Amka Muafrika

Amka Muafrika

Mtuache

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2021
Posts
260
Reaction score
707
Habari za Viumbe wenzangu, poleni kwa kadhia mbalimbali. Wale mnaoteswa na mapenzi, siasa na uchumi, tambueni ya kuwa hamko peke yenu.

Naomba nianze na swali. Unafikiria picha aina maana yoyote katika maisha yako? Kiimani au hata kisaikolojia?

Unafikiri rangi ya Watu inayotumiwa kumchora Mwokozi wako au Mungu wako haijalishi na aina maana yoyote?

Huu ni mtihani wako.

Em jaribu hili zoezi dogo, funga macho yako kwa sekunde 10. Fikiria kuwa Yesu ni mtu mweusi au fikiria kuwa sura ya Yesu ni tofauti na picha ambazo umeziona maishani mwako.

Tayari ee? Jaribu na hili

Funga macho yako, na fikiria malaika weusi wamekuja kwako. Aidha kwa ndoto au wamekutokea mahala popote

Fikiria malaika Michael, Gabriel na wengine ni weusi.

Umejaribu?

Umeonaje? (nijibu kwenye koment)

Kuwa mwaminifu, usidanganye.

Hili ni jaribio la kisaikolojia.

Hivyo ndivyo akili yako ilivyopangwa na
Kutengenezwa kupitia picha.

Mchungaji mmoja aliwahi kuniambia jinsi shetani alivyomjia kwenye ndoto kama malaika wenye ngozi nyeusi na akamkemea, kwasababu alisema malaika lazima wawe Wazungu

.......Inaumiza sana.......

Kwa mfano malaika wakiwatokea, malaika wakiwa na rangi nyeusi za Kiafrika kama nyie wenyewe, nina hakika wengi wenu mtafunga, kuomba na kuwakemea mkidhani ni wachawi ama mashetani.

Nadanganya? Nikiwaita watumwa nitakuwa nakosea?

Yesu, malaika na manabii wote kuchorwa Katika rangi ya mkoloni haikuwa jambo la bahati mbaya, walifanya hivyo kwa makusudi ili waweze kuzitawala Akili zetu. Kwasababu Akili ya mwanadamu inaifadhi kila kitu Katika picha.

Baadhi ya Wakristo wa Kiafrika husema haijalishi Yesu ana rangi gani, lakini ndani yao wanafurahia kuwa yesu ni mzungu na ndio maana wasomi husema, mkristo mzuri ni MTUMWA mzuri wa Wazungu.

Lakini ngoja tusema haijalishi yesu ana rangi gani.

Sawa!

Ebu jaribu kuchora rangi ya Yesu na malaika weusi kwenye tisheti zenu, vitenge vyenu na kente zenu alafu uone jinsi Wakristo wenzako kutoka jamii zingine watakavyo kushanga, na kwa unyonge watawakubali kama wewe ulivyofanya bila kujua.

Akili hufanya kazi kupitia picha. wewe kwa ufahamu au kwa kutokufahamu upendo wa Yesu mweupe umekufanya kuwapenda wazungu wanao fanana na Yesu.

Waafrika tuna takiwa kukubali kwamba tumechezewa akili zetu, na Sasa ni wakati wa kuanza kujikomboa na kuzijenga upya Akili zetu ziwe timamu.

Wenye kunipinga nipingeni watakaokubaliana na mimi sawa lakini kauli yangu ni moja tu

Amka Mwafrika
InShot_20221006_181257530.jpg
 
Mbona kama naona mizimu tu
Ulishakuwa brain washed, huwezi kufikiri kama malaika wanaweza kuwa weusi waliovaa hivyo kama kwenye picha

Akili yako imeshaamini malaika ni weupe na mdo maana umesema hao ni mizimu.

Mizimu si jambo baya, lakini je? Kutaja kwako mizimu kulikuwa na maana ipi?

Viumbe waovu wenye kuleta dhambi, mauani, uchawi ambao kwa misingi ya ukristo na uislamu kuwa ni dhambi.

Au ulimaanisha mizimu kama viumbe waliokuwa msaada kwa mababu zetu kabla ya ukoloni, mzimu walioombwa kuleta mvua na mvua ikanyesha, walioombwa kutibu watu na watu wakapona..
 
There are so many imagined realities in this world ... Know em ... Understand em Shut the fuckup ... And evolve
 
Dini ni kitu fulani hivi cha kijinga kijinga ambacho watu wame kikumbatia sana kinacho pelekea wao kuwa wapumbavu .

Ways of mass control, Nimekuwa nikiipinga Sana dini ila Wacha ziendelee kuwepo .

Na zitaendelea kuwepo ... Bse they are the products of human mind..

Uchumi /Noti

Utawala/Mamlaka.

Dini

Those mentioned above mfs Have united the world than ever before , Controlling ... And they are still on the lane
 
yani wewe mwenyewe umeshindwa jitambua eti MUAFRICA hilo jina umeanzaje kulikubali na wametoa hao hao wazungu,kaka uwe unatulia tu kama mambo yamekuzidi sio lazima uyajue yaache ivyo ivyo sababu kwanza ww mwenyewe hujielewi.
 
Kwanni malaika wapo kama sisi tulivyo?? Kwa mimi sidhani, hata hizo picha ni imagination tu kua wako hivo.

Ila hiyo picha yako hapo juu inatisha mkuu, niwe mkweli wala sio mambo ya kua brainwashed kama unavyosema. Binafsi imenitisha
 
Back
Top Bottom