Amegundua vidonge vya ARV's chumbani kwa mpenzi wake

Ngaliba Dume

JF-Expert Member
Oct 6, 2010
1,710
3,669
Ni mshikaji wa muda mrefu!Tulifahamiana Tabora School(Boys) miaka iyooo.Tulipendana sana sbb 2likuwa tukiishi room moja,hata baada ya kumaliza tuliendelea na Elimu ya juu tena kwa Mafanikio makubwa. Jamaa yangu ni mtalaam wa i minara ya simu ktk kampun flani ya simu apa Tz,ana mpenz wake ambaye jamaa yng ana nia kabsa ya kuoa..uyu dada(shemej yangu)ni mkaguzi(Auditor)..."wanapendana sana"...lakn kama wiki imepta Mwanamke alpata likzo,akamua toka kwao kuja kukaa kwa rafk yngu kwa mda..ktk kipindi iki jamaa yangu aligundua ktk mkoba wa mpenz wake kuna "kadi",maelekezo na namna ya ku2mia vdonge vya kurefusha maisha,msichana hakuwah kumwambia jamaa wala ata sisi atukuwah kujua...japo kuna wakat walikuwa wanataka kwenda kupma ila mwnmke akawa relactant...jamaa anashndwa atamuanzaje mwanamke kumuliza mana alpekua tu mkobani bila ruhusa. Sabab mi n rakfye kanishrksha,jamaa kachanganyikiwa mpaka baadh ya kazi za kwenda kurekebsha minara watu wapate netwek kaziweka pending...yaan kachzka!TUNAFANYAJE?Mana mjini kushakuwa kuchungu..huzun yake n huzuni yangu! NAWASILISHA:
 
Kuwa muathirika sio mwisho wa maisha wanaweza wakaishi kama mume na mke na wakapata watoto hata kama mmoja wao ni muathirika, lakini hilo lazima iwe choice ya jamaa na kama yeye hataki kuoa muathirika basi asimwambie kama ameona ARV's bali amsisitize waende wakapime kabla ya kuendelea na mahusiano

By the Way umemaliza Boyz mwaka gani?
 
Thanx VoiceofReason nimekpata ushauri wako...nazd kujfunza!1990's ndo boyzia nimepta!vp na wewe mazngra ayo nin?
 
Wapo watakaouliza huyo jamaa yako alikuwa akitafuta nini kwenye mkoba wa mdada. Watasema kufukunyua fukunyua mikoba ya wadada ni kujirusha roho bure tu.

Binafsi naona mdada hakuwa 'forthcoming' kuhusiana na hivyo vidonge kama ni vyake au la. Inasikitisha lakini ndo hivyo tena, mtu utafanyaje sasa. Jamaa ni apige moyo konde, aongee naye apate kujua kinachoendelea halafu achukue hatua atakayoona inamfaa.

But I must confess, finding such pills in your lady's purse can be devastating....
 
Hapo sasa. Hili gonjwa ni balaa. Sasa mpaka anatumia dawa manake alishaugua huyo binti. Kwa kifupi ni muuaji angekuwa na upendo wa kweli angemwambia mwenzie ili kumnusuru who knows labda angejua mapema angepona. Lets hope jamaa hajaukwaa. Jamani nyie mlio single pimeni afya kabla ya kuingia kwenye mahusiano na si ndoa tu.
 
Wapo watakaouliza huyo jamaa yako alikuwa akitafuta nini kwenye mkoba wa mdada. Watasema kufukunyua fukunyua mikoba ya wadada ni kujirusha roho bure tu.

Binafsi naona mdada hakuwa 'forthcoming' kuhusiana na hivyo vidonge kama ni vyake au la. Inasikitisha lakini ndo hivyo tena, mtu utafanyaje sasa. Jamaa ni apige moyo konde, aongee naye apate kujua kinachoendelea halafu achukue hatua atakayoona inamfaa.

But I must confess, finding such pills in your lady's purse can be devastating....

And it will never be the same!!!!
 
Dah!..................kweli inachanganya sana...

1. Wewe kama rafiki wa karibu.......zidisha ukaribu kuliko mwanzo.............rafikio yupo kwenye shida kubwa sana.
2. Sina hakika kama walipoanza mahusiano walipima vvu kabla ya kujamiiana.....kwa hiyo hakuna wakumlaumu mwenzake
3. Kama ambavyo VOR amesema hapo juu,jamaa amshauri mwenzake waende kupima.............baada ya hapo.............watapa ushauri namna ya kuishi
4. Simshauri kumuacha kwa kuwa kama itaonekana tatizo wote wanalo.............na umesema wanapendana............si sahihi yeye kwenda kutafuta ambaye hajaathirika.......na kuendeleza maambukizi.
5. Kama ataamua kumuacha iwe kwasababu nyingine na si hii ya kuathirika................ajiulize angekuwa ni yeye yuko katikati ya mahusiano....halafu akajigundua ameathirika........angefanyaje?
6. Kuwa muathirika sio mwisho wa maisha...........ni mwanzo wa maisha ya kujitambua zaidi................endelea kumpa moyo.
 
