Ni dhahiri ya kwamba ccm na serikali yake vimeshashindwa kazi. Na leo hii tumemsikia Dr wa ukweli Slaa akimjibu Tendwa ya kuwa hili swala liko tayari kwenye vyombo vya sheria, pale Tendwa alipotaka CHADEMA ijieleze kwa maandishi kuhusu 'kuleta vurugu' kunakodaiwa na ccm na vikaragosi vyao. Bado tuna mwendo mrefu sana mpaka haki ya mwananchi inayopiganiwa na CDM itakapopatikana. Lakini safari imeshaanza, hakuna kurudi nyuma mpaka kieleweke.
Poleni sana makamanda, lakini penye ukweli kila siku uongo hujitenga!
People's Power!