cutelove
JF-Expert Member
- Oct 3, 2017
- 3,317
- 7,509
Kuna vibwanga duniania aisee, unaweza ukawaza mpaka usipate jibu
Huyu mdada akiwa na umri wa miaka 20 aliwahi kutongozwa na mwanaume mwenye umri wa miaka 38 hivi,lakini huyu dada alimkataa kwa kumpa sababu kuu mbili
1. Sababu ya Kwanza unanizidi umri mbali sana, yaani inapaswa wewe uwe mzazi wangu
2. Una familia yako na mke wako, siwezi kuingilia familia yako
Basi mwanaume akawa ameridhika na majibu ingawa awali binti alikuwa anapokea vizawadi na hela ya matumizi kabla hajampa jibu la hivyo
Binti akawa ameingia kwenye mahusiano na mwanaume mwingine miaka 25 hivi mpaka wakaoana wakaenda kuishi mkoa mwingine. Baada ya miaka miwili binti karudi ana mtoto na maisha yamempiga hatari,hadi muda mwingine anawaza ajiuze ili mwanae ale na avae maana baba yake alisha toweka akaingia mikoani huko
Sasa binti amekuwa anatumia njia za kuomba watu wamwambie huyu mwanaume mwenye familia yake yule ya mwanzoni wawe kwenye mahusiano. Mbaba anamwambia siwezi kuwa na wewe maana umewahi kunikataa na sababu nzito
Binti anadai alikuwa hana akili kipindi hicho, hata hivyo mbaba amemkataa ila cha ajabu binti anawambia watu mtaani kuwa anatembea naye. Cha ajabu zaidi anawasiliana na mganga mmoja wa kienyeji ili ampe dawa amnase mbaba wa watu na kuwauliza wanawake wengine wampe dawa au njia ya kumnasa huyo mbaba awe chini yake
Mbaba anafanya juu chini mambo hayo yaishie mitaani yasije yakamfikia mke wake yakaleta mtafaruku kwenye familia yake
Yaani mambo yanaenda kwa kasi kwenye hii dunia. Na nyie wanaume mkome kutongoza ovyo
Huyu mdada akiwa na umri wa miaka 20 aliwahi kutongozwa na mwanaume mwenye umri wa miaka 38 hivi,lakini huyu dada alimkataa kwa kumpa sababu kuu mbili
1. Sababu ya Kwanza unanizidi umri mbali sana, yaani inapaswa wewe uwe mzazi wangu
2. Una familia yako na mke wako, siwezi kuingilia familia yako
Basi mwanaume akawa ameridhika na majibu ingawa awali binti alikuwa anapokea vizawadi na hela ya matumizi kabla hajampa jibu la hivyo
Binti akawa ameingia kwenye mahusiano na mwanaume mwingine miaka 25 hivi mpaka wakaoana wakaenda kuishi mkoa mwingine. Baada ya miaka miwili binti karudi ana mtoto na maisha yamempiga hatari,hadi muda mwingine anawaza ajiuze ili mwanae ale na avae maana baba yake alisha toweka akaingia mikoani huko
Sasa binti amekuwa anatumia njia za kuomba watu wamwambie huyu mwanaume mwenye familia yake yule ya mwanzoni wawe kwenye mahusiano. Mbaba anamwambia siwezi kuwa na wewe maana umewahi kunikataa na sababu nzito
Binti anadai alikuwa hana akili kipindi hicho, hata hivyo mbaba amemkataa ila cha ajabu binti anawambia watu mtaani kuwa anatembea naye. Cha ajabu zaidi anawasiliana na mganga mmoja wa kienyeji ili ampe dawa amnase mbaba wa watu na kuwauliza wanawake wengine wampe dawa au njia ya kumnasa huyo mbaba awe chini yake
Mbaba anafanya juu chini mambo hayo yaishie mitaani yasije yakamfikia mke wake yakaleta mtafaruku kwenye familia yake
Yaani mambo yanaenda kwa kasi kwenye hii dunia. Na nyie wanaume mkome kutongoza ovyo