Aliyekuwa mkuu wa majeshi akamatwa

sulphadoxine

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
2,257
645
Aliyekuwa mkuu wa majeshi wa Guinea amekamatwa kufuatia shambulio lililofanyika nyumbani kwa Rais Alpha Conde kwenye mji mkuu, Conakry.
Mke wa Jenerali Nouhou Thiam alisema mume wake alichukuliwa saa chache baada ya shambulio hilo.
110719084349_alpha_conde_president_guinea_304x171_getty_nocredit.jpg
Rais Alpha Conde


Bw Conde ambaye alikuwa nyumbani kwa wakati huo ametoa wito wa kuwepo na utulivu.
Takriban mtu mmoja amefariki dunia.
Sehemu kadhaa za makazi ya rais ziliharibiwa baada ya kushambuliwa na silaha kali mapema Jumanne asubuhi.
Bw Conde aliingia madarakani katika uchaguzi uliofanyika Desemba iliyopita, baada ya utawala wa kijeshi uliodumu miaka miwili nchini humo.

 
Back
Top Bottom