Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi CPA Amos Makalla amesema uchaguzi mkuu mwaka huu utafanyika kwa mujibu wa katiba na sheria kama ilivyopangwa, hivyo hata watu wakichapisha (kupost) na kutuma ‘No Reform No Election’ haisaidii.
Makalla ameeleza hayo Juni 8, 2025 katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja Manyema Wilaya ya Moshi Mjini Mkoani Kilimanjaro akiendelea na ziara yake ya Kanda ya Kaskazini.
Akizungumza kujibu sekeseke linaloendelea katika mitandao ya kijamii Makalla amesema machapisho yanayochapishwa yakiandikwa ‘No reform no election’ hayana maana yoyote na haiwezi kuwa sababu ya kuahirishwa kwa uchaguzi.
"Kwahiyo hata yale yanayoendelea kwenye mitandao hata wakichapisha machapisho mamilioni na mamilioni ya ‘No Reform no election’ uchaguzi upo pale pale haisaidii we njoo tu weka pale tukiweka post weka(comment) haisaidii, uchaguzi hausogezwi utafanyika kama ulivyopangwa."
Makalla ameeleza hayo Juni 8, 2025 katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja Manyema Wilaya ya Moshi Mjini Mkoani Kilimanjaro akiendelea na ziara yake ya Kanda ya Kaskazini.
Akizungumza kujibu sekeseke linaloendelea katika mitandao ya kijamii Makalla amesema machapisho yanayochapishwa yakiandikwa ‘No reform no election’ hayana maana yoyote na haiwezi kuwa sababu ya kuahirishwa kwa uchaguzi.
"Kwahiyo hata yale yanayoendelea kwenye mitandao hata wakichapisha machapisho mamilioni na mamilioni ya ‘No Reform no election’ uchaguzi upo pale pale haisaidii we njoo tu weka pale tukiweka post weka(comment) haisaidii, uchaguzi hausogezwi utafanyika kama ulivyopangwa."