Anaandika Shaffih Dauda kuhusu Mechi ya Simba ya leo

Anaandika Shaffih Dauda kuhusu Mechi ya Simba ya leo

Meja Jenerali Isamuhyo

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2017
Posts
3,126
Reaction score
9,661
◽️Jean Charles Ahoua
Aliuanza mchezo akiwa chini sana , licha ya kuwa ndiye mfungaji wa bao pekee hii leo sitashangaa kuona watu wakimsema ,alikuwa anakosa uharaka wa maamuzi na kujikuta unachelewesha movements

Tutakumbuka aliumia na kuomba kutoka , lakini bado atazibeba lawama kwa mpira alioshindwa kuumalizia dakika ya mwisho ya mchezo , pale unataka ufanye nini tena upo wewe na lango na mechi ni Nusu Fainali 🤔

◽️Joshua Mutale
Hadi sasa sishangai kwanini huwa hapati nafasi ya kuanza , leo Mwalimu Fadlu amechukua maamuzi magumu kwenye mechi muhimu kumpa dakika lakini bado ameshindwa kuonesha

Ukiacha shuti moja ambalo lilizaa kona ,Mutale hakuwa na hatari kabisa akiwa na mpira na hata akiwa hana mpira Simba ilikuwa kama ipo pungufu uwanjani.

◽️Leonel Ateba
Leo kwa mara ya kwanza naandika kuwa Ateba ni mshambuliaji wa kawaida sana, nimejiridhisha kwa kumtazama kwenye mechi za Ligi na hata Kimataifa.

Ameyakosea sana macho ya wanasimba waliotenga muda kuangalia Nusu Fainali waliyoisubiri kwa miaka mingi , tukio pekee jema kwake ni shuti moja ambalo liliishia kupanguliwa na golikipa , Mshambuliaji kweli pale hakuachi.

DIGALA was here
 
Ateba huwezi kulaumu Kwa muda alipata na alichokifanya
Ateba sio scorer mzuri ila anakimbia sana na anasumbua mabeki sana
Coach angeanza nao wawili Ateba na Mukwala
Mpanzu ni mchezaji hatari sana sema anacheza na manyumbu tu
Ahoua sijawahi kumwelewa Yuko slow mno anasubiri apige dead balls

Kibu anajitahidi ila Bado akili yake ni ndogo
 
Kwa kifupi Simba haina quality players. Huu ni ukweli wanaoukataa Wana simba.
 
Back
Top Bottom