Ushauri uliotolewa 90% ni bidada uachane na jamaa ushituke, utakuwa nyumba ndogo, wengi tumehisi sababu alizotoa mchumba wako wa "kichaga" ni uongo ili asikuumize.
Kwenye uhalisia wewe unaeweza kufahamu zaidi sababu za yeye kuchaguliwa mke wa kichaga badala yako, nakumbuka hili swala pamoja na kuonekana kwa sasa ni upuuzi kijana kuchaguliwa mke lakini kwenye baadhi ya koo bado lipo.
Ndoa za sasa ambazo ni (za kidigitali) ambazo tunaenda kuwapa taarifa wazazi bila kuzingatia ushauri na maoni yao. Ndio hizi ambazo zina matatizo makubwa ndio hizi za nusu mwaka, ndio hizi za marioo, ndio hizi za mke mume mume mke.
Kuna fact nyingi zinazo weza kuwepo kati mazingira haya wazazi wasiporidhia mahusiano yenu pia ni tatizo, ingawa wengi wakati wa huu wa usasa tunalipuuza na baadae tunajuta. Nilicho kiona hapa wewe unaweza kuwa na mapungufu ambayo huyaoni lakini wazazi kwa kuhitaji kijana wao ayaishi maisha waliyo mkuza nayo wameyaona na sababu waliyoitoa ni ukabila (kitu ambacho kinapingwa lakini hufanya kazi kwenye utamaduni wa ndoa).
Jambo jingine ambalo nahisi pia 90% imekuonya ni wewe kuwa nyumba ndogo baada ya jamaa kuoa, swali hapa je wewe unaridhia kuwa nyumba ndogo ya "mchaga"? Ni kweli nyumba ndogo zitaisha? Ni kweli wanawake wote wataolewa? Au wote wanaoolewa ni bora? Kabla ya kukuamulia fanya mmeng'enyo wa yote kuanzia day one mlipo kutana mpaka siku aliyo kutamkia hilo then utapata jibu.
Ukiona unamudu mapenzi ya kuwa nyumba ndogo amua, ukiona vipi waambie wazazi wako wakusaidie kupata sifa za mwanaume atakae lingana na maisha waliyo kukuza wao. Ikiwezeka nawe rudi kwenye kabla lako.