HALELUYA MOSHI
JF-Expert Member
- Aug 14, 2014
- 2,121
- 1,206
Kumbe unakubali kuna baadhi ya makosa yamesababishwa na Lowassa, sasa kama kuna ufisadi anahusika unapata wapi ujasiri wa kumtetea.
Sawa tumeichoka ccm, na waliosababisha ccm ichokwe ni Pamoja na Lowassa na genge lake.
Leo anapata wapi uhalali wa kuwania urais ikiwa faili lake Lina makando kando yasiyo na majibu?
Na mkijitaidi kijibu mnasema Mbona ufisadi haukuisha hata pale alipoondoka .
Hivi toka lini kosa likafutwa kwa kosa.?
Kwenye mikutano yenu fanyeni haya halafu urudi tena hapa JF:
1. Msitumie malori kusafirisha watu
2. Msiwatangulize jukwaani akina daimond na ze komedi!
Unajua hawa jamaa wa CCM wanafurahisha sana. Jana kwenye mkutano wamegombana kwelikweli. Kisa kuna wengine hawakupewa T-shirt na kofia. Yaani mambo mengine yanatia hata kichefuchefu kuyasikia. Naamini shida yao sio hizo T-shirt ila nikuonekana kwamba nao ni makada. Halafu jana hiyo nikasikia kuwa walishindwa kupata uongozi wa CCM kwa sababu kila mtu alitaka kuwa mwenyekiti. Wameshikana masharti na kununiana.
Kilichoniuma roho zaidi ni pale nilipomuona Juma Pinto na jamaa zake wakiwa mbele kwa mbele na T-shirt za CCM wakijidai makada wa kutupa wakati Mbowe alipokuja kufungia Tawi la CHADEMA hawahawa ndio waliokuwa wanambebea breafcase na kumwambia kila kitu kipo sawa. Na walijifanya CHADEMA wa kutupa, kumbe walikuwa wanatafuta ngawila tu. Jamani njaa hadi London?!
Asante sana!
Lowasa ni mmoja kati ya mafisadi hatar waliofanya ccm ichokwe! ! ! Unaweza kuwa uko sahihi! !
Hao wengine wako wapi? (hiv tunavoongea)
Hebu tufanye lowassa kaenda monduli kupumzika! !
Kina tibaijuka wako wapi?
Chenge yuko wapi?
Wengine wale hatar 10 wako wapi?
Hawa ni watu wa chama gani?Kwenye mikutano yenu fanyeni haya halafu urudi tena hapa JF:
1. Msitumie malori kusafirisha watu
2. Msiwatangulize jukwaani akina daimond na ze komedi!
Unaposema watanzania wachache.....je, hao wachache watampa kura za ushindi!
Kubali kataa Lowassa rais 2015!
View attachment 287752
Hao ni Akina nani.?
View attachment 287752
Hao ni wana mabadiliko, tuonyeshe malori mengi
yenye kokoto hata 5 tu sababu nyie mlisomba zaidi ya lori 30. CDM hakuna kokoto
Kwenye mikutano yenu fanyeni haya halafu urudi tena hapa JF:
1. Msitumie malori kusafirisha watu
2. Msiwatangulize jukwaani akina daimond na ze komedi!
1. Kwani CHADEMA hawatumii malori/hawabebi watu?
2. Kwani CHADEMA/UKAWA hawatumii wasanii?....Hawa akina Ney wa Mitego...Bob Junior...Wolper..Shamsa Ford sio wasanii?...
Pamoja na Kujiandaa Kuchukua nchi kwa zaidi ya miaka 25.
Pamoja na kuwanunua aslimia kubwa ya wahariri na waandishi wa kawaida wa vyombo vya habari
Pamoja na kuwanunua robo tatu ya wajumbe wa kamati kuu hadi kufikia hatua ya kumzomea Mwenyekiti.
Pamoja na kuvinunua vyama vikubwa vinne vya upinzani na yeye akiwa ndio mgombea pekee.
Pamoja na kumiliki mtandao mpana zaidi na wa hatari nchini Mafioso & Mafisadi Unity (MMU)
Lakini bado anaonekana kupwaya kwa Magufuli,alieanza harakati za urais juzi ,tena hana mtandao ,hana vyombo vya habari vya kueleweka hata ule mtandao hatari Mafioso & Mafisadi Unity (MMU) unamwogopa na kumwangalia kwa jicho la tatu.!
Magufuli usikate tamaa ,watanzania wachache wenye uelewa na nchi yao wanatambua juhudi zako.!
Ingekuwa urais unapatikana kwenye mitandao basi Lowasa angekuwa rais,lakini bahati nzuri wapiga kura asilimia kubwa ni wale ambao hawajawahi kutumia mtandao
Mkuu hoja sio wasanii,Mbona na nyie mnatumia Chopa Kama kivutio.
Ukweli ni kwamba Lowassa anapwaya kwa Magufuli Pamoja na mtandao hatari alionao.!
2010 Dr.Slaa angekua Rais wa Tanzania, na kwenye mitandao ccm haijawai kushinda ila Mwisho Siku wengi wetu huduwaa.!