kingazi
Member
- Jul 4, 2011
- 35
- 7
nina rafiki mmoja anamchumba wake ambaye anampenda sana ila hakujua kama mchumba wake naye ana mpenda basi aliamua kumtega,kwanza alizima sim yake kwa muda wa wiki 1 kisha akaiwasha muda huo huo yule mchumba akapiga sim huku akimlaumu kwa kutopatikana basi jamaa akajib kwa upole kuwa yuko hospitalini kwani alipata jali iliyompelekea kupoteza faham siku 4 na sasa hiv amekatwa miguu yote hivyo hawezi tembea tena na akamuomba aje ili amsaidie basi yule mwanamke akamjib kuwa hawezi kumsaidia kwa hilo kwani hakuwa na mpango wa kuishi na mlemavu hapo wakakata mawasiliano lakini baada ya miezi 2 walikuja kukutana tena yule mwanamke akahamaki,jamaa akamueleza ukweli basi yule msichana anaomba msamaha na hata ndugu zake pia wanamuombea msamaha,sasa japo tunatakiwa kusamehe na huyu nae vipi?