Aliyeshindwa ubunge kuvunja chungu

Aliyeshindwa ubunge kuvunja chungu

Ngongo

Platinum Member
Joined
Sep 20, 2008
Posts
21,198
Reaction score
37,526
Uchaguzi mdogo umemalizika mgombea XYZ kashindwa kunyakua ubunge baada ya kumwaga mifedha kibao,alianzisha vikundi vya vijana na kina Mama fedha zilitolewa kwaajili ya kuanzisha miradi ya kiuchumi,alitoa viroba vya unga wenye njaa wakapona na njaa zao,alitumia karata ya ukabila haikufua dafu.Iweje kura hazikutosha hakuna namna lazima chungu kivunjwe wale wote waliotafuna fedha za mgombea na kura hamkutoa jiandaeni kupuputika kama majani makavu.

Haiwezekani mtafune fedha za mgombea XYZ halafu kura mkampigie mgombea ABC hakuna namna safari hii lazima mkomeshwa mjifunze kutunza ahadi mchana hadi usiku. Mifuko iliyojaa unga mlichukua ili mpate nguvu za kupiga kura bila makosa wengine hamkufika hata vituoni kupiga kura maana yake nini kama si dharau wakati wa kukomesha tabia mbaya ya kula vya watu bila fadhila wala uchungu ndio huu.

Tangazo hili ni sehemu ya taarifa rasmi kabla chungu hakijavunjwa wale wote walioshiriki kutafuna fedha na mgombea heshima wajitokeze watubu,wajiapize kutokurudia tena makosa yao yasiyosameheka.Mji umetaharuki wapiga kura wanapenda maisha yao kitisho cha kuvunjwa chungu kimewatia kiwewe X-MASS na Mwaka mpya si muhimu tena nguo hazinunuliwi,mbuzi wa sikukuu hanunuliwi kwa hofu ya kufanywa kitowewo cha misiba.

Yarabi tunusuru maisha yetu yapo hatarini.

Nawasilisha.
 
mbona unatuficha ni wapi huko.
kama ni arusha alikosea angewachinjia mbuzi na pombe wangempa kura lakini hela ya maendeleo hawajui zaidi ya pombe
 
John D na Monaban wameahidi kuvunja vyungu,
nawashauri wavunje kabisa vile vyungu pori.
 
Moshi tulishasahau siku nyingi. Ila kama fedha aliyotoa ilipatikana kifisadi, chungu kitaanza na yeye!
 
Preta atusaidie akupata kiroba cha unga kweli maana nasikia wamama ndio waliwezeshwa zaidi.Mungu apendi rushwa hivyo akivunja hiyo chungu inaweza mrudia yeye,bora apoe na kuanza maisha upya,hila mbona nasikia huyo XYZ alienda kufungua kesi ya kupinga matokeo inasememekana kuna gari ilikuwa na kura ikatoroshwa fasta maajabu haya zuga zuga tu hiyo,imekula kwakee kwisha kwisha kwisha kabisa.
 
Wachaga/watu wa Arusha huwawezi, mlimuweza tu Yule wa geita ila wachaga wenyewe ni ma mafia
 
Sie wengine wageni hapa, kuvunja chungu ndio nini? kwanza wengi siku hizi wanatumia sufuri
 
Kuvunja Chungu ni Ibada ya matambiko ya kimila ya jamii nyingi za kiAfrika zikilenga kutanzua tatizo au kulipiza kisasi bada ya kufanywa jambo/mambo ya uonevu.

Sie wengine wageni hapa, kuvunja chungu ndio nini? kwanza wengi siku hizi wanatumia sufuri
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom