia,hutokua wa mwisho pia
Jifunze adabu kumtia,pindi mambo yakimchachia
Mwache atange na njia,Machweo atakurejea

Si unamfahamu judi,bintie mzee daudi
mumewe alitia juhudi,kuidhulumu nafsi ya judi
kuchukua hatua ilibidi,kulinda yake shadidi
Mwache atange na njia,machweo atakurejea

Jifanye kama hujali,huhangaishwi na zake pilika
Anza kusaka mali,tunza mwili kwa uhakika
fikiri ya watoto hali,mwanamke chakarika
Mwache atange na njia,machweo atakurejea
 
Umenikumbusha kwenye mitihani ya Kiswahili kutunga ushairi ilikua balaa basi ntafikiriaa mistari ya diamondi nikiona haielekei nahamia ya stamina nikiona namna gani nachukua mistari ya bibi kidude
Nilikua nanunaje!!??maana kutunga mashairi kipaji afadhali hata utenzi
mmmmmh!! Embu nisalimie kwanza......wenzako tulitungia mashairi nyimbo za Mbaraka Mwinshehe
 
Baba Eddy nitarudi, vidonge kuwapasheni...

Cc: Angela mke wangu lara 1, na mama wa jirani mwallu.
 
Last edited by a moderator:
mwallu hakika yote nimekusikia, Na pia ukweli nimeshawishika
Lakini bibie mie nakuapia, Hapa nilipo si pakujishika
Sheitwan mume huyu keshamuingia, Katu siwezi hata salimika
Nafsi yangu nyongo ishatumbkia, Navumilia tu wanangu kuwaweka
Ndoa yangu imgeuka ndoano shosti!
 
Last edited by a moderator:
mwallu hakika yote nimekusikia, Na pia ukweli nimeshawishika
Lakini bibie mie nakuapia, Hapa nilipo si pakujishika
Sheitwan mume huyu keshamuingia, Katu siwezi hata salimika
Nafsi yangu nyongo ishatumbkia, Navumilia tu wanangu kuwaweka
Ndoa yangu imgeuka ndoano shosti!
 
Last edited by a moderator:
Mpita njia
Mama itulize nafsi, bure usijewehuka, kaamua jinafasi, hajui anatabika,
Upunguze wasiwasi, ishi nae kama kaka,
Huu ushauri bure, mapenzi si mashindano.

Waite wakubwa wenu, bayana uwaeleze,
Ndoa si hii ya kwenu, akutenda waeleze,
watamani rudi kwenu, usisite waeleze,
Huu ushauri bure, mapenzi si mashindano.

Bado wampenda sana, tatizo mbele huoni,
Umeshamuonya sana, mabadiliko huoni,
Na utashukuru sana, kibadilika mwandani,
Huu ushauri bure, mapenzi si mashindano
 
Angela nimekuja kukujibu Mentor Mume wangu!

Waungwana mwenzenu nipeni pole, Mwenzeu sipendwi kama upele
Wenzngu wamepata waume wapole, Mie nabakia napiga kelele
Mwanaume niajua ni mwenda pole, kumbe ndo mla nyama mwenda pole
Tarajio langu la ndo limepotea kizani

Mwanaume mvuvi halisi, Wala huvui vingisi
Si kazi Huotea mifulusi, Majabi huya jalisi
Haogopi kaskazi wala kusi, Kutwa kuntia mie nuksi
Trajio langu la ndoa limepota kizani

Niliamua niolewe na anenifaa, Mume mwenye kusfiwa
Niolewe mie ndoani nipate kuzaa, Kama vile nilivozaliwa
Mengi niliahidiwa mume kunituzaa, Zote ahadi hewa
Trajio langu la ndoa limepota kizani

Nikavishwa johoza kifahari, Nikajua ndoa ni ya kheri
Mama yangu aliona fahari, Bintie kumlete uzeeni kheri
Nikajua nitaiepuka mibuzi shari, Nimtendee mume kila lakheri
Trajio langu la ndoa limepota kizani

Mume wewe si mume tena, Bali gume gume aliokataza Mtume
Mume wanifoke mbele ya wana, Huna hata mswalie mtume
Kila siku wewe kunitukana, Hjui maana ya mume
Trajio langu la ndoa limepota kizani

Wenzangu wapigwa na khanga, Mie najikaza nibaki kulea wana
Dharau zako kali kama upanga, Najitahidi hapa kwako kujibana
Nikiondoka nita tanga tanga, Pia nitawatesa wangu wana.
Trajio langu la ndoa limepota kizani

Hali ngumu kulalama, ilihali washinda bar na kina salma
Watoto kutwa walalama, Mie nawambia wazi upo kwa Salma
Sijui kwanini hukumuoa Salma, Labda tu hamkukutana mapema
Trajio langu la ndoa limepota kizani

Machahce nimeyasema uwazi ila mengi yako siyaweki wazi
Wadada kuolewa wala si kazi, Mda mwengine ni uduwanzi
Vimada wako ktwa wako zanzi, Mie ndani nakuna nazi
Trajio langu la ndoa limepota kizani

Huyu msichana yuko very smart, very smart indeed!
 
Angela mekusikia, kilio menifikia
Japo kijaniingia, huruma watafutia
Majirani meniitia, wambea wapita njia
Angela Mke Wangu, yote ulitaka wewe!

Hawaujui ukweli, wa yetu ndani nyumbani
Nje wajifanya asali, ndani kwetu ni vitani
Maneno tu mie silali, lalamikacho sikioni
Angela Mke Wangu, yote ulitaka wewe!

Muulize na Aneti, dada wetu wa nyumbani
Hadi kushushia neti, ulimwita kitandani
Kisa upo kwenye net, bize kutwa jukwaani
Angela Mke Wangu, yote ulitaka wewe!

Ndoa hii meichoka, nyumba ndogo sitoacha
Unaniona mi kaka, n'kikugusa w'sema "Acha"
Kuvuja kwake pakacha, mchukuzi hatoacha
Angela Mke Wangu, yote ulitaka wewe!

Ukweli nakuambia, hata uite ukoo
Ndiyo nitaitikia, kesho nipo kwa Ufoo
Usipo badilikia, Eddy ndo aniweka kwako
Angela Mke Wangu, yote ulitaka wewe!

Maneno ya majirani, endelea kusikiza
Waeleze mtaani, mbeleni watakuliza
Beti zo watazighani, wanifata kuki-giza
Angela Mke Wangu, yote ulitaka wewe!
 
Angela mekusikia, kilio menifikia
Japo kijaniingia, huruma watafutia
Majirani meniitia, wambea wapita njia
Angela Mke Wangu, yote ulitaka wewe!

Hawaujui ukweli, wa yetu ndani nyumbani
Nje wajifanya asali, ndani kwetu ni vitani
Maneno tu mie silali, lalamikacho sikioni
Angela Mke Wangu, yote ulitaka wewe!

Muulize na Aneti, dada wetu wa nyumbani
Hadi kushushia neti, ulimwita kitandani
Kisa upo kwenye net, bize kutwa jukwaani
Angela Mke Wangu, yote ulitaka wewe!

Ndoa hii meichoka, nyumba ndogo sitoacha
Unaniona mi kaka, n’kikugusa w'sema “Acha”
Kuvuja kwake pakacha, mchukuzi hatoacha
Angela Mke Wangu, yote ulitaka wewe!

Ukweli nakuambia, hata uite ukoo
Ndiyo nitaitikia, kesho nipo kwa Ufoo
Usipo badilikia, Eddy ndo aniweka kwako
Angela Mke Wangu, yote ulitaka wewe!

Maneno ya majirani, endelea kusikiza
Waeleze mtaani, mbeleni watakuliza
Beti zo watazighani, wanifata kuki-giza
Angela Mke Wangu, yote ulitaka wewe!

Mwache aendelee kukuna nazi wacha tujinywee zanzi huku tukimhudumia abdala bichwa wazi
 
mpita njia

mapenzi ni ya wawili, kidume umechemka,
usiwe kama tumbili, matatizo kuyaruka,
ongea na wako mwali, dawa yake si kutoka,
huu ushauri bure, mapenzi si mashindano.

kichwa dogo wa tumia, nje unaenda kuruka,
kinga usipotumia, mapema utakauka,
mwishoni utajutia, matatizo yashafika,
huu ushauri bure, mapenzi si mashindano.

eddy tabaki mkiwa, ubabe kiendekeza,
kamwe hutofanikiwa, kwa ubabe nadokeza,
mengi umeshaambiwa, mebaki kutekeleza,
huu ushauri bure, mapenzi si mashindano.

heri kelele hekima, kuliko liwazo ovu,
na bora ukayapima, usisubirie makovu,
nyumba ndogo sio dawa, kidogo kuwa mwelevu,
huu ushauri bure, mapenzi si mashindano.
 
hahaha ni baba Vivi ama baba Eddy. kiroho safi leo nimepata kitu kikubwa hapa.
 
Da mmenikumbusha mashairi ya Charles Mloka na Andanenga.Safi sana baba Eddy
 
Back
Top Bottom