Gushleviv
JF-Expert Member
- Mar 14, 2011
- 3,457
- 5,324
Wadau wa jukwaa hili leo naweza kukiri mbele yenu kuwa nimekuwa nikihamahama katika matumizi ya simu kutokana na kufifia kwa Simu za Blackberry katika soko la simu hivyo nikawa sina uhakika na usalama wa simu yoyote zaidi ya Blackberry licha ya kwamba kuna Iphone na Windows Phone ambayo kwa mtazamo wangu ni simu ambayo naona inanifunga jela(Kuninyima uhuru wa kufanya yale ninayotaka katika simu). Hivyo ujio wa Blackberry katika Android na Usalama walionihakikishia imenifanya nijione kuingia Android milele! Hivyo labda kunaweza kuwepo yeyote mwenye taarifa zaidi za kiusalama katika toleo jipya la simu za Blackberry zinazotumia Android OS basi aje hapa kufafanua zaidi.
Long Live Blackberry!
Long Live Blackberry!