View attachment 325562 View attachment 325563
Ni kama sinema lakini ndio ukweli wenyewe!!Mambo ya Wakinga na "kinga" zao
Huyu ni mwizi aliyenaswa na "sumaku ya asili" darini.
Hiyo miguu kwenye TV imenasa. Wamevuta Askari wanne haiajaachia.Wakamvutia kwa juu ya bati alikoingilia, akalalamika anadai msinivute kwa juu mnivutie kwa ndani(Yaani kuelekea chini )kwa juu mnavyonivuta kuna kitu dukani nacho kinanivuta nitafia hapa hapa jamani(huku akilia).
Baada ya polisi kushindwa kumchomoa wakamuomba mwenye duka tunaomba ukamtoe,maana kila Polisi wakimvuta na "sumaku ya asili" inavuta,ndo akavutwa na mwenye duka, akafanikiwa kutoka na kuchukuliwa na Polisi
Yaani ile "Law of gravitation" leo ime-fail,miguu ilinasa kwenye TV na mikono darini na huku akining'inia kama panga-boy.
Jamani Wakinga wa Kariakoo,hii Sayansi kwanini msimgawie na Magufuli ili wale wabishi wa kukwapua mali za umma nao wagande??