G777
JF-Expert Member
- Aug 1, 2020
- 227
- 608
Hatuna tofauti chifu,Mapema Ningekupa kona.Kwa uzoefu wangu maranyingi ukimuomba msichana namba akakupatia halafu baadae unamtumia text anaishia kutizama tu hajibu hapo jua kabisa kuna vitu kadhaa vinamuongoza kufanya maamuzi hayo.
1. Hajapendezwa na muonekano wako. Wasichana wengi hasa hawa wa vyuoni hasa mwaka wa pili au wa tatu hawa wameshazoea kudanga na watu wenye hadhi fulani sasa ukienda wewe na ndala zako unalazimisha namba atakupatia lakini mwisho wake utakua ndo huo.
2. Huenda ndo kwaanza yupo kwenye penzi motomoto. Mara nyingi katika hatua hii msichana hua hana muda na hawa wanaoimba namba barabarani kwa sababu moja kwa moja hisia zake zitampeleka kwamba huyu anataka kunitongoza hivyo hatokupa ushirikiano ili kuepuka usumbufu na kupelekea kuleta shida kwa mpenzi wake.
CHA KUFANYA
Wewe endelea ku view status zake akiweka picha nzuri msifie akijibu muitikie huku ukichunguza reaction yake kama je! Ninaweza kuendelea na mazungumzo au hapana.
Akijirekodi kavideo chenye nyimbo nyuma yake reply mwambie nimeipenda hio nyimbo naomba nitumie. Akikutumia mwambie napenda sana nyimbo zenye mahadhi haya kama unazo baadhi tafadhari pia naziomba basi unatafuta na story ya kuungia taratibu.
Ila ningekua mimi kwa ninavyojijua ningesha Mmute mapema sana...
Sent using Jamii Forums mobile app