belie
JF-Expert Member
- Sep 19, 2014
- 387
- 261
Habari zenu jamani, wakubwa shikamoo.
Natumai wote mko fine, ngoja niwape kisa hiki mwenzenu maana nina bahati mbaya kweli na wanaume.
Kuna kaka mmoja tulisoma nae o-level, akaanza kunitongoza kuanzia form 2 akidai ananipenda sana, mimi nilimkatalia kwa sababu kwa kipindi kile sikutaka kujihusisha na mambo ya mapenzi akawa anaendelea kila kukicha haishi vituko. Akawa ananitoa breakfast na kuniletea zawadi kila siku, mara ya kwanza nikawa nakataa, nikikataa wakati wa kurudi home navikuta kwenye begi langu, na nikifungua daftari usiku kusoma nakuta barua na hela nikawa nimemzoea hivyo.
Basi bwana, nikawa kila siku napewa zawadi za nguvu kama viatu, nguo, peni za maana zile na kuna siku aliniletea pure gold chain. Nikawa nitake nini mie nikose, lakini kumbuka nilimkatalia (sasa sijui alikuwa anajua nikimaliza shule nitamkubalia? sijui) basi ikafika mwisho wa mwaka tukafunga shule na kurudi nyumbani, siku hyo aliniletea box kubwa lenye mazaga zaga kibao ikiwemo simu (siemens kipindi hicho) akanambia tutakuwa tukiwasiliana.
Muda ukapita tutakutana tena mwaka mwingine, mambo yakawa yale yale, lakini safari hii naona wivu ulimjaa sana, kwa sababu alikua hataki niongee wala kukaa na mwanaume yoyote yule akiniona nae anamfata yule mwanaume anampiga, mambo yakawa mabaya zaidi kwani ilifika mpaka kwa headmaster wetu wakaniuliza nini chanzo wananitaja mimi.
Baba yangu akawa anaitwa shule kila siku kusikiliza kesi za kijinga, nikawa nachukia sana coz sipendi nishushe heshima yangu hasa kwa mambo ya kipuuzi.
Siku hiyo nikamrudishia vitu vyaake vyote kasoro hela coz nilikua nishazitumia, akakataa kuvichukua nikavitupa chini nikaondoka, kurudi nyumbani nikavikuta alikua amempa dada wetu wa kazi na kudai nilivisahau shule, nikavichoma moto vilivyochomeka na vingne nikaviweka ndani ili ikitokea siku anavihitaji nimpe.
Nikamwambia sitaki mazoea na wewe na usinisumbue kumbe ndo nilikua nazidi kuharibu, nikawa namkwepa shule, nikija home namkuta nje ya geti ananisubiri, yaani alikua king'ang'anizi sijapata kuona.
Nikawa namkwepa hivyo hivyo, tukafika form 4, nakumbuka nilifanya vizuri kwenye mtihani wa mock hivyo kaka yangu aliyeko nje, akaninunulia simu, nilifurahi sana, sasa yeye alivyoniona nayo akajua nimepewa na bwana yangu sijui, kuna siku tulikua tunafanya mtihani mabegi tunaacha kwenye chumba kimoja hivi, yeye alikua wa mwisho kuingia hivyo alivyoenda kuweka begi lake akatafuta begi langu lilipo na kuichukua simu yangu, ikumbukwe vile vitu vyake vingine ikiwemo simu nilibahatika kumrudishia.
Basi bwana, natoka kwenye mtihani sioni simu yangu yaani nilipata shock ya ajabu nikaanza kulia, na kwenda kuwaelezea walimu ofisini, baadae akaja rafiki yake mmoja akaniambia huyo mkaka anataka kuongea na mimi kwenye simu yake, nikapokea na kuongea nae.
