Kingsmann
JF-Expert Member
- Oct 4, 2018
- 5,351
- 20,101
Amapiano ndio habari ya mujini kwa sasa kunako sekta ya burudani hasahasa kiwanda cha muziki. Kama Amapiano ni jina geni kwako basi sikiliza wimbo wa Mama Amina wa kwake Marioo ft Sho Madjozi na utakuwa umeshaelewa hapa nazungumzia aina gani ya muziki, hiyo ndiyo Amapiano kutoka bondeni kwa Wazulu.
AMAPIANO NI NINI?
Amapiano ni mtindo wa muziki wa "House" ambao chimbuko lake ni Afrika Kusini. Mtindo huu uliibuka Afrika Kusini mnamo mwaka 2012.
Amapiano (Piano kwa lugha ya Kizulu) ni mseto wa muziki wa deep house, jazz na lounge music wenye sifa ya synths, airy pads na basslines pana na za kupendeza.
Muziki wa Amapiano una sifa ya kipekee kwa kuwa na high pitched piano melodies, Kwaito basslines, low tempo 90s South African house rhythms na percussions kutoka aina nyingine ya muziki wa wenyeji(local) wa house unaoitwa Bacardi.
ASILI.
Ingawa aina hii ya muziki ilipata umaarufu katika mji wa Gauteng, kuna utata mwingi juu ya asili yake, na akaunti anuwai za mitindo ya muziki katika vitongoji vya Johannesburg - Soweto, Alexandra, Vosloorus na Katlehong.
Kwa sababu ya kufanana kwa aina hiyo na Barcadi, watu wengine wanadai aina hiyo ilianzia Pretoria na imekuwa mjadala wa kuendelea juu ya asili ya Amapiano.
UMAARUFU
Mwaka 2020 aina hii ya muziki ilipata kujiongezea umaarufu kote bara la Afrika na kuongezeka kwa digital streams na mafanikio ya kuingia katika chati za juu za muziki katika nchi mbalimbali tofauti na Afrika Kusini.
Tanzania.
Kwa sasa msanii aliyefanikiwa kutoa hit song ya miondoko hii ya Amapiano ni Marioo na ngoma yake ya Mama Amina akiwa amemshirikisha Sho Madjozi & Bontle Smith.
Wengine ni Amber Lulu na ngoma yake ya Shingapi, Damian Soul na ngoma yake ya Mapopo.
[/b]
AMAPIANO NI NINI?
Amapiano ni mtindo wa muziki wa "House" ambao chimbuko lake ni Afrika Kusini. Mtindo huu uliibuka Afrika Kusini mnamo mwaka 2012.
Amapiano (Piano kwa lugha ya Kizulu) ni mseto wa muziki wa deep house, jazz na lounge music wenye sifa ya synths, airy pads na basslines pana na za kupendeza.
Muziki wa Amapiano una sifa ya kipekee kwa kuwa na high pitched piano melodies, Kwaito basslines, low tempo 90s South African house rhythms na percussions kutoka aina nyingine ya muziki wa wenyeji(local) wa house unaoitwa Bacardi.
ASILI.
Ingawa aina hii ya muziki ilipata umaarufu katika mji wa Gauteng, kuna utata mwingi juu ya asili yake, na akaunti anuwai za mitindo ya muziki katika vitongoji vya Johannesburg - Soweto, Alexandra, Vosloorus na Katlehong.
Kwa sababu ya kufanana kwa aina hiyo na Barcadi, watu wengine wanadai aina hiyo ilianzia Pretoria na imekuwa mjadala wa kuendelea juu ya asili ya Amapiano.
UMAARUFU
Mwaka 2020 aina hii ya muziki ilipata kujiongezea umaarufu kote bara la Afrika na kuongezeka kwa digital streams na mafanikio ya kuingia katika chati za juu za muziki katika nchi mbalimbali tofauti na Afrika Kusini.
Tanzania.
Kwa sasa msanii aliyefanikiwa kutoa hit song ya miondoko hii ya Amapiano ni Marioo na ngoma yake ya Mama Amina akiwa amemshirikisha Sho Madjozi & Bontle Smith.
Wengine ni Amber Lulu na ngoma yake ya Shingapi, Damian Soul na ngoma yake ya Mapopo.
[/b]