Dah!..................kweli inachanganya sana...1. Wewe kama rafiki wa karibu.......zidisha ukaribu kuliko mwanzo.............rafikio yupo kwenye shida kubwa sana.2. Sina hakika kama walipoanza mahusiano walipima vvu kabla ya kujamiiana.....kwa hiyo hakuna wakumlaumu mwenzake3. Kama ambavyo VOR amesema hapo juu,jamaa amshauri mwenzake waende kupima.............baada ya hapo.............watapa ushauri namna ya kuishi4. Simshauri kumuacha kwa kuwa kama itaonekana tatizo wote wanalo.............na umesema wanapendana............si sahihi yeye kwenda kutafuta ambaye hajaathirika.......na kuendeleza maambukizi.5. Kama ataamua kumuacha iwe kwasababu nyingine na si hii ya kuathirika................ajiulize angekuwa ni yeye yuko katikati ya mahusiano....halafu akajigundua ameathirika........angefanyaje?6. Kuwa muathirika sio mwisho wa maisha...........ni mwanzo wa maisha ya kujitambua zaidi................endelea kumpa moyo.
Thanx mkuu for your talented advice...thats why i feel proud of JF!Siwez kumtenga,sitaweza!tumetoka mbali sana....na apa napokwambia na mpango nchukue ata likizo ata tuende Zenji kupumzka!...I wl take y advice in a seriously manner
 
Hapo sasa. Hili gonjwa ni balaa. Sasa mpaka anatumia dawa manake alishaugua huyo binti. Kwa kifupi ni muuaji angekuwa na upendo wa kweli angemwambia mwenzie ili kumnusuru who knows labda angejua mapema angepona. Lets hope jamaa hajaukwaa. Jamani nyie mlio single pimeni afya kabla ya kuingia kwenye mahusiano na si ndoa tu.

Nashindwa kumlaumu huyu dada kwa kuwa;
.........hatujajua kama walipima kabla ya mahusiano
.........hatuna hakika nani kamwambukiza mwenzake

Pengine..............walianza mahusiano blindly...........dada hajijui na kaka hajijui..............baadae dada kupima akajikuta kaathirika.........akajaribu kuvuta kumbukumbu zake za mahusiano ya nyuma............hakuwa anatumia kinga........hivyo akahisi labda yeye ndie chanzo na kuamua kufanya siri akihofia kuvunja mahusiano.....Kumbe labda kaka nae huko nyuma ndie aliye vibeba......

NB:Kuambukizwa si kwa njia ya ngono pekee.
Naomba nisilaumu yeyote hapa,hata kama yuko wa kulaumiwa,.....si wakati wake huu.....haitawajenga kuface tatizo.
 
Akapime/wakapime kama dada akikubali alafu akishapata majibu ndo aamue nini cha kufanya.

Inawezekana dada kambebea mtu tu akajisahau navyo.
 
pole sana kwa huyo kaka,kama huyo dada ni muathirika,kiukweli alikuwa na mapenzi ya kinafiki.mapenzi gani hayo ya kutokuambiana jambo kama hilo?kuogopa kuachwa?juu ya yote,ipo siku ingejulikana tu,kwa nini umuangamize mwenzio kimawazo{maana lazima ujihisi kuchanganyikiwa}mmmh,kuambukizana kimakusudi sio jambo zuri.mungu atamsaidia anaweza akawa negative,kikubwa akapime
 
Kweli nataka kuchangia ila namna yako ya kuandika kiswahili... haki naumia kichwa maana ni kama unaandika codes.
Nitarudi nikielewa kupitia ushahuri wa wengine.
 
Kweli nataka kuchangia ila namna yako ya kuandika kiswahili... haki naumia kichwa maana ni kama unaandika codes.Nitarudi nikielewa kupitia ushahuri wa wengine.
Pole sana RR...Haikuwa dhamira yangu wewe usiielewe hii thread...lengo la thread hii ni kupata ushauri kwa Wana-JF na wewe ukiwemo! Kutokuielewa thread sabab ya codes kumepnguza idad ya ushauri,ushaur wako ulikuwa muhmu sana,pengne endelea kufatlia utajielimisha na utanipa nasaha zako!POLE KWA KUKUWEKA KANDO KWA UANDSHI WA KISWAHL CHANGU (little I hv been addicted wth codes)
 
Kitendo cha binti kuficha kadi/vidonge kuna maanisha alikuwa muathirika toka mwanzo kabla ya uhusiano na jamaa yako na ameanza kumeza dawa baada ya CD count kushuka sana,pia inathibitisha amekuwa akienda kujuwa hali yake mara kwa mara.Hapa hamna cha ushauri wala kumung'unya maneno jamaa akapime kama ameathirika.Vyovyote atakavyokuta huyu mwanamke si wakuendelea nae.
 