Akaniambia naomba tuonane posta sehemu moja hivi ya fast food, nikamjibu sitaki, akanambia kama unaitaka simu yako njoo kama huitaki basi usije, nikawa sina jinsi nikaenda, nilivyofika akaanza kuexpress feeling zake pale nikamwambia mimi nataka simu yangu, usinieleze upuuzi, akasema sikupi simu yako mpaka unikubali mimi nikawa nabishana nae.
Mara akaingia mfukoni akatoa sumu ya panya na kuiweka kwenye kile chakula kilichobaki na kula, mimi nikawa namuangalia 2, akanambia bora afe tu coz simpendi, mara akameza akataka kumeza, nikamwambia basi nimekubali akatema pale yakaisha, nikamwambia sasa simu yangu vipi akatoa simu nyingine nzuri zaidi ya ile akanipa akanambia tumia hii, ile achana nayo, nikamwambia mimi sitaki simu nzuri wala mbaya nachotaka simu yangu, tukagombana pale hakunipa nikaondoka kwa hasira na hakunipa tena simu yangu ikabidi nyumbani nidanganye nimepoteza.
Ngoja nifupishe stori kidogo, ugomvi ukawa mkubwa hadi tukapigana na wakati tunapigana nilikua nimeshika peni mkononi nikamkwaruza nayo usoni, akatoka damu nyingi na likawa jeraha kubwa.
Tukamaliza tukapotezana coz nilienda kusoma boarding so hakuniona tena, sasa lengo la haya yote niliyohadithia hapa ni kwamba juzi kati sijui alipata wapi no yangu na kunipigia, akaniambia bado ananipenda, na akaniambia anakataliwa na wanawake kwa sababu ya kovu usoni nililomsababishia, hivyo lazima nimkubali la sivyo na mimi ataniweka zaidi ya hilo au kuniua kabisa.
Nimelifikiria sana hili, nikaamua nililete kwenu jamani, embu nishauri nifanye nini, maana kuna watu ambao ni familia yake nimeongea nao wameniambia alishauguaguaga ugonjwa wa akili, na alishaiba kwao na kutaka kuchoma moto nyumba yao, na baba yake akampeleka jela apate adabu.
Sasa jamani nafanyaje hapa?
Ushauri please
Natumai wote mko fine, ngoja niwape kisa hiki mwenzenu maana nina bahati mbaya kweli na wanaume.
Kuna kaka mmoja tulisoma nae o-level, akaanza kunitongoza kuanzia form 2 akidai ananipenda sana, mimi nilimkatalia kwa sababu kwa kipindi kile sikutaka kujihusisha na mambo ya mapenzi akawa anaendelea kila kukicha haishi vituko. Akawa ananitoa breakfast na kuniletea zawadi kila siku, mara ya kwanza nikawa nakataa, nikikataa wakati wa kurudi home navikuta kwenye begi langu, na nikifungua daftari usiku kusoma nakuta barua na hela nikawa nimemzoea hivyo.
Basi bwana, nikawa kila siku napewa zawadi za nguvu kama viatu, nguo, peni za maana zile na kuna siku aliniletea pure gold chain. Nikawa nitake nini mie nikose, lakini kumbuka nilimkatalia (sasa sijui alikuwa anajua nikimaliza shule nitamkubalia? sijui) basi ikafika mwisho wa mwaka tukafunga shule na kurudi nyumbani, siku hyo aliniletea box kubwa lenye mazaga zaga kibao ikiwemo simu (siemens kipindi hicho) akanambia tutakuwa tukiwasiliana.
Muda ukapita tutakutana tena mwaka mwingine, mambo yakawa yale yale, lakini safari hii naona wivu ulimjaa sana, kwa sababu alikua hataki niongee wala kukaa na mwanaume yoyote yule akiniona nae anamfata yule mwanaume anampiga, mambo yakawa mabaya zaidi kwani ilifika mpaka kwa headmaster wetu wakaniuliza nini chanzo wananitaja mimi.
Baba yangu akawa anaitwa shule kila siku kusikiliza kesi za kijinga, nikawa nachukia sana coz sipendi nishushe heshima yangu hasa kwa mambo ya kipuuzi.
