Ananipenda au ananijaribu?

Ananipenda au ananijaribu?

jojoe35

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2014
Posts
262
Reaction score
379
Nilitokea kumpenda binti flani chuoni, kila tulipoonana alionyesha dalili za kuwa interested na mimi.Sikusita kumweleza hisia zangu, bahati nzuri alikua keshanielewa hata kabla yakumwambia akasema "usijal nmeshakuelewa hitaji lako.

Naomba unipe mda coz nimetoka kubreak-up na mtu wangu mwezi ulopita" nikasema isiwe shida takusubiria mama.Muda wote huo wakumsubiria alipenda kuwa karibu na mimi muda wote nikiwa mbali anakuwa mpweke sana, so nilijitahidi kuwa karibu nae.

Kuna siku nilimkumbusha ''lini utakuwa wangu?" Nilimuuliza, akajibu akajibu naomba hili swala tuliweke katika maombi, kila mmoja aombe Mungu kumdhihirishia kama nikweli tunafanana, nikasema poa.

Sikumoja Jumamosi mchana nimepumzka chumbani, nikashtukia anagonga hodi, nikamkarbisha ndani, tulipiga story sana, siku hiyo hadi, nikamuomba kumkiss ata once.

Mtoto alikataa kata nikapotezea, kushitukia kanirukia nakuanza kunila denda sikucta nikampa sapot.Badae tukaachana akarud hostel kwake, ni kawaida yake kunishtukiza maana ata zaman nilipokuwa nataka kumchum shavuni anakataa but nikipotezea nashangaa ananirukia nakunichum, hasa nashindwa kumuelewa.

Tangu siku ile Jumamosi tulipo dendeka alibadirika ghafla, alinipigia simu nakuniambia alikosea kufanya hivo na hataki ukaribu wa hivo tena, tuwe marafiki wa kawaida.

Anapenda kusalimiana sana na wanaume kila anapokua, yaani nikitembea naye hadi nilikuwa nakereka.Sasa wakuu nimeshindwa kumuelewa, ni kwamba hanitaki au bado ananipenda?

Na kwanini ana act strange hivo?

Msaada wakuu
 
Chuo upo ngazi gani brother, cheti, stashahada, shahada, stashahada/shahada ya uzamili??
 
We bwana mdogo unaonesha ni mdhaifu but kwa uzoefu wangu wa wanawake wa aina hiyo..kuna mambo ya msingi lazima uelewe..

Kwanza je huyo demu alishawah kusex na mtu aliye break nae!? Kama kashawahi bhas elewa anakufanyia maigizo tuu mwambie wewe hutaki urafiki nae.. unataka awe dem waako na si vinginevyo..
Pia usiogope yeye kuwa na marafik wengi ila wewe ndio unatakiwa umfanye apunguze hao marafik..kwa kuwa nae bize, kumkeep bize chatting n.k..
Jiamini bwana mdogo jipange huyo dem keshakuwa wakooo....
Acha woga na wasiwasi
 
Mpeleke "Discussion" mtu mbili tu alafu fanya yako. Ukishindwa hapo ujue ndiyo humpati tena. Huyo anatafuta kitu kinaitwa "Friends with benefit" yani mnapigana marungu tu lakini hakuna "Feelings involved" hataki "any commitments" huyo.
 
Ligi ya miaka hii imetawaliwa na viungo(makuwadi) na mabeki(domo zege) kiasi kwamba vijana hawajui kabisa kua washambuliaji wenye uchu na goli inakuaje anaingia kwenye kumi na nane unashindwa kufosi goli aaaagghrrrr 😁😁 ungekua mdogo wangu makwenzi yangekuhusu nyambafu maana kesho akigongwa na mwenzie ndio mnajiuaga nyie.
 
hakua tayari kua wa wewe in a romantic way (mmekiss) but hisia zimempelekea huko.. mi nnadhani ni bint anae jielewa coz she knws what she wants ndo maana amekaa mbali nawe…
kwa upande wako talk to her in black en white aseme kama anakupenda na ukiridhika na majibu yake wait for her…
kuhusu kusalimiana na wanaume sometimes hyo ni tabia ya mtu tu unakuta yeye yupo social lakin kama unaona litakusumbua pindi mkiingia kwenye mahusiano mwambie apunguze
 
yaani wewe uko so outdated
umeshindwa kabisa kumsoma kabisa ..kwa ufupi we bado mshamba kulinganisha na huyo dada
 
Back
Top Bottom