Thanx mkuu for your talented advice...thats why i feel proud of JF!Siwez kumtenga,sitaweza!tumetoka mbali sana....na apa napokwambia na mpango nchukue ata likizo ata tuende Zenji kupumzka!...I wl take y advice in a seriously manner


Litakuwa jambo la busara sana..............mshauri naye aombe likizo ili peformance yake isishuke......................
Pia usimsisitize kwenda kupima kwa sasa.....................unahitaji kupata ushauri wa kumrudisha kwenye normal state kwanza..........
alafu ndio aanze kushauriwa kupima.....................
 
Litakuwa jambo la busara sana..............mshauri naye aombe likizo ili peformance yake isishuke......................
Pia usimsisitize kwenda kupima kwa sasa.....................unahitaji kupata ushauri wa kumrudisha kwenye normal state kwanza..........
alafu ndio aanze kushauriwa kupima.....................
Ballerina sikubaliani nawe kuhusu kuchelewa kupima,sehemu ya kupima ina washauri wazuri wenye utaalamu na pia kuchelewa kunazidi kumchanganya akili na anaweza kupima na kukuta hana.Kuna rafiki yangu walienda kupima yeye akakutwa anao na mpenzi wake hana na walikuwa hawatumii condom zaidi ya miezi sita ya uhusiano wao.
 
Halafu ikumbukwe kuwa ukimwi uligundulika nchini miaka ya 80 mwanzoni..................(uligundulika.....sio ulianza).

Kuna wale waliozaliwa miaka hiyo na wazazi waathirika...............ambao walizaliwa wameathirika..................................
Wapo ambao immunity zao ziko juu na wanaishi mpaka leo tena ni mabinti/wavulana wenye mvuto hasa.

NB:Si kila mvulana aliyetulia au msichana bikra hana maambukizi ya VVU............ni muhimu kupima kabla kuanza mahusiano.
 
Ballerina sikubaliani nawe kuhusu kuchelewa kupima,sehemu ya kupima ina washauri wazuri wenye utaalamu na pia kuchelewa kunazidi kumchanganya akili na anaweza kupima na kukuta hana.Kuna rafiki yangu walienda kupima yeye akakutwa anao na mpenzi wake hana na walikuwa hawatumii condom zaidi ya miezi sita ya uhusiano wao.

Kupima hata mahospitali ya binafsi yanapima....................ila kwa kutoa ushauri wengine hawana hata muda......utafikiri anakuambia ukapime malaria................nimemshakumbana nao kama mara mbili...................sipendi kuzitaja hizo hospitali.

Yaani unamwambia docta,mimi ningependa kupima na vvu..............anakuuliza tu "umewahi kupima".......unamjibu hapana......anauliza tena "kwanini unataka kupima" ....unajibu nataka kujua afya yangu.............anakwambi, "ok....nimekuandikia tayari.....watakupima"!.................hivi hapo kakushauri nini?

Mimi nilimaanisha apate ushauri nasaha ambao utamuweka sawa ndio akapime..............mara nyingi AMREF wako makini na wanawashauri nasaha wazuri sana.
Akikurupuka na kwenda private hospital, sitanii....tunaweza kumpoteza iwapo atajikuta ameathirika kwani atakuwa ameongeza stress.
 
Kupima hata mahospitali ya binafsi yanapima....................ila kwa kutoa ushauri wengine hawana hata muda......utafikiri anakuambia ukapime malaria................nimemshakumbana nao kama mara mbili...................sipendi kuzitaja hizo hospitali.

Yaani unamwambia docta,mimi ningependa kupima na vvu..............anakuuliza tu "umewahi kupima".......unamjibu hapana......anauliza tena "kwanini unataka kupima" ....unajibu nataka kujua afya yangu.............anakwambi, "ok....nimekuandikia tayari.....watakupima"!.................hivi hapo kakushauri nini?

Mimi nilimaanisha apate ushauri nasaha ambao utamuweka sawa ndio akapime..............mara nyingi AMREFU wako makini na wanawashauri nasaha wazuri sana.
Akikurupuka na kwenda private hospital, sitanii....tunaweza kumpoteza iwapo atajikuta ameathirika kwani atakuwa ameongeza stress.
Sio Amref tu hata Muhimbili kama yuko Dar au hospitali za Mkoa ua Wilaya ni kweli hospitali nyingi za binafsi hawaipi uzito swala la ushauri kabla na baada ya kupima.
 
pole sana kwa huyo kaka,kama huyo dada ni muathirika,kiukweli alikuwa na mapenzi ya kinafiki.mapenzi gani hayo ya kutokuambiana jambo kama hilo?kuogopa kuachwa?juu ya yote,ipo siku ingejulikana tu,kwa nini umuangamize mwenzio kimawazo{maana lazima ujihisi kuchanganyikiwa}mmmh,kuambukizana kimakusudi sio jambo zuri.mungu atamsaidia anaweza akawa negative,kikubwa akapime
Tusimlaumu huyu dada , labda alikuwa anasubiri muda muafaka kuongea na mwenzake!
 
Back
Top Bottom