Siku hiyo nikamrudishia vitu vyaake vyote kasoro hela coz nilikua nishazitumia, akakataa kuvichukua nikavitupa chini nikaondoka, kurudi nyumbani nikavikuta alikua amempa dada wetu wa kazi na kudai nilivisahau shule, nikavichoma moto vilivyochomeka na vingne nikaviweka ndani ili ikitokea siku anavihitaji nimpe.
Nikamwambia sitaki mazoea na wewe na usinisumbue kumbe ndo nilikua nazidi kuharibu, nikawa namkwepa shule, nikija home namkuta nje ya geti ananisubiri, yaani alikua king'ang'anizi sijapata kuona.
Nikawa namkwepa hivyo hivyo, tukafika form 4, nakumbuka nilifanya vizuri kwenye mtihani wa mock hivyo kaka yangu aliyeko nje, akaninunulia simu, nilifurahi sana, sasa yeye alivyoniona nayo akajua nimepewa na bwana yangu sijui, kuna siku tulikua tunafanya mtihani mabegi tunaacha kwenye chumba kimoja hivi, yeye alikua wa mwisho kuingia hivyo alivyoenda kuweka begi lake akatafuta begi langu lilipo na kuichukua simu yangu, ikumbukwe vile vitu vyake vingine ikiwemo simu nilibahatika kumrudishia.
Basi bwana, natoka kwenye mtihani sioni simu yangu yaani nilipata shock ya ajabu nikaanza kulia, na kwenda kuwaelezea walimu ofisini, baadae akaja rafiki yake mmoja akaniambia huyo mkaka anataka kuongea na mimi kwenye simu yake, nikapokea na kuongea nae.
Akaniambia naomba tuonane posta sehemu moja hivi ya fast food, nikamjibu sitaki, akanambia kama unaitaka simu yako njoo kama huitaki basi usije, nikawa sina jinsi nikaenda, nilivyofika akaanza kuexpress feeling zake pale nikamwambia mimi nataka simu yangu, usinieleze upuuzi, akasema sikupi simu yako mpaka unikubali mimi nikawa nabishana nae.
Mara akaingia mfukoni akatoa sumu ya panya na kuiweka kwenye kile chakula kilichobaki na kula, mimi nikawa namuangalia 2, akanambia bora afe tu coz simpendi, mara akameza akataka kumeza, nikamwambia basi nimekubali akatema pale yakaisha, nikamwambia sasa simu yangu vipi akatoa simu nyingine nzuri zaidi ya ile akanipa akanambia tumia hii, ile achana nayo, nikamwambia mimi sitaki simu nzuri wala mbaya nachotaka simu yangu, tukagombana pale hakunipa nikaondoka kwa hasira na hakunipa tena simu yangu ikabidi nyumbani nidanganye nimepoteza.
Ngoja nifupishe stori kidogo, ugomvi ukawa mkubwa hadi tukapigana na wakati tunapigana nilikua nimeshika peni mkononi nikamkwaruza nayo usoni, akatoka damu nyingi na likawa jeraha kubwa.
Tukamaliza tukapotezana coz nilienda kusoma boarding so hakuniona tena, sasa lengo la haya yote niliyohadithia hapa ni kwamba juzi kati sijui alipata wapi no yangu na kunipigia, akaniambia bado ananipenda, na akaniambia anakataliwa na wanawake kwa sababu ya kovu usoni nililomsababishia, hivyo lazima nimkubali la sivyo na mimi ataniweka zaidi ya hilo au kuniua kabisa.
Nimelifikiria sana hili, nikaamua nililete kwenu jamani, embu nishauri nifanye nini, maana kuna watu ambao ni familia yake nimeongea nao wameniambia alishauguaguaga ugonjwa wa akili, na alishaiba kwao na kutaka kuchoma moto nyumba yao, na baba yake akampeleka jela apate adabu.
Sasa jamani nafanyaje hapa?
Ushauri please