VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Siyo vizuri kabisa yaani. Mgombea wa Ubunge wa CHADEMA/UKAWA Jimbo la Busanda, Alphonce Mawazo anachachafya CCM mkoani Geita na hata kumshtua/kumtisha Dr. Magufuli anayetokea mkoa huo. Taarifa nilizonazo ni kuwa Mawazo anatamba mkoa mzima wa Geita. Anasingizia kuwa kwakuwa yeye ni Mwenyekiti wa CHADEMA Geita anapaswa kutamba mkoa mzima ili kuzoa majimbo yote ya Geita.
Si vyema kabisa. Dr. Magufuli anapata wasiwasi wa kasi na kukosa utulivu. Anashambuliwa nyumbani kwake. Ashindwe mkoani mwake kweli!? Anabanwa mbavu hata jimboni mwake na huyu Mawazo wa CHADEMA. Mawazo, kumbuka ulikuwa CCM. CCM ilikulea na hata kukupa Udiwani kule Arusha. Mbona hukumbuki kulipa fadhila? Ndiyo shukrani ya punda hiyo? Wewe ungetulia tu jimboni mwako Busanda na kujipigia kampeni. Ingetosha. Si kutetemesha na kutisha. Majimbo mengine waachie wenyewe.
'Kamanda' Mawazo, punguza sifa. Au nije? Tupe nafasi ya kula nanasi bwana!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Si vyema kabisa. Dr. Magufuli anapata wasiwasi wa kasi na kukosa utulivu. Anashambuliwa nyumbani kwake. Ashindwe mkoani mwake kweli!? Anabanwa mbavu hata jimboni mwake na huyu Mawazo wa CHADEMA. Mawazo, kumbuka ulikuwa CCM. CCM ilikulea na hata kukupa Udiwani kule Arusha. Mbona hukumbuki kulipa fadhila? Ndiyo shukrani ya punda hiyo? Wewe ungetulia tu jimboni mwako Busanda na kujipigia kampeni. Ingetosha. Si kutetemesha na kutisha. Majimbo mengine waachie wenyewe.
'Kamanda' Mawazo, punguza sifa. Au nije? Tupe nafasi ya kula nanasi bwana!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam