Aliyesafirisha twiga atoweka

Aliyesafirisha twiga atoweka

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
GIZA nene limetanda juu ya mahali alipo mshitakiwa namba moja katika kesi ya kusafirisha wanyama hai nchini Qatar, Kamran Ahmed.

Mshtakiwa huyo jana alipaswa kuwepo mahakamani ambako inasikilizwa kesi yake lakini hakutokea kwa mara ya tatu.
Juzi kesi hiyo iliyopo mbele ya Hakimu Mkazi, Simon Kobelo, iliahirishwa baada ya mshitakiwa huyo kutotokea mahakamani bila taarifa yoyote.

Wakili wa Ahmed, Edmund Ngemela na wadhamini wake nao hawakutokea hivyo mahakama ilitoa hati ya kukamatwa mshitakiwa huyo.

Hata hivyo licha ya mahakama hiyo kutoa hati ya kukamatwa kwa mshatikiwa huyo, jana pia Ahmed hakufika mahakamani bila taarifa zozote.

Kutokana na mshtakiwa huyo kutofika mahakamani hapo kwa mara ya tatu, upande wa mashitaka ukiongozwa na wakili wa serikali, Evetha Mushi, ulidai unafuatilia anwani za wadhamini wake.

Mushi, alidai wadhamini hao hawafiki wala kutoa taarifa mahakamani juu ya mtu waliyemdhamini.
Hakimu Simon Kobelo, aliiahirisha kesi hiyo hadi Aprili 17, mwaka huu na kama mshtakiwa Kamran Ahmed, atakuwa amepatikana itaanza kusikilizwa mfululizo Mei 6 na Mei 7.

Ahmed na wenzake watatu Martin Kimath, Michael Mrutu na Hawa Mang'unyuka wanadaiwa kusafrisha wanyama hao hai Novemba 26, mwaka 2010 kwenda Qatar kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Wanyama wanaodaiwa kukamatwa maeneo ya Mto wa Mbu, Elboret na Engaruka Wilaya ya Monduli mkoani Arusha .

Chanzo: Tanzania Daima la leo (26/3/2014)
 
Hii ndio Tanzania yetu kila mtu anafanya atakavyo.....Acha jamaa asepe
 
Hiyo ndiyo tanzania!!!rushwA kama kawaida mpakistani anakula bata sasa.Cha ajabu waliompa passport hawatakamatwa
 
Labda alikuwepo kwenye ndege ya Malaysia
 
Ukiona hivi, basi ujue mnyororo ni mrefu, haiwezekani nchi yenye serikali inayotangaza "utawala wa sheria" kila kukicha kuchezewa kwa kiwango hicho, yatakuwa yaleyale ya gorofa 18 karibu na state house, usikute kapelekwa Marekani kubadilishwa sura
 
nakumbuka enzi za Balali wa BOT
Na jinsi Akasha alivyotokomea........
i love TZ,
 
huyo mtu aliyeshtakiwa aliletaje au aliruhusuje ndege ya kivita kutua Tanzania na kupakia Twiga.

Naombeni hiyo kesi ifutwe tuendelee na mambo mengine
 
Kinachonifurahisha kwa watz na nchi hii ni kuwa mtu hata akipewa hesabu za 1+1=? na kushindwa, badala ya kufikiri zaidi utasikia "hii tunamuachia Mwenyezi Mungu"! Hapo sijui akilietewa zile hesabu za 2x + y/z = ? atamwachia nani..!?
Mshitakiwa hawezi kutoweka hivi hivi bwana na huu ni ushahidi mwingine kuwa wengi wa walioko jela hawakupaswa kuwepo wakati wanaostahili kuwepo ndio hivi wanatambaa mitaani!
 
Jamani sijui nanyie huwa linawatokea yaani kila nikiwangalia viongozi wa hii nchi kwenye luninga huwa nasikia kichefuchefu sijui kwa nini.
 
Jamani sijui nanyie huwa linawatokea yaani kila nikiwangalia viongozi wa hii nchi kwenye luninga huwa nasikia kichefuchefu sijui kwa nini.
Yani hata mimi utafikiri ni mwanamke mwenye mimba changa
 
GIZA nene limetanda juu ya mahali alipo mshitakiwa namba moja katika kesi ya kusafirisha wanyama hai nchini Qatar, Kamran Ahmed.

Mshtakiwa huyo jana alipaswa kuwepo mahakamani ambako inasikilizwa kesi yake lakini hakutokea kwa mara ya tatu.
Juzi kesi hiyo iliyopo mbele ya Hakimu Mkazi, Simon Kobelo, iliahirishwa baada ya mshitakiwa huyo kutotokea mahakamani bila taarifa yoyote.

Wakili wa Ahmed, Edmund Ngemela na wadhamini wake nao hawakutokea hivyo mahakama ilitoa hati ya kukamatwa mshitakiwa huyo.

Hata hivyo licha ya mahakama hiyo kutoa hati ya kukamatwa kwa mshatikiwa huyo, jana pia Ahmed hakufika mahakamani bila taarifa zozote.

Kutokana na mshtakiwa huyo kutofika mahakamani hapo kwa mara ya tatu, upande wa mashitaka ukiongozwa na wakili wa serikali, Evetha Mushi, ulidai unafuatilia anwani za wadhamini wake.

Mushi, alidai wadhamini hao hawafiki wala kutoa taarifa mahakamani juu ya mtu waliyemdhamini.
Hakimu Simon Kobelo, aliiahirisha kesi hiyo hadi Aprili 17, mwaka huu na kama mshtakiwa Kamran Ahmed, atakuwa amepatikana itaanza kusikilizwa mfululizo Mei 6 na Mei 7.

Ahmed na wenzake watatu Martin Kimath, Michael Mrutu na Hawa Mang’unyuka wanadaiwa kusafrisha wanyama hao hai Novemba 26, mwaka 2010 kwenda Qatar kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Wanyama wanaodaiwa kukamatwa maeneo ya Mto wa Mbu, Elboret na Engaruka Wilaya ya Monduli mkoani Arusha .

Chanzo: Tanzania Daima la leo (26/3/2014)
Qatar tena... hiyo ndo ntoleee ndo maana nami nikipataga nafasi ya kupiga nabutua tu
 
Hii inajaza hasira kwenye mioyo yetu sisi wazalendo. Ilikuwa ya rada, mhindi kala kona but anamiliki mtaa london knyuma tu ya zilipo ofisi za waziri mkuu. Akaja balali naye kazikwa akingali hai. Sasa huyu nae! Aghrrrrrr! Kwani nini maana maana ya kuwepo kwa mawizara ya sijui usalama wa taifa na mengineyo? Ipo siku isiyo na jina atazaliwa idd amin ambaye ataitawala nchi hii na ili aonyeshe kukubaliwa ataanza kuchimbua visiki hivi vya miiba ikasirishayo! Watawala zidisheni kutulimbikizieni hasira tu.
 
Kweli CCM na vyombo vyake vya dola vinawaona na kutambua kuwa watanzania ni wajinga,ni kama uongozi wa Rage wa Simba na wanachama!!! Kibali cha dege la jeshi kutua pale KIA pia alietoa hajulikani?! Wizara ya ulinzi pia haikufahamu ujio huo wa dege?! Foreign and internal affairs je??!! Kweli awamu ya nne hawakula tu bali wamekomba!!
 
Inakuje mtu mwenye kes nzito kama hiyo apokonyw passport.KOd zetu zinatumika kuwalipa mishahara watu wasojua majukumu yao.KAMA AYUPO NNCHN ALIONDOKAJE BILA VIBAL,rudisen twiga wetu na pia rudishen iman yenu kwa wananch kwa kuwajibishana wote walohusika
 
Back
Top Bottom