Hamna neno. Twende kazi sasa.
Ni kweli. Chochote chaweza kutokea kwenye siasa. Nani alidhani kwamba Obama angeisambaratisha Clinton machine mwaka 2008? Team Clinton walikuwa hata hawana plan beyond Super Tuesday. Wote tunajua kilichotokea baada ya hapo.
Nakumbuka mama baada ya kuangushwa Iowa alipoenda NH akalia. Unakumbuka ile?
And just an FYI, mwaka 2008 hakuna mtu aliyekuwa pro-mama zaidi yangu humu. Kama ukiweza utafute ule uzi wa uchaguzi wa mwaka 2008.
Ni kweli. Sisi [au kwa mahsusi nijiongelee mwenyewe] tunajadili tu kutoka kwenye mtazamo wa mbali.
Ngoja kwanza. Hivi Obama hiyo nafasi ya kugombea urais 'alipewa' tu au alichaguliwa na wanachama wa chama chake cha Democrats? Manake mi nijuavyo ni kwamba wagombea wanashindana kwa hoja mbele ya wanachama wao halafu wanachama ndo wanaamua wanamtaka nani kwa kupitia njia ya kidemokrasia, kupiga kura.
Sasa Obama alipewa hiyo nafasi? Ina maana tulikuwa tunadanganywa tu kuhusu mchakato mzima wa kumpata mgombea wa chama chao? Au unamaanisha nini unaposema alipewa?
Ni kweli. Mama aliteuliwa kuwa waziri wa mambo ya nje na akathibitishwa na Congress. Wadadisi wa mambo walikitafsiri kitendo kile kuwa ni cha kuleta maelewano kwenye chama chao baada ya mchuano mkali sana wa kumpata mgombea wao. Hivi unakumbuka kuwa ilifikia kipindi team Obama wakawa wanasema kwamba Bill Clinton ni racist? Hukumsikia Bill Clinton aliposema 'they played the race card on me'?
Unakumbuka jinsi mama alivyosema 'shame on you Barack Obama'?
Hebu bofya hiyo video ujikumbushe kidogo jinsi mambo yalivokuwa.
Well, mbona John Kerry sasa hivi ndo secretary of state na kwenye uchaguzi wa 2004 na alibwagwa na W? Kwa hiyo sidhani kama udhaifu ni hoja inayohusika hapa. Au pengine labda sijakuelewa?
Hiyo ya kufukuza watu si kwamba wanaofukuzwa ni watu wasio na hatia. Ni watu waliovunja sheria. Nitajie nchi ambayo huwa haifukuzi wahamiaji haramu? Kwa taarifa yako, kama ulikuwa hujui, hata Mexico huwa inafukuza wahamiaji haramu. Hata Tanzania.
Nadhani ikija kwenye wahamiaji haramu hata kura za maoni zinaonyesha kwamba majority ya Wamarekani wanaunga mkono sheria zifuatwe.
Halafu, narudia tena, kama kweli sera za GOP zingekuwa mbaya kama ambavyo unavyoamini au unavyodhani, basi kwa hakika hata huko kwenye ma governors mansions wangekuwa ni wachache sana kutoka kwenye hicho chama.
Lakini sasa hivi wao ndo wako wengi zaidi. Kwenye seneti nako wako wengi zaidi. Hata kwenye house of representatives wako wengi zaidi [ingawa unadai sijui huko walifanya ujanja ujanja].
Huduma nyingi za jamii kwa Marekani zinatoka kwenye local na state governments. Sasa kama kweli hao jamaa ni wabaya kihivyo inakuwaje wanatawala kwenye majimbo 31 kati ya 50? Dems sasa hivi wanashikilia majimbo 18 tu. How come?
Sawa, tutaona mwezi novemba. Siyo mbali kivile. Ila kumbuka tu kwamba chaguzi za Marekani huwa zinafuata mwenendo wa kupokezana. Kama sijakosea, katika karne iliyopita ni mara moja tu ambapo rais wa kutoka chama tawala alirithiwa madaraka na rais wa kutoka chama chake. Kwa kufuata mkondo huo wa kihistoria utaona basi kwamba mwaka huu GOP ni wao [ingawa kiuhalisia haina maana kwamba ndo watashinda].
Sawa, kama watu wanataka kadi za kijani kwa nini wasitumie taratibu za kisheria zilizopo? Kuna watu kibao ambao wako kwenye mstari wakisubiri zamu yao lakini kuna wengine wanaotumia njia mkato. Kuna haja gani sasa ya kuwa na sheria kama zilizopo hazifuatwi?
Hii ni kweli kabisa. Bush Sr. baada ya Desert Storm approval rating yake ilifikia sijui asilimia 91 au 92 mwaka 1991. Lakini mwaka ulofuatia akabwagwa.
Hahahaaaaa usije tu kuumwa ukiona electoral college votes hazitoshi hiyo jumanne ya kwanza ya mwezi novemba.
Tuombee uzima tu.
Naona umetumia muda wa kutosha kunijibu kwa kirefu.
Nashukuru kwa muda wako.
Nadhani siyo sehemu zote, tutaelewana, lakini ndiyo uzuri wa kuelimishana hapa. Kila mtu ana haki ya maoni yake.
Kuna vitu vingine unafikiria zaidi kupita kiasi. Nikisema Obama "amepewa" nafasi, simaanishi kuwa hajagombania kwa jasho lake, ila amepewa kura na wananchi. Wamemwona anafaa zaidi kuliko Hillary.
Naomba nikujibu kifupi kwa leo.
Magavana na viongozi wingine wanakuja na kuondoka. Wawe GOP au Democrats. Leo ni zamu ya GOP.
Obama kamchagua Biden kwa sababu kwa wakati huo, alikuwa hana uzoefu na siasa za kimataifa, DC politics bado hazijui kama Biden na alitaka swing votes katika majimbo ambae Biden anajulikana.
McCain kakosea step kumchukua Sarah Palin katika ticket. Uzee wake na ujinga wa Palin ulimponza. Pia, muda wa GOP ulikuwa umeisha. Watu wamewachoka.
Pia, kama ulivyosema, siasa inabadilika na kwenda kwa zamu. Mara Tembo, mara Pundamilia katika ofisi. Wakati wa Pundamilia ulifika, na watu walitaka kuona mabadiliko. Wakamchagua Obama.
Kuhusu watu kupinga "undocumented" folks, nakubali kabisa. Lakini inakuwa vigumu kuwafukuza wale waliozaa tayari.
Moja, ni huruma ya kibinadamu. Familia zitatengana.
Mbili ni siasa. Watoto wao ni wakubwa na raia kamili na wamejiandikisha kwa wingi kupiga kura. GOP wanataka wasio na haki waondoke kwa kuwa wengi kama wakipata haki ya uraia, watakuwa Democrats.
Tatu, uchumi unategemea hawa cheap labors. Siamini kama serikali haijui wanakaa wapi au wanashindwa kuwaondoa kwa nguvu. (Wana uwezo wa kunasa mawasiliano ya aina yote).
Wakiondolewa, wananchi wengi hawawezi kufanya kazi zao za kuchuma matunda, kusafisha vyumba vya hoteli na kulea watoto.
Walijaribu miaka ya nyuma lakini wanashindwa kupata wafanyakazi walipotangaza ajira za kilimo na mifugo katika magazeti ya Alabama na Iowa. Kazi ngumu, pesa ndogo.
Nne, wanasiasa wanapenda kuwatumia Illegals kama punching bags. Wanaonekana "tough" kwa wapiga kura. Lakini ikiisha kampeni, maisha yanaendelea.
Hamna urafiki katika siasa za huko. Watatumia njia yoyote kupata kura. Urafiki ni wa maneno tu. Kama strategist akisema tukifanya hivi, tutapata kura zaidi, wanasiasa wanafuata. Wakati wa mapambano ya kutafuta kura, wanapenda kuchafuana majina.
So, I am not surprised when Hillary said "Shame on you" to Obama while Obama camp called Hillary's anger as "tactical".
Leo marafiki, Hillary kapewa Uaziri na top campaign strategists wa Obama sasa wameajiriwa na Hillary.
Politics is a dirty game.
Nitaishia hapa kwa leo.
Tuendelee siku nyingine. Ahsante.