Nashukuru kwa ufafanuzi wako mzuri wenye kujenga, na kuelimisha maana kweli wengi wetu tunatafuta kazi na pengine tunakosa kazi kwasababu hatutoi taarifa zetu za kutosha ama tunaomba kazi kwakuorodhesha changamoto za maisha zinazotukabili.
Hakika soko la ajira nchini inachangamoto kubwa sana ikiwa na wahitimu wengi kutoka vyuo vikuu nchini na vyuo vingine vidogo vidogo, hivyo sisi kama Watanzania wenye nia njema na wenzetu na nchi yetu kwa ujumla, tusaidiane kwa hili hasa kwa hali na mali, ili kuweza kuendeleza uchumi wetu na ustawi wa nchi yetu kwa ujumla.
Chonde chonde kwa wote watakao fanikiwa kuona meseji hii kila mmoja kwa nafasi yake, awaze kutoa mchango wake kwa hili, kwani nchi ikiendelea mafanikio ni kwa wote sio kwa wachache.
Mungu awabariki wote:angry: