PostGE2025 Amani yatawala Singida licha ya tishio la maandamano

PostGE2025 Amani yatawala Singida licha ya tishio la maandamano

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

PAYE

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2025
Posts
354
Reaction score
395
Licha ya kuwepo kwa taarifa na tetesi za uwezekano wa kutokea maandamano katika maeneo mbalimbali nchini, hali ya amani imetawala katika mji wa Singida, huku shughuli za ulinzi na usalama zikiimarishwa katika maeneo yote muhimu.

Hata hivyo, uchunguzi uliofanyika mapema leo katika mitaa ya mji wa Singida unaonyesha kuwa baadhi ya wafanyabiashara hawajafungua maduka yao wakisema wanachukua tahadhari kutokana na taarifa hizo, ili kuepusha hasara iwapo kutatokea vurugu au uvunjifu wa amani.

Aidha, imebainika kuwa vituo kadhaa vya mafuta vimefungwa, hatua inayodaiwa kuchukuliwa kwa tahadhari ya kuangalia mwenendo wa siku nzima. Baadhi ya madereva walionekana wakizunguka kutafuta huduma katika maeneo mbalimbali ya mji bila mafanikio, jambo lililosababisha msongamano mdogo katika vituo vilivyoamua kuendelea na shughuli.

 
Hivi maandamano ni tishio?

Kama ni tishio kwanini yamekubaliqa kikatiba?

Ikiwa hakuna namna yeyote ya kuwawezesha wananchi kuwasilisha mawazo yao kwa yale wasioyapenda kwenye nchi yao. Je tunaweza kudhani kwamba tupo huru?
 
Singida hali ni shwari wananchi wanaendelea na shughuli zao kama kawaida hakuna vitendo vya uvunjifu wa amani.
 
Wamepuuza ushauri wa serikali, maana walisema kama huna dharura ukae ndani😏
 
Singida hata ile 29 Oktoba, Ukikaa na Wanyampaa unawaambia Mwanza, Dar, Arusha kuna moja mbili tatu wanakushangaa kabisa vijana wanapiga visungura sana na wanapenda kugongea vibaya mnoo
 
Back
Top Bottom