Wapendwa wana jamii naomba nifike kwenu japo kwa neno la faraja na ushauri maana mpenzi wangu tumekuwa pamoja kwa muda wa miaka miwili sasa...takribani miezi miwili kuna siku nilimshauri tabia ya kupenda pombe kama mtoto wa kike kuwa si njema...si bia moja au mbili bali ile ya kulewa tirarira...sasa baada ya maneno hayo amenuna na wala hataki mawasiliano na mimi...wanajamii ushauri au hata neno la nini nifanye katika mazingira